Mwisho niseme tu,wengi wanataka kujitia unabii kuitabiria mabaya mbeya city na kujifanya wanaijua sana hii timu,sasa mkae mkijua kuwa Mbeya city haitapotea na wala haitashuka daraja kama wengi mnavyoiombea.Sisi wana mbeya na mashabiki wa timu yetu ya Mbeya city tutaendelea kuiunga mkono na kamwe hatutasikiliza maeneo yenu.Tunashikilia mkia lakini mkae mkijua tu tutarudi kwenye fomu yetu.
IDUMU MBEYA CITY,WADUMU MASHABIKI WAKE,WADUMU WANA MBEYA,WADUMU WADHAMINI.
TIMU YETU TUNAIPENDA NA DAIMA TUTAKUWA NAYO.
MUNGU IBARIKI MBEYA CITY FC,MUNGU TUBARIKI WANA-MBEYA......AMEN