Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Udasa: Tume ya katiba ni mali ya rais
Wednesday, 12 January 2011 21:22
Salim Said
JUMUIYA ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udasa), imesema haitoacha kutoa elimu kwa Watanzania jinsi ya kutoa majibu kwa Tume ya katiba itakayoundwa na Rais Jakaya Kikwete kutekeleza mchakato wa katiba mpya, kwa sababu wanaamini tume hiyo sio shirikishi.
Akitoa salamu za kuuaga mwaka jana na kukaribisha mwaka huu, Rais Kikwete alitangaza kuanza mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya.
Kikwete alisema ameamua kuunda Tume maalum ya Katiba, itakayoongozwa na mwanasheria aliyebobea na itakuwa na wajumbe wanaowakilisha makundi mbalimbali kwenye jamii yetu kutoka pande zetu mbili za Muungano. Lakini kabla, Rais Kikwete hajatangaza tume hiyo, Udasa ilisema tume hiyo ni mali ya rais mwenyewe na haitakuwa shirikishi.
Kutokana na hali hiyo, ili kuepukana katiba mpya ambayo itakuwa mbaya kuliko hata iliyopo, Udasa imeamua kufanya mfululizo wa makongamano ya wazi ya kutoa elimu kwa Watanzania kuandaa majibu ya kutoa pindi Tume hiyo itakapoundwa na kuanza kutafuta maoni.
Kongamano la kwanza litafanyika Januari 15, mwaka huu ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kwamba, tayari Udasa imealikwa watu mbalimbali kutoka serikalini, vyama vya siasa na vyama vya kiraia na jamii. Makamu Mwenyekiti wa Udasa, Dk Kitila Mkumbo, alisema tume ya kupitia katiba ya Rais Kikwete haitokuwa shirikishi.
Sio shirikishi kwa sababu inateuliwa na mtu mmoja, hivyo hatuwezi kusema ni shirikishi, kungekuwa na utaratibu wa kitaifa wa kuunda tume hiyo, basi tungekubali kuwa ni shirikishi, alisema Dk Mkumbo. Dk Mkumbo alisema hawajui idadi ya makongamano watakayoendesha kwa mwaka, lakini yatakuwa mfululizo kwa ajili ya kuelimisha Watanzania.
Sisi hatuna bajeti kubwa, tunatumia fedha yetu, hatujaomba msaada kutoka kwa mfadhili yeyote na shughuli nyingi zinafanywa na vijana wetu hapa, hivyo hatuna haja ya kutengeneza bajeti kubwa, alisema Dk Mkumbo na kuongeza: Tumeshamwalika Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, makatibu wakuu wa vyama siasa na jamii au kiraia, lakini pia tunawaalika wananchi wa kawaida waje kwa wingi.
Alisema makongamano hayo yanalenga kuonyesha udhaifu na ubora wa katiba iliyopo, kuonyesha haja, maudhui na mchakato bora wa katiba mpya ya Watanzania sio kundi moja la jamii au kisiasa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Udasa, Profesa Mushumbusi Kibogoyo, alisema kuandaa makongamano hayo kwa ajili ya kutoa elimu kwa umma, hawajaingilia kazi za rais wala waziri yeyote, bali wanatimiza lengo lao kwa mujibu wa katiba yao.
Kama Rais alikuwa na nia ya kuunda tume kwa lengo la kuwanyamazisha wengine wasiseme katika mchakato wa katiba, basi amechanganyikiwa. Tume ni mali yake, ana mamlaka ya ripoti yake na yeye ndiye ataamua kuitoa ikimridhisha au kuificha iwapo hataridhika nayo, alisema Profesa Kibogoyo.
Wednesday, 12 January 2011 21:22
Salim Said
JUMUIYA ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udasa), imesema haitoacha kutoa elimu kwa Watanzania jinsi ya kutoa majibu kwa Tume ya katiba itakayoundwa na Rais Jakaya Kikwete kutekeleza mchakato wa katiba mpya, kwa sababu wanaamini tume hiyo sio shirikishi.
Akitoa salamu za kuuaga mwaka jana na kukaribisha mwaka huu, Rais Kikwete alitangaza kuanza mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya.
Kikwete alisema ameamua kuunda Tume maalum ya Katiba, itakayoongozwa na mwanasheria aliyebobea na itakuwa na wajumbe wanaowakilisha makundi mbalimbali kwenye jamii yetu kutoka pande zetu mbili za Muungano. Lakini kabla, Rais Kikwete hajatangaza tume hiyo, Udasa ilisema tume hiyo ni mali ya rais mwenyewe na haitakuwa shirikishi.
Kutokana na hali hiyo, ili kuepukana katiba mpya ambayo itakuwa mbaya kuliko hata iliyopo, Udasa imeamua kufanya mfululizo wa makongamano ya wazi ya kutoa elimu kwa Watanzania kuandaa majibu ya kutoa pindi Tume hiyo itakapoundwa na kuanza kutafuta maoni.
Kongamano la kwanza litafanyika Januari 15, mwaka huu ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kwamba, tayari Udasa imealikwa watu mbalimbali kutoka serikalini, vyama vya siasa na vyama vya kiraia na jamii. Makamu Mwenyekiti wa Udasa, Dk Kitila Mkumbo, alisema tume ya kupitia katiba ya Rais Kikwete haitokuwa shirikishi.
Sio shirikishi kwa sababu inateuliwa na mtu mmoja, hivyo hatuwezi kusema ni shirikishi, kungekuwa na utaratibu wa kitaifa wa kuunda tume hiyo, basi tungekubali kuwa ni shirikishi, alisema Dk Mkumbo. Dk Mkumbo alisema hawajui idadi ya makongamano watakayoendesha kwa mwaka, lakini yatakuwa mfululizo kwa ajili ya kuelimisha Watanzania.
Sisi hatuna bajeti kubwa, tunatumia fedha yetu, hatujaomba msaada kutoka kwa mfadhili yeyote na shughuli nyingi zinafanywa na vijana wetu hapa, hivyo hatuna haja ya kutengeneza bajeti kubwa, alisema Dk Mkumbo na kuongeza: Tumeshamwalika Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, makatibu wakuu wa vyama siasa na jamii au kiraia, lakini pia tunawaalika wananchi wa kawaida waje kwa wingi.
Alisema makongamano hayo yanalenga kuonyesha udhaifu na ubora wa katiba iliyopo, kuonyesha haja, maudhui na mchakato bora wa katiba mpya ya Watanzania sio kundi moja la jamii au kisiasa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Udasa, Profesa Mushumbusi Kibogoyo, alisema kuandaa makongamano hayo kwa ajili ya kutoa elimu kwa umma, hawajaingilia kazi za rais wala waziri yeyote, bali wanatimiza lengo lao kwa mujibu wa katiba yao.
Kama Rais alikuwa na nia ya kuunda tume kwa lengo la kuwanyamazisha wengine wasiseme katika mchakato wa katiba, basi amechanganyikiwa. Tume ni mali yake, ana mamlaka ya ripoti yake na yeye ndiye ataamua kuitoa ikimridhisha au kuificha iwapo hataridhika nayo, alisema Profesa Kibogoyo.