Ufafanuzi jamani manake hii ni aibu

Ufafanuzi jamani manake hii ni aibu

Automatiki huyo ni baba yako (step father) Mume wa mama ni baba !! kweli unauchungu lakini sheria na hiari haikulindi !
 
Naomba kuwauliza wana jamvi,Mimi ninamzazi mmoja yaani mama ndo aliyebaki kwani Baba yangu alifariki miaka 8 iliyopita kwa upande wetu tumezaliwa wengi na tayari tuna watoto wa kuwazaa wanafikia kama 27 ( wajukuu wa mama ) cha kushangaza mama yetu ameanza tabia ya uzinzi na mbaya zaidi anamleta jamaa mpa home na kulala nae kitanda alichokuwa analala na marehemu Baba yetu,na pia anakuja nae mjini tunapoishi na kupokelewa na kaka yetu na analala na huyo jamaa kwa kaka.mimi hiyo hali napingana nayo na imenifanya nitengwe kwani nilikereka sana nilipogundua.

Nawasilisha

mkuu sikulaumu sana. That is bound to happen. Naturally watoto wa kiume walio wengi wako jealous na over protective sana na mama zao. Jealous in the sense that they would not stand the sight of their mum with another man apart from their father. Cha kufanya nadhani kuna umuhimu wa kuitana ndugu na kumshauri mama aachane na hizo tabia kwani inawaharibia image sio tu yake bali hata yenu huko nje. Mshaurini kama anaweza akubali kuolewa na sio kufanya anachofanya. Tafuteni njia ya kufikisha ujumbe kwa ustaarabu na hekima zaidi na mkiona mnashindwa tafuteni mtu mzima ndani a familia yenu kwa maana ya shangazi, au mwingine mliyemzoea ili mumfikishie ujumbe.
Kuna namna inaweza fanyika. Inaanza na nyinyi kwanza kukalishana pamoja na kulizungumzia hilo suala kila mtu awe wazi
 
ILIPASWA MAMA AMFUATE KWAKE HUYO KIJANA,SII KUMLETA KWENU!Ndio maana zamani wajane walikua hawapewi urithi wa nyumba,ardhi kwa sababu kama hizo
 
Nadhani unamkosea mamaako adabu kusema ameanza tabia ya uzinzi ilhali hujaeleza kama nje ya babaako aliolewa tena.
Kumbuka mama naye ni mwanadamu na ana hisia kama binadamu mwinginewe yeyote...unatakiwa uwe very specific kwamba ni KITU gani kinakukera katika mahusiano mazima ya mama na huyo jamaa yake..kuliko kusema tu ameanza uzinzi.....Ushauri wangu: Mwambie mamaako kile kitu kinachokukera umsikilize naye anasemaje.. (like humpendi mtu wake, au wanafanyia hadharani, au jamaa yake ni mhuni ..n.k). Otherwise i dont see the point!
 
Naomba kuwauliza wana jamvi,Mimi ninamzazi mmoja yaani mama ndo aliyebaki kwani Baba yangu alifariki miaka 8 iliyopita kwa upande wetu tumezaliwa wengi na tayari tuna watoto wa kuwazaa wanafikia kama 27 ( wajukuu wa mama ) cha kushangaza mama yetu ameanza tabia ya uzinzi na mbaya zaidi anamleta jamaa mpa home na kulala nae kitanda alichokuwa analala na marehemu Baba yetu,na pia anakuja nae mjini tunapoishi na kupokelewa na kaka yetu na analala na huyo jamaa kwa kaka.mimi hiyo hali napingana nayo na imenifanya nitengwe kwani nilikereka sana nilipogundua.

Nawasilisha

Mjane hazini wewe, usimkosee heshima mama yako. Ana jamaa boyfriend mmoja tu na ndio huyo anayekuwa naye na kuzunguka naye kwanini unaleta picha as if ni malaya?
Bado mwili unadai (hamu anayo) na upweke unamuumiza; hivyo ni haki yake kuwa na mpenzi.
 
Kama bado hamu anazo bas aolewe na aondoke hapo nyumbani.Kulala na mwanaume katika nyumba ya marehemu mumewe tena kitandan alipokuwa akilala na mumewe ni utovu wa nidhamu na kwakuwa nyie ni watu wazima yapaswa aambiwe.
Wala hakuna laana itakayokupata maana afanyacho si sahihi.
 
Ndicho nilichomueleza....kiukweli aseme tu kinachomkera kuliko kuwa too general...

Mjane hazini wewe, usimkosee heshima mama yako. Ana jamaa boyfriend mmoja tu na ndio huyo anayekuwa naye na kuzunguka naye kwanini unaleta picha as if ni malaya?
Bado mwili unadai (hamu anayo) na upweke unamuumiza; hivyo ni haki yake kuwa na mpenzi.
 
Ndicho nilichomueleza....kiukweli aseme tu kinachomkera kuliko kuwa too general...

somehow tunapaswa kubadilika; hivi ingekuwa ndio baba yake kamleta mamamdogo angesema "baba mzinzi"?

kuhusu kufunga ndoa, hiyo ni issue ya mama yake na sio watoto. tena ingekuwa kwa selfish me, kama wanaishi bila ndoa ningefurahi zaidi maana yake siku akimboa tu mama ana uwezo wa kumtimua kuliko kama wanakuwa wamefungwa kwa pingu za maisha.
 
Ni kweli unahitaji ushauri,lkn kiukweli binafsi sijafurahia kuanika nyeti za mama yako huku...
Me sioni kama ni tatizo kwa anachokifanya mama yako,ili mradi atulie na huyo mmoja,na pia huyo mwanaume asiwe na mke tayari...wajiheshimu,na waenende kwa heshima.
 
Jamaa ni mdogo kumri na ana mke na ilishatokea mother akala kichapo na huyo mke wa jamaa,najua kila mtu ana mtizamo wake ila kiukweli ikitokea kwako sijui utafanya vip.ila ipo siku nikimkuta huyo jamaa nadhani mgazeti ya udaku yataandika
 
Back
Top Bottom