Uendelelezwaji wa eneo la mbele ya bahari jijini Dar Es Salaam unanifikirisha sana

Uendelelezwaji wa eneo la mbele ya bahari jijini Dar Es Salaam unanifikirisha sana

GANJIBHAAI

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2018
Posts
690
Reaction score
1,836
Katika eneo linalonifikirisha zaidi katika kuendeleza Jiji letu la Biashara la Dar es Salaam, ni mwendelezo wa Sura ya mbele ya bahari iliyopakana na nchi kavu ya Jiji la kibiashara la Dar es Salaam ( DAR ES SALAAM WATER FRONT)

Nimejitahidi sana kutafuta maandiko yanayozungumzia eneo hili, unapotafuta taarifa kwenye mtandao, kwa kiasi kikubwa unakutana na maandiko yanatoka kwa watu wa kawaida kama mimi, labda yakishauri ama kushangaa kama ninavyoshangaa mimi ni kwa namma gani tulivyolala kwenye uendelezaji wa eneo hili, lakini ukija upande wa serikali ambapo uelekeo ndipo ulipo hukutani na taarifa ambayo kwangu mimi ndio raarifa rasmi itakayonipa picha halisi ya maamuzi na uelekeo wetu wa uendelezaji kwenye kipande hiki cha nchi yetu kama nchi.

Aidha, kwenye wa kipande hiki cha bahari una faida nyingi sana kwetu. ikiwemo;

Kuongeza hadhi ya Jiji letu, sisi kama watendaji wakati mwingine ktk kutimiza majukumu yetu ya kila siku, tunapata kigumimizi pale tunapoulizwa na wageni “kwa nini niichague Dar es Salaam out all destination in Africa. Niambie wewe ungejibuje?!

Kuna mtu mmoja alishawahi kuniambia “Niamini pale unapokuwa na kipande cha bahari kwenye dunia hii you already Blessed” Najiuliza Tanzania imebarikiwa Mara Ngapi?!.

Najiuliza, kuna sababu gani DMI kubakia eneo lile?’

Najiuliza, kuna sababu gani Marine to and from Znz kujiendesha kwenye eneo lile,

Najiuliza hivi hivi huu sio wkt sahihi wa kuwa na SAMIA WATER FRONT na ndio legacy ambayo haitofutika maisha yetu yote milele na milele Amiiin, twende kwa phases Mama. Kikubwa tuhakikishe tunatengeza pesa kwenye kila hatua, pendezesha mji pia-unlock the possibilities 🙏🏾.
 
Hakika ni ushauri mzuri, nashangaa kwanini miezi 9 yote hujapata like wala comment kwenye uzi wako huu.
 
Imagine ile senyenge iliyochoka kuanzia pale zanzibar ferry mpaka kigamboni ferry ni shilingi ngapi kureplace wkt mkisubiri mipango mikubwa kwenye eneo husika kama ipo.
 
Yaani kama ile beach , mbele ya Agakhan Hospital ni HELA tupu..ukiuliza ohoo kuna issue ya Usalama maana ni ukanda wa Jumba jeupe.. TUAMKE!
 
Back
Top Bottom