Der Spiegel
Member
- Aug 4, 2016
- 20
- 9
Wakati wa mchakato wa kutengeneza katiba mpya, tuliona jinsi utawala wa Kikwete ulivyokatisha ndoto kubwa ya watanzania wengi wenye uelewa kupata Katiba ya Warioba iliyokuwa na maudhui mengi yaliyokuwa yakipendelewa sana na ''ma-elites'' nchi nzima. Hata hivyo, wengi walifurahia sana baada ya mchakato wa kuipigia kura katiba hiyo pendekezwa uliposhindikana.
Hata hivyo ukichunguza kwa makini kampeni za vyama vya upinzani katika kipindi kile cha kuhamasisha umma cha 2014, utagundua kuwa masuala mengi ambayo vyama vya upinzani hasa CHADEMA, vilivyokuwa vikiyapigania, yameanza kushughulikiwa na Rais John Pombe Magufuli kwa namna ambayo si mimi, wala mwana-CCM ama mpinzani aliyetarajia huyu jamaa angeyafanya yote hayo na ndani ya kipindi kifupi sana.
Kwa ajili ya kupanua mjadala, tushirikiane tuyajadili vyema ili tumhukumu kwa haki Rais huyu.
Hivi tunaifahamu vyema nchi yetu, je ni haki tumhukumu Rais wetu kwa sababu hataki bunge liwe live, au kwa sababu sukari imepanda bei? Uwezo wetu wa kufikiri ndio umeishia hapo ama?
Nikiri wazi mi ni mpenzi mkubwa sana wa plurality katika siasa ambapo hakuna Chama kinacho-dominate vyama vingine. Mwenye uelewa mzuri wa Comparative Politics atakiri kuwa, kati ya CCM na CHADEMA/UKAWA, anayepaswa kushangilia kwa anayoyafanya Rais Magufuli ni CHADEMA/UKAWA kwa sababu anawasomesha namba vibaya sana wana-CCM, huku akitekeleza yale ambayo wapinzani waliyataka.
Nani atasumbuka kuangalia bunge live wakati Rais anaonekana moja kwa moja akitekeleza watu wanayoyataka na hivyo kupelekea bunge kupitisha kila kitu.
Jamani wapinzani nyie ndio mlio win kuliko wana-CCM, fikirieni mara mbili mbili.
Hata hivyo ukichunguza kwa makini kampeni za vyama vya upinzani katika kipindi kile cha kuhamasisha umma cha 2014, utagundua kuwa masuala mengi ambayo vyama vya upinzani hasa CHADEMA, vilivyokuwa vikiyapigania, yameanza kushughulikiwa na Rais John Pombe Magufuli kwa namna ambayo si mimi, wala mwana-CCM ama mpinzani aliyetarajia huyu jamaa angeyafanya yote hayo na ndani ya kipindi kifupi sana.
Kwa ajili ya kupanua mjadala, tushirikiane tuyajadili vyema ili tumhukumu kwa haki Rais huyu.
Hivi tunaifahamu vyema nchi yetu, je ni haki tumhukumu Rais wetu kwa sababu hataki bunge liwe live, au kwa sababu sukari imepanda bei? Uwezo wetu wa kufikiri ndio umeishia hapo ama?
Nikiri wazi mi ni mpenzi mkubwa sana wa plurality katika siasa ambapo hakuna Chama kinacho-dominate vyama vingine. Mwenye uelewa mzuri wa Comparative Politics atakiri kuwa, kati ya CCM na CHADEMA/UKAWA, anayepaswa kushangilia kwa anayoyafanya Rais Magufuli ni CHADEMA/UKAWA kwa sababu anawasomesha namba vibaya sana wana-CCM, huku akitekeleza yale ambayo wapinzani waliyataka.
Nani atasumbuka kuangalia bunge live wakati Rais anaonekana moja kwa moja akitekeleza watu wanayoyataka na hivyo kupelekea bunge kupitisha kila kitu.
Jamani wapinzani nyie ndio mlio win kuliko wana-CCM, fikirieni mara mbili mbili.