Uelewa wa mambo wa Ndugai ndio Shida, yupo tofauti na Watangulizi wake. Haelewi kua yeye ni Spika.

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Mtu anayeshindwa kubainisha udhaifu uliosemwa na CAG ni wa aina gani, uwezo wake wa kusimamia sheria,taratibu na kanuni za bunge utatoka wapi?Mimi sijawahi kuona SPIKA mwenye uelewa wa hivi. Wabunge wa CCM walienda kishabiki zaidi, ni mara 100 zaidi spika angekua dada TULIA AKSON au ANDREW CHENGE na sio huyu mzee.


CAG ameulizwa swali na Mtangazaji Anold Kayanda vipi mbona mmetoa ripoti nyingi halafu hatuoni hatu zikichukuliwa? Mzee wa watu akasema kua kama hatua hazichukuliwi ni udhaifu wa bunge, yeye kafuatwa na mwanahabari na wala hajamwita, sasa kwa kauli hiyo kadhalilisha vipi taifa?. Yeye makosa yake ni yepi? Sasa huyu spika badala ya kutazama ujumbe ahangaike nao, yeye anahangaika na mtu ambaye kisheria kwanza hagusiki. Kwanza CAG sio Prof Assad bali ni taasisi.

Wabunge wa CCM wana kila sababu ya kulaumiwa kwa kumchagua huyu mzee, ni bora hata angekua mzee Chenge.Angalau huyu anaelewa na anajua kuchanganua mambo.

Bunge lishughulike na ripoti za CAG liache kujihami kwa udhaifu wake.Kama sio dhaifu ziko wapi 1.5t? Zilitumikaje?
 
Tunawarithisha wajukuu zetu matatizo makubwa sana mana hatujangi nchi kitaasisi.
Kila MTU ni mbinafsi na anajenga taasisi ya Tumbo lake.

Ndugai anaona ufahari kutumia mamlaka yake kama spika kutisha watu na kutumia vyombo vya dola kutisha watu kama mbinu ya kujenga heshima ya bunge.
Bunge siku zote litapata heshima kwa kuisimamia serikali ipasavyo na kuwatetea wapiga kura.

Dharau hizi kwa wapiga kura zinatokana na huu mfumo wa Serikali na Chama cha mapinduzi kuua demokrasia na kupeana nafasi za kuwawakilisha wananchi kwa nguvu.

Hili ni tatizo kubwa.
Wametoka kwenye kusifi serikali wamehamia kwenye kutisha watu wanaosema kweli.

Spika anajisahau kuwa yeye ni kama Refa sio Kocha.
Kocha ni wananchi na vyama vyao wanaoleta wabunge.

Ndugai siku akisimama kama refa ndio ataona udhaifu wa Bunge lakini kwa sasa anajiona ni Kocha wa Timu moja wapo iliyopo kwenye mashindano wakati yeye ndiye refa. Matokeo yake anakua na wazo la kuihami na kulinda timu yake muda wote hata kwenye faulu za wazi matokeo yake anaharibu mchezo.

Kuna wakati fulani Zito Kabwe alisema kuwa nchi ............... washamba.
Bado natafakari kama alikua na maana gani!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunawarithisha wajukuu zetu matatizo makubwa sana mana hatujangi nchi kitaasisi.
Kila MTU ni mbinafsi na anajenga taasisi ya Tumbo lake.

Ndugai anaona ufahari kutumia mamlaka yake kama spika kutisha watu na kutumia vyombo vya dola kutisha watu kama mbinu ya kujenga heshima ya bunge.
Bunge siku zote litapata heshima kwa kuisimamia serikali ipasavyo na kuwatetea wapiga kura.

Dharau hizi kwa wapiga kura zinatokana na huu mfumo wa Serikali na Chama cha mapinduzi kuua demokrasia na kupeana nafasi za kuwawakilisha wananchi kwa nguvu.

Hili ni tatizo kubwa.
Wametoka kwenye kusifi serikali wamehamia kwenye kutisha watu wanaosema kweli.

Spika anajisahau kuwa yeye ni kama Refa sio Kocha.
Kocha ni wananchi na vyama vyao wanaoleta wabunge.

Ndugai siku akisimama kama refa ndio ataona udhaifu wa Bunge lakini kwa sasa anajiona ni Kocha wa Timu moja wapo iliyopo kwenye mashindano wakati yeye ndiye refa. Matokeo yake anakua na wazo la kuihami na kulinda timu yake muda wote hata kwenye faulu za wazi matokeo yake anaharibu mchezo.

Kuna wakati fulani Zito Kabwe alisema kuwa nchi ............... washamba.
Bado natafakari kama alikua na maana gani!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mfumojiwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom