Travelogue_tz
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 855
- 1,224
Habari JF: Kwa muda mrefu nimefuatilia uanzishwaji wa ACT na harakati zake kisiasa nikabaini mambo muhimu ambayo yanafanya chama hiki kidogo kuwa dhaifu mapema zaidi lakini pia kukosa fursa ya kukua kitaasisi :
Mosi : Waanzilishi wake hawakuwa na nia wala malengo ya kuanzisha chama cha siasa. Uanzishwaji wake ni matokeo ya usaliti na ukibaraka
Pili : Chama hiki kimepoteza autonomy kama taasisi kwa sababu kimemsubiri mtu afukuzwe then ndio ajiunge, katiba ipitishwe, Uchaguzi ufanyike na mtu huyo akabidhiwa madaraka makubwa zaidi ya chama.
Tatu : Chama hicho kuakisi taswira na haiba yake kuwa kinafadhiliwa na watawala kwa lengo la kupunguza kura za Ukawa.
Nne : Chama hiki kukosa agenda ya pamoja ya kufikisha kwa umma, wakati Mkuu wa Chama anasema Viongozi wa ACT wataje mali zao hakuna hata mmoja anayefikiria kufanya hivyo.
Tano : Kukosa dira ya kizalendo na kijamaa katika kufikisha Ujumbe. Zimesikika kelele tu za Uzalendo lakini hakuna tafsiri rahisi katika hoja zao zinazotumika katika mikutano ambazo zinarutubisha Uzalendo. Kusema tunarudisha Uzalendo ni hoja zisizo na mashiko.
Sita : Ni mamlaka aliyopewa Mkuu wa Chama ambapo kimsingi inaathiri utendaji wa Viongozi wengine. Sio rahisi kueneza itikadi ya taasisi kwa kutegemea mtu mmoja. Mfano mtu huyo akishindwa kufanya kazi na taasisi inakufa.
Mwisho kabisa ni aina ya wanachama wanaotumika katika mitandao ya kijamii wengi wao ni kutoka chama tawala, hata wale wachache wamepotoka na kujikuta wanashindwa kujenga hoja za ushawishi ili kupata ufuasi.
Mosi : Waanzilishi wake hawakuwa na nia wala malengo ya kuanzisha chama cha siasa. Uanzishwaji wake ni matokeo ya usaliti na ukibaraka
Pili : Chama hiki kimepoteza autonomy kama taasisi kwa sababu kimemsubiri mtu afukuzwe then ndio ajiunge, katiba ipitishwe, Uchaguzi ufanyike na mtu huyo akabidhiwa madaraka makubwa zaidi ya chama.
Tatu : Chama hicho kuakisi taswira na haiba yake kuwa kinafadhiliwa na watawala kwa lengo la kupunguza kura za Ukawa.
Nne : Chama hiki kukosa agenda ya pamoja ya kufikisha kwa umma, wakati Mkuu wa Chama anasema Viongozi wa ACT wataje mali zao hakuna hata mmoja anayefikiria kufanya hivyo.
Tano : Kukosa dira ya kizalendo na kijamaa katika kufikisha Ujumbe. Zimesikika kelele tu za Uzalendo lakini hakuna tafsiri rahisi katika hoja zao zinazotumika katika mikutano ambazo zinarutubisha Uzalendo. Kusema tunarudisha Uzalendo ni hoja zisizo na mashiko.
Sita : Ni mamlaka aliyopewa Mkuu wa Chama ambapo kimsingi inaathiri utendaji wa Viongozi wengine. Sio rahisi kueneza itikadi ya taasisi kwa kutegemea mtu mmoja. Mfano mtu huyo akishindwa kufanya kazi na taasisi inakufa.
Mwisho kabisa ni aina ya wanachama wanaotumika katika mitandao ya kijamii wengi wao ni kutoka chama tawala, hata wale wachache wamepotoka na kujikuta wanashindwa kujenga hoja za ushawishi ili kupata ufuasi.