Ghost MVP
JF-Expert Member
- May 19, 2022
- 440
- 740
Usipakue 'APP' Isiyokuwa Rasmi, katika Vifaa vyako kama Compyuta na Simu
Wapo wanaopakuwa App kutoka katika Tovuti zikisema zitawasaidia Kusafisha simu, kuweka muonekano mzuri wa Simu, App hizo hutumika kama Nyenzo ya kudukua kifaa cha Mtu huyo pasipo yeye kujua.
Zinamtaka mpakuaji kuipa APP hiyo ruhusa ya kufikia Taarifa za Simu Ulizopiga na kupigiwa, Hifadhi ya simu, Kujua app ulizonazo katika simu na hata Kufanya mabadiliko katika kifaa chako, Hivyo mdukuzi anaweza Kupata Taarifa zako bila wewe kujua na Kuchukua anachohitaji kwenye simu yako.
Wengi huwa na App za Kifedha hivyo mdukuzi huweza kupata taarifa zote hata kujiamishia Fedha pasipo mhusika kujua na Huweza kufuta kila kitu kwenye simu yako pasipo muhusika kujua.
Wapo wanaopakuwa App kutoka katika Tovuti zikisema zitawasaidia Kusafisha simu, kuweka muonekano mzuri wa Simu, App hizo hutumika kama Nyenzo ya kudukua kifaa cha Mtu huyo pasipo yeye kujua.
Zinamtaka mpakuaji kuipa APP hiyo ruhusa ya kufikia Taarifa za Simu Ulizopiga na kupigiwa, Hifadhi ya simu, Kujua app ulizonazo katika simu na hata Kufanya mabadiliko katika kifaa chako, Hivyo mdukuzi anaweza Kupata Taarifa zako bila wewe kujua na Kuchukua anachohitaji kwenye simu yako.
Wengi huwa na App za Kifedha hivyo mdukuzi huweza kupata taarifa zote hata kujiamishia Fedha pasipo mhusika kujua na Huweza kufuta kila kitu kwenye simu yako pasipo muhusika kujua.