Leonard Robert
JF-Expert Member
- Apr 22, 2011
- 11,143
- 7,403
Waislam mbona wachache sana! Hawana effect kwanza kura zao ni za mapepo.
Ili uwe sheikh unatakiwa uwe na Elimu ya dini na maadili safi. Elimu ni jambo la kudumu kwani ukishaipata elimu basi umeshaipata. tuwahukumu hawa masheikh kwa uadilifu wao na si kwa elimu kwani kama elimu ya dini ya Kiislamu wanayo ila sina hakika na uadilifu wao au uwezo wao wa kuhimili ushabiki wao wa kisiasa ili wasije wakaingiza siasa chafu kwenye dini ya Mwenyezimungu.Tatizo elimu za nashehe ni ndogo
na sijui ili uwe shehe unapaswa kuwa na sifa gani . Ndio maana viongozi
wa Dini wanatakiwa wachaguliwe wenye elimu na weledi wa kutosha tatizo wengine wanachaguana kama ccm sio sifa wanaangalia waangalia uwe na udhaifu ndio sifa kuu
Hawa waislam ni makuadi wa CCM,Wamekalia kutumika tu,ndiyo mana wamenyimwa kadhi.
aise wajemen hali siyo nzur basi kikwete akeme matamko kama hayo ambayo yanaweza kuja kutugawa sisi watanzania kama raisi
Sikilizeni wadau, inshu hapa ni propaganda za CCM, enzi zile suala lilikuwa ni kuizoofisha CUF kwa sababu ya zanzibar, tuhuma zile hazikuwa na ukweli wowote, na mpaka leo CUF waliachwa na majeruhi makubwa kiasi kwamba tunao elewa kwa sasa uhalisia wa mambo ni wachache, hata prof Lipumba si wa kulaumu "kwa nini amegobea mara zote na kushindwa lakini bado anaendelea kugombea", inshu nadhani alifanya makusudi ili kulinda hadhi ya chama na kusubiri ukweli ujulikane kama ilivyo sasa. Naamini propaganda za CCM na kitengo chake sasa walishafika mwisho na endapo tu vyama vya upinzani vyenye nguvu (CDM+CUF) wakiungana basi CCM ni kifo 2015,
Sema mimi nasema co sisi p........umlianza tunamaliza. Kama cuf mlikkita cha kiislam. Na sisi tunasema chadema ni chenu
Leo katika ibaada ya ijumaa katika msikiti mkuu wa igunga mjini shekhe ama mtoa mawaidha amesema chadema na wakristo ni makafiri. Katika mawaidha hayo shekhe huyo alisikika kupitia spika za mskitini (Public annoucement system) akisema chadema ni chama cha kidi kwa sababu ya kumdharirisha mkuu wa wilaya ambaye ni mwislam. nami ni kiwa eneo ka msikitini nilisikia maneno hayo ya shekhe. Kweli shekhe katugawa wana igunga. Anadai kwa mwislam yeyote atakaye chagua chadema atalaaniwa. Baada ya ibaada wapo baadhi ya waislam wamechukizwa na hotuba ya shekhe huyo. Mbaya yaidi waislam wanashindwa kuelewa kama kuchagua chadema ni dhambi kwa kauli ya shekhe! je wachague chama kipi? Kwani katika vyama venye nguvu hapa ni chadema, ccm na cuf. Wagombea wote kupitia vyama hivyo wote ni wakristo. Kuna mgombea mmoja tu kutoka chama kimoja cha UDPD ambacho hakina mashiko kabisa hapa igunga hata kampeni bado hakijazindua. Sijui huu udini utatupekeka wapi? haya ni ya kweli nimeyackia mwenyewe na kama una dungu yako hapa igunga ambaye anafuatilia siasa kwa ukaribu please jaribu kumuuliza. Tunaomba dua zenu uchaguzi huu umalizike kwa amani.
Taarifa ya habari ya ITV saa mbili imeonyesha tamko Rasmi la Bakwata kuwataka waislam wa Igunga wasimpigie kura mgombea wa chadema.Nimepata mshtuko mkubwa na kuona taifa letu sasa linaangamia.Hivi ni halali kwa mujibu wa sheria za uchaguzi dini kutangaza rasmi chama fulani kisipigiwe kura? Watu wote wapenda haki demokrasia na amani walaani tamko hili haramu.
Taarifa ya habari ya ITV saa mbili imeonyesha tamko Rasmi la Bakwata kuwataka waislam wa Igunga wasimpigie kura mgombea wa chadema.Nimepata mshtuko mkubwa na kuona taifa letu sasa linaangamia.Hivi ni halali kwa mujibu wa sheria za uchaguzi dini kutangaza rasmi chama fulani kisipigiwe kura? Watu wote wapenda haki demokrasia na amani walaani tamko hili haramu.
Soon dini kitakuwa chanzo cha vurugu nchi hii, hebu tusubiri na tuone
Nimetiza picha ya DC mtandao auliouvaa kuuhita hijjab ni kutukana uislaam ni hijjab gani inayowacha kifua wazi.
chadematv's Channel - YouTube
Si halali kabisa kwa viongozi wadini kutoa maelekezo kwa wapiga kura! Lakini pamoja na Bakwata kusema hayo uchaguzi mkuu 2010 Mapadri bila aibu na magauni yao walisema Waumini tusiichague CCM! Mfaano ni Parokia ya Mpandaa,Ifakara,Bariadi,Tabora na Mbulu! Walitaaka waumini wamchague Padri mwenzaao Dr Slaa! Ukistaajabu ya Bakwata utaonaa ya Roman Catholic na Chaadema!
Nachukia sana watu wanaodhani hisia zao ndiyo fikira zao. Hapa idadi ya waislamu imeingiaje na mapepo ya kura za waislamu yamekujaje kwenye hii mada. Humu ndani kuna tabia mbaya sana inaendelea kukua ya kuuona Uislamu ni dini ya kishetani na waislamu ni watu wasio na uwezo wa kufikiri.
Prof. Safari, Dk. mohammed Bakari wa Mzumbe na Prof. Lipumba kwa kuwataja wachache ni waislamu waliobobea kwenye fani zao lakini ni wazalendo nisio na shaka nao. Sasa kama uislam ni ushetani na ujinga hawa mbona si wajinga wala siuoni ushetani wao.
Najua kuna watu humu ndani wamemeza propaganda za wamarekani kama samaki amezavyo ndoano au mbwa anavyokimbilia kwenye mdomo wa Chatu. Hao Masheikh inawezekana kabisa ni wafuasi wa chama ambacho si CHADEMA na wamesema hayo waliyoyasema si kwa faida ya Uislam bali kwa faida ya chama chao wanachokishabikia.
Wingi wa watu kwenye eneo husika halihusiani na ushawishi wa watu hao kwenye jamii. Nyerere alikuwa Mkristo lakini akafanikiwa kujenga ushawishi kati ya wazee waanzilishi wa TAA na baadaye TANU ambao wengi wao waliku ni waislamu.Tuuheshimu Uislamu kama tunavyouheshimu Ukrsito. Kama hatutawaheshimu waislamu hatutakuwa na haki ya kuheshimiwa nao.
Maisha yangu yote nimeishi katikati ya jamii ya waislamu na wakristo wakiwa wamechanganyika na sijawahi kuona wakipimana uwezo wao wa kufikiri kwa kutegemea asili ya dini zao. Manchester United, Chelsea, Arsenal na timu nyinginezo tunazozipenda tunazipenda kwa sababu zimejaza waislamu tupu au wakristo tupu?