Ndugu zangu wanajamii, nimekua nikipata taabu sana kutambua uwezo wetu wa kutafiti, kuchambua na kubainisha mada zenye mashiko humu. Mara nyingine tunaleta mada kiushabiki au kwa kupata dokezo tu. Hii ni sawa na mwandishi wa habari anapopata tip kuhusu habari fulani badala ya kuifanyia kazi kujua undani wake yeye anaenda newsroom anaandika anayoyajua kisha story inatoka vivyo sivyo.
Nimeanza na utangulizi huo hasa kwasababu ya hoja aliyoilete vuta-nkuvute kuhusu Mukandala kuendelea kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilihali ameshastaafu. Nadhani huyu ndugu yangu anahoja nyingine ya sirini zaidi ya hiyo ya kustaafu maana ameleza mwanzo vyema kisha anamalizia "hakuna maprofesa wengine wa kushika wadhifa huo mpaka wastaafu waendelee kuongoza?" Baada ya utafiti na uchambuzi na kuongea na baadhi ya maprofesa wakongwe pale UDSM nimeona niwashirikishe haya yafuatayo:-
Prof. Mpangala ameniambia si kila profesa anaweza kuwa VC, wapo maprofesa wengi ambao tangu wameanza kufundisha chuo wakiwa adogo hadi wamekua maprofesa hawajawahi kushika hata wadhifa wa Ukuu wa Idara (Head of Department), pili kiongozi wa chuo anaajiriwa kama mwalimu tu na sii kama vc au kiongozi mwingine na ndiyo maana hata vc analipwa mshahara wake kama profesa pamoja na leadership allowances and benefits.
Profesa mwingine ambaye hakupenda nitaje jina lake ila inasemekana ndiye mwenye umri mkubwa na amekitumika chuo kwa zaidi ya miaka 45 ikiwa ni kama profesa na nyadhifa nyingine za juu, anasema, hapo kale Mtendaji mkuu wa chuo aliletwa na Waziri Mkuu Nyerere ambaye aliitwa Prof. Cranford Pratt mwaka 1961, baada ya kuweka mazingira ya chuo vyema, baada ya hapo alikuja mswahili lakini ikaamuliwa kiongozi wa chuo atoke kwenye chama na serikali ndipo Ndugu Pius Msekwa akachuka uongozi miaka ya 1970 ambapo ndipo kilikuwa chuo kamili. Ikumbuke mwanzo kilikua sehemu ya chuo cha East Africa. Baada ya msekwa wakaja wengine kina Dr. Chagula, Balozi Kuhanga, Prof. Mmari na kisha Prof. Luhanga. hao wote walichaguliwa kwa kuteuliwa na rais lakini utaratibu wa chuo ulifuatwa kiukamilifu. Prof. Chachage na timu yake walipigana kufa na kupona kuhakisha chuo kinapata Hati Idhini (Charter) ambayo pamoja na mambo mengine waliyokua wanapigania ni viongozi kuchaguliwa na wanachuo yaani waalimu, wanafunzi na wafanyakazi waendeshaji kupitia tume u kamati maalumu (credible search team) kisha baada ya kupata watu watatu wenye weledi basi hupekwa kwenye mamlaka za uteuzi. Ndiyo maana hata wakati wa kutafuta VC baada ya Prof. Luhanga kumaliza muda wake kulikua na purukushani sana zikiongozwa na Chachage na mwisho alifanikiwa maana Raisi Mkapa alibariki chuo kiwe na Charter yake kwa mujibu wa sheria na viongozi watafutwe kupitia search teams na siyo Makampuni, agents au kutoka serikalini moja kwa moja. Prof. Mukandala alipitia mchakato huo ambao uliungwa mkono na UDASA chini ya mwenyekiti Chahchage na Baraza la wafanyakazi.
Profesa mwingine wa SUA ameniambia kuwa kamati ya viongozi wa vyuo vya umma (CPCVT) ikishirikiana na vyama vya wafanyakazi wa vyuo vikuu walikutana na Rais na Watendaji wa Wizara ya Utumishi na Hazina wakatoa mapendekezo yao ikiwa ni pamoja na ombi la kubadili umri wa kustaafu kwa waalimu wa vyuo vikuu na baada ya mchakato mrefu ikakubaliwa kuwa Senior Lecturers watastaafu wakiwa na miaka 65 na Maprofesa ni miaka 70 ila akipenda anaweza kustaafu akiwa na umri wa chini ya hapo.
Baada ya hayo naomba msaada katika haya:-
Kwa maelezo hayo je mleta mada ni kwamba hajui vc anapatikanaje? Kuhusu sheria kuwa haimruhusu Prof. Mukandala kuwa VC kwanini hatuendi mahakamani? kwanini tunasemea chinichini? Tuache majungu yasiyo na tija.
Ndugu Lokisa amesema uongozi wa UDSM umejaa wahaya. Sijamuelewa labda atuweke wazi kwa kutoa majina ya viongozi hao na kutueleza yupi mhaya na yupi ni kabila gani. Nasema hivi kwasababu nimeona kwenye website ya UDSM list ya viongozi kama kuna wahaya ni aslimia 1 tu ambaye nimeweza kumuona ni dean wa Sheria na wengine wawili ni heads of departments. Labda ndugu yetu anawafanhamu vyema atuletee hapa otherwise atakua ni mbaywayu.
Ndugu Mnyamahodzo, nadhani tunahitaji kujua kikomo cha utendaji kazi ni kipi kati uprofesa na uongozi. Ila umesema napaswa kuondoka kama Luhanga alivyoondoka. Nimejaribu kumpata Prof. Luhanga akasema kuwa yeye ndiye VC aliyedumu kwenye uongozi kwa muda mrefu sana tangu 1991 hadi 2005 na hadhani kama itakujatokea mtu atakayefikia record yake maana siku hizi utaratibu umebadilika. sasa sijui ndugu mnyamahodzo alitaka kumaanisha luhanga aliondoka kabla ya umri wake wa kustaafu au vipi ila anaweza kutuweka wazi tu kuwa Luhanga aliondoka madakani akiwa na umri gani?
Kkarumekenge, umeuliza kama mukandala anamaandiko aliyoyachapisha hahaaaaaaa nashangaa maana mukandala ameanza kuchapisha vitabu tangu akiwa Berkely na pia atakuwaje Profesa kama haja publish? Nadhani hapa uelewa wako ni mdogo sana kuhusu taratibu za mtu kuwa Prof. Uprofesa siyo cheo ni Degree kwa maneno mengine ambapo mwisho kabisa kama ngazi ya kuhitimu Prof. anatoa kitu kinaitwa Professorial Lectuer sijui kama unakifahamu. Swala la Redet kumpa Mukandala utajiri sijui kama ni kweli labda utuwekee hadharani utaji wake na namna hiyo redet ilivyouleta maana katika matajiri sijui kama mukandala anathubutu hata kutia kidole achila mbali mguu!!!!!!!!!!!!!! Kwa mimi ninavyofahamu na kwa kazi ambayo nimeshapewa na baraza moja la redet huko Zanzibar miaka ya 2005 sijui kama kuna tamko lilishatolewa bila kuwa na data yakinifu. Nakushauri uende pale UDSM umuone Dr. mmoja anaitwa Dr. Makulilo wa Political Science ambaye alifanya utafiti yakinifu kuhusu tafiti za siasa na hayo matamko akupe nini alichogundua. Ukweli ni kwamba REDET inafanya kazi kimataifa syo kama agents wa mifukoni mmmh. Kuhusu Tido Mhando nadhani nilishawahi andika humu kuwa Tido ndiye aliyoifikisha TBC ilipo ndiyo alitaka TBC ifanye kazi kama BBC bila kujua TBC ni ya Tanzania na BBC ni ya UK na hivyo kila moja ina maslahi tofauti. Sikatai kuwa aliiweka TBC katika hali ya sasa, hali ya hadhi ya juu lakini pia hakua mzalendo mshahara wake tunaujua? alikua analipwa kiasi gani na kwa Pound au kwa Shilingi?
Nadhani humu kuna mipasho mingi au kuna watu wanahitaji u VC, nawashauri msubiri ikifika wakati mjaze majina ili michakato ifanyike. Mambo ya vyuo vikuu tuwaachie wao huko si kwenye siasa hasa zetu za majitaka zenye tamaa na ulafi wa madaraka badala ya kujenga nchi. Kuna watu wanakaa chini kazi yao ni kuangalia Mukandala kakosea wapi, kikwete ameenda wapi kombo ili apate pa kuanzia. Mbana nasi hatuanzishi ya kwetu ili tuonekane tuwe viongozi au matajiri. Swala la imempendeza mkuu yanatoka wapi katika u VC? Tena kwa ufahamu wangu Mukandala amefanya kazi karibu na Mkapa zaidi kuliko JK kama mshauri wake wa siasa.
Mwisho tufanye kazi tuchambue mambo tuache kutemewa na kupelekwa kilisulisu, lemalema, lusindelusinde au nchembanchemba humu