Udhaifu wa Bunge uko wapi?

Udhaifu wa Bunge uko wapi?

Ulimbo

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2009
Posts
3,766
Reaction score
4,046
Kumekuwa na thread nyingi zinazo husu udhaifu wa Bunge la Tanzania.

Naomba kila mtu aweze kuchangia mawazo yake huru kuondoa ukakasi uliopo kwa sasa juu ya adhabu zinazotolewa kwa watu wanaosema bunge ni dhaifu.

Je, udhaifu wa bunge uko wapi?

1- Kushindwa kutoa orodha/list ya watu walioficha fedha nje ya nchi sijui uswizi?

2- Kushindwa kutoa orodha/list ya watu waliochota hela za EPA, IPTL, TANGOLD na MEREMETA n.k?

3- Kushindwa kutupa mrejesho wa pesa za kishika uchumba - ACACIA/BARCK?

4- Kushindwa kutupa majina ya watu wasiojulikana waliompiga Mbuge mwenzao risasi?

5- Kushindwa kuisimaia/kuiuliza serikali katika matumizi abayo budget yake haikupitishwa na Bunge?

6- Kushindwa kuiojii serikali zilipo 1.5 trilion alizosema mkaguzi wa mahesabuya serikali?

Orodha ni ndefu, naomba uongeze ya kwako ili tupate majibu stahiki.
 
Kumekuwa na thread nyingi zinazo husu udhaifu wa Bunge la Tanzania.
Naomba mods msiuchanganye uzi huu na nyingine, ili kila mtu aweze kuchangia mawazo yake huru kuondoa ukakasi uliopo kwa sasa juu ya adhabu zinazotolewa kwa watu wanaosema bunge ni dhaifu.

Je udhaifu wa bunge uko wapi?
Bunge letu ni imara sana na halina udhaifu wowote, ndio maana kila anayesema Bunge dhaifu, huitwa Dodoma na kuonyeshwa uimara wa Bunge letu. Mimi mwenyewe naujua uimara wa Bunge letu maana nami niliishawahi kuitwa Dodoma.
P.
 
Bunge letu ni imara sana na halina udhaifu wowote, ndio maana kila anayesema Bunge dhaifu, huitwa Dodoma na kuonyeshwa uimara wa Bunge letu. Mimi mwenyewe naujua uimara wa Bunge letu maana nami niliishawahi kuitwa Dodoma.
P.
Mlio karibu na huyu memba jitahidini muwe karibu nae 24/7

Pascal Mayalla take it easy and calm down!

Take deep breath, take some puffs and rest.
 
Bunge letu ni imara sana na halina udhaifu wowote, ndio maana kila anayesema Bunge dhaifu, huitwa Dodoma na kuonyeshwa uimara wa Bunge letu. Mimi mwenyewe naujua uimara wa Bunge letu maana nami niliishawahi kuitwa Dodoma.
P.

Ina maana pia wewe ni dhaifu ndiyo maana unaogopa kusema kuwa Bunge ni dhaifu? Je wewe uliitwa kwa sababu hiyo?
 
1)Bunge ni imara kama taasisi na kunawabunge imara pia
2) kuna wabunge ambao ni dhaifu kama wabunge tu.
Ikiwa bunge taasisi ndo dhaifu hakukua na haja mbunge kuingia ndani ya bunge dhaifu.. na akiingia basi na huyo mbunge nae anakua dhaifu..

Bunge letu ni imara sana na halina udhaifu wowote, ndio maana kila anayesema Bunge dhaifu, huitwa Dodoma na kuonyeshwa uimara wa Bunge letu. Mimi mwenyewe naujua uimara wa Bunge letu maana nami niliishawahi kuitwa Dodoma.
P.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bunge letu ni imara sana na halina udhaifu wowote, ndio maana kila anayesema Bunge dhaifu, huitwa Dodoma na kuonyeshwa uimara wa Bunge letu. Mimi mwenyewe naujua uimara wa Bunge letu maana nami niliishawahi kuitwa Dodoma.
P.
Kuna haja sasa ya kuwaita takribani nusu ya wa Tanzania pale dodoma ili wakaonyeshwe uimara wa bunge letu,hii ya kuita mmoja mmoja ndio inayochangia kuenea na kusambaa kwa hii Hali ya sintofahamu juu ya uimara au udhaifu wa bunge letu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1)Bunge ni imara kama taasisi na kunawabunge imara pia
2) kuna wabunge ambao ni dhaifu kama wabunge tu.
Ikiwa bunge taasisi ndo dhaifu hakukua na haja mbunge kuingia ndani ya bunge dhaifu.. na akiingia basi na huyo mbunge nae anakua dhaifu..



Sent using Jamii Forums mobile app

Kifupi mtu akisema Bunge ni dhaifu, ina maana kiongozi wao -spika- ndiye dhaifu
 
Sasa Bunge ndio linaonyesh udhaifu wa hali juu kabisa
  1. Kiongozi wa Bunge ni mtu anapaswa kuwa na maadili na kujua miiko ya uongozi. Lakini ndio anaongoza kuvunja kusema mkopo wa Lema hadharani pasipo kuombwa na mtu au taasisi yeyote, ni kiwango cha hali ya juu cha kukosa maadili ya uongozi na kinyume na maadili ya uongozi. Je Bunge litamchukulia hatua? kio sio huo ndio udhaifu wenyewe wa Bunge
  2. Mtuhumiwa wa kosa la kuliita bunge ni dhaifu ni Prof. Asad, na katika kusema huko yeye anakuwa mtuthumiwa mkuu. cha ajabu walioendorse statement ya Prof. Asad wamepewa adhabu kubwa kuliko Asad Mwenyewe. Je huo sio ushaifu unaonyeshwa na watawala wa Bunge pamoja na wabunge wenyewe?
  3. Kiongozi Mmoja wa Bunge alionekana nje ya Bunge akiongea na Pierre Liquid akisalimiana na kupiga picha na wakaagana wataonana mjengoni na baadae anasema alikua hamfahamu. Je kama kiongozi wa Taasisi anaweza kuongopa mbele ya camera au kusahau baada ya muda mfupi, vipi kuhusu taasisi anayoiongoza.
  4. Kiongozi napmoja na Bunge lenyewe linatambua halina mamlaka ya kumwajibisha CAG kwani hawajaibiki kwao lakini wamepitisha "adhabu" huku wakijua haina madhara yeyyote kwa mpewa adhabu. Je huoni Bunge limeonesha udhaifu mkubwa kuliko aliyoyasema mtuhumiwa
  5. Fedha za umma zimepotea, hakuna aliyewajibishwa iwe na serikali wala Bunge lenyewe. Mkaguzi kusema mnaudhaifu katika kuisimamia serikali manona mmedhalilishwa? Je sheria mbaya zilizosababishia hasara serikali na hata kupelekea kunyimwa misaada, inatokana na kukosa umakini wa Bunge hivyo ndio udhaifu wenyewe.
  6. Need to say more, Ni dhaifu
 
Watajitahidi sana kuficha madhaifu yao kwa kuwaadhibu wasiokuwa na hatia, lakini udhifu ni udhaifu tu, hauwezi kuuondoa kwa kulazimisha watu wasiuone na kuusema
 
Kwa hiyo CAG anafuatilia issues za watu wasiojulikana?
 
Bunge letu ni imara sana na halina udhaifu wowote, ndio maana kila anayesema Bunge dhaifu, huitwa Dodoma na kuonyeshwa uimara wa Bunge letu. Mimi mwenyewe naujua uimara wa Bunge letu maana nami niliishawahi kuitwa Dodoma.
P.
"ndio maana kila anayesema Bunge dhaifu, huitwa Dodoma na kuonyeshwa uimara wa Bunge letu"

Umenifanya nicheke sana.Hilo sasa ni bunge la KAMATI YA MAADILI balada ya BJMT.
 
Back
Top Bottom