Ufaulu mwisho iwe Division 3

Ufaulu mwisho iwe Division 3

Serikali itoe agizo kuwa wenye Divion 4 wasiruhusiwe kuendelea na elimu katika mfumo rasmi, warudie mitihani au wasiendelee na masomo kabisa
Kidato gani unazungumzia? maana form four div 4 huendelei mbele labda vyuo vya kati, lkn form two ukiwa na D mbili umepita au C moja unaenda form three
 
Fafanua kisomi maana sijakuelewa. Kwamba Div 4 hana uwezo kabla na baada ya kumaliza masomo yake ya juu au una jambo lingine limekutuma kihisia. Ukitumia mifano iliyo hai kama shuhuda itafaa kulinda hoja yako.

Kwani naamini ukipeleka hoja yako mbele ya taasisi za kusimamia mifumo ya elimu kama TCU, NECTA, NACTE, n.k.... hawataweza kukusikiliza na kama ni mhitimu wa ngazi ya chuo huenda unaweza kunyang'anywa uthibitisho wa elimu yako.

Kwako mtoa mada tafadhali, Tulia eleza kipi kimekupata.
 
Vyuo vina ngazi kama certificate, diploma, degree na kuendelea....!!! Au acha tu niishie hapa.
 
Serikali itoe agizo kuwa wenye Divion 4 wasiruhusiwe kuendelea na elimu katika mfumo rasmi, warudie mitihani au wasiendelee na masomo kabisa
Mwenye SHIBE hamkumbuki mwenye NJAA. Mtihani ni mmoja nchini nzima lakini mazingira ya kujifunzia tofauti. Hivi unampima Mwanafunzi wa FEZA SCHOOL na mwanafunzi wa kijijini while haina Library wala Maabara kwa mtihani ule ule? Mfano halisi Serikali imeweka SPECIAL Schools na Shule za kata, je mazingira ya kujifunzia yapo sawa. Special school wana soma hadi usiku, shule ya kata mwisho saa name nyumbani. Nenda mwenye Special school kaangalie miundombinu ukarabati tu 500 milioni, ofisi za kutosha, na nyumba jirani na shule. Shule za kata darasa halina sakafu, walimu hawana ofisi na hakuna nyumba ya mwalimu hata moja. Jiulize kwanini serikali inatenga wanafunzi hawa bora hawa sio bora, hawa mazingira mazuri, hawa mabovu? Labda kwa sasa kwa madarasa mapya ya Samia lakini kabla ya hapo hali ilikuwa mbaya sana. Mw Fikiria kuhusu Tanzania nzima sio sehemu moja ya Tanzania utaona hali ilivyo mbaya. Ndugu ELIMU na KUELIMIKA sio kufaulu mtihani kwani hata ukiiba utafaulu. ELIMU ni kupata UJUZI na KUELIMIKA ni kutumia UJUZI uliopata ipasavyo kwa kufanya mambo sahihi kwa wakati sahihi na kwa watu sahihi ikiambatana na maadili ya UJUZI wako. Ufaulu wa mtihani sio kipimo cha UJUZI, UJUZI hauandikwi UNATENDWA.
 
Kweli mkuu yani ni upumbavu ulioje mtu anapata div four kisa ana vi D vinne anaenda kusoma clinical medicine au engineering...
Unakuta mgonjwa alifaulu vizuri biology kuliko daktari..

Kikawaida mtu akipata D uwezo wake kwenye somo husika ni mdogo kuliko kawaida mwenye D na F hawana utofaut
 
Dr.Harison, Prof. Paramagamba, Mh. Mbowe, Dr. Hangaya, na wengine wengi...walipata Division ngapi...?

Kama ni 3, 2 au 1 mbona hawana.......
images%20(6).jpg
 
Kweli mkuu yani ni upumbavu ulioje mtu anapata div four kisa ana vi D vinne anaenda kusoma clinical medicine au engineering...
Unakuta mgonjwa alifaulu vizuri biology kuliko daktari..

Kikawaida mtu akipata D uwezo wake kwenye somo husika ni mdogo kuliko kawaida mwenye D na F hawana utofaut
Sasa biology ndo udaktari...
Una kichwa Empty sana...


Anayehudumia mgonjwa ni Nurse co au lab na ana leseni ya kumhudumia mtu....
 
Elimu ya lazima iwe mpaka kidato cha nne. Uko form 2 mwanafunzi arudie mpaka afike form four. Kisha baada ya hapo kuwe na mchuzo mzuri waende vyuoni na Advanced level wale tu ambao wamefanya vizuri. Kujazana wanafunzi vyuoni wakiwa na D zao hizo mara nyingi ni hasara.
 
Serikali itoe agizo kuwa wenye Divion 4 wasiruhusiwe kuendelea na elimu katika mfumo rasmi, warudie mitihani au wasiendelee na masomo kabisa
Hao wa Div 1 ukiondoa hizo A zao kuna kitu cha ziada walicho nacho? Mfano unaweza mchukua mwanafunzi kapara Div 1 umuweke mtaani asurvive? Mdio mnajidanganya kwamba ukipata Div 1 basi una akili ya kuubda hata chombo cha kwenda mwezini
 
Back
Top Bottom