UDA, Fursa Hiyooo Ruti Ya Makumbusho Mwenge

JAYJAY

JF-Expert Member
Oct 31, 2008
7,521
7,568
Kana kwamba maisha ni nafuu sana maumivu mengine yanaongezwa. Baada ya kulipa nauli ya kukufikisha Makumbusho sasa inabidi utafute nauli nyingine ya kukufikisha Mwenge au utembee tu. Yaleyale ya Mnazi Mmoja Kivukoni. Kisha utasikia UDA wamepewa ruti hiyo. Safari ndefu hawaendi ila fupifupi za kupiga pesa fasta ndio wanazoenda. Tutaumia sana tunaotegemea daladala!
 
Maswali yasiyojibika... Kura yako kwa CCM ndio inakugharimu... hamna rangi mtakayoacha kuiona.... Mtalia sana na kusaga meno...Na Bado sana mbele kunakuja lazima Mkimbie Dar Itafika wakati Mtaomba Mwokozi aje.....

Kwa Taarifa fupi Mapato ya Jiji yameshaanza kupungua... hivyo Mtakamuliwa sana.... Rudini Kigoma... Mashamba mengi mmeacha... mawese tunatumia ya nje,hadi Korosho za Nje,Nguo za Pamba za Nje tena Mitumba,Nyerere alisema Tengenezeni hata matrekta yanayoenda kinyume nyume kama walivyoanza Korea Mjini wanahitajika Wanasayansi na Wataalamu tu sio Wauza Ubuyu na mafenesi...na Madafu...
 
naona nililokuwa nalifikiria na kuliwaza Sasa naona linatimia kwa kasi hakika suala la usafiri hasa wa daladala nadhani UDA pekee ndio wanaotakiwa kubakia jijini dar wakitoa Huduma ya usafiri huwa nahisi kama wapo juu ya sheria vile wanapakia na kukata Kara ruti watakavyo.unaweza ukatoka nao gongo la mboto wakakwambia mwisho buguruni ukishuka buguruni utasikia wanapakia tena ubungo mwisho ubungo wakifika ubungo wanapakia MWENGE mwisho wakifika MWENGE wanapakia TEGETA utaona safari 1 wanapiga 1 kwa 4. kwahiyo ukitoka g mboto mpaka MWENGE utatumia sh 1200.

kwanini nao wasipigiwe mkorogo?? sasa hivi wao wanapeta tuu magari mengine hayapitii MWENGE ila uda pekee ndio anapitia MWENGE.
 
Kawaida tu,hata hao UKAWA hawana jipya.
Watu tutalipa tu,sie sio watuwa siasa,tunatafuta pesa ili kutumia.
We piga kelele na ukawa wako usibiri muokozi wako Lema aje akusaidie,uache kufanyakazi
Fanyakazi acha issue hizo za siasa kijana utapotea wakati wenzio wanaingiza siku
 
Kawaida tu,hata hao UKAWA hawana jipya.
Watu tutalipa tu,sie sio watuwa siasa,tunatafuta pesa ili kutumia.
We piga kelele na ukawa wako usibiri muokozi wako Lema aje akusaidie,uache kufanyakazi
Fanyakazi acha issue hizo za siasa kijana utapotea wakati wenzio wanaingiza siku

Mkuu ni ww kweli uliendika huo UGORO huamini kwamba SIASA ndo inaweka Mazingira hata ya Biashara zetu kuwa sawa? na kuwasusia tunajikomoa wenyewe? duh km nihivi basi Tunasafari ndefu...!!
 
wanaitengenezea UDA fursa za kupig hela; utasikia "kutokana na malalamiko ya wananchi, serikali imeliamuru shirika la UDA kuanza kutoa huduma ya usafiri kwa ruti ya makumbushi-mwenge"
 
wanaitengenezea UDA fursa za kupig hela; utasikia "kutokana na malalamiko ya wananchi, serikali imeliamuru shirika la UDA kuanza kutoa huduma ya usafiri kwa ruti ya makumbushi-mwenge"


Kufa hatutakufa ila cha moto tutakiona, naona wamedhamiria kutufukuza jijini sidi akina kcc ili wabaki wao na familia zao
 
Ingekuwa China watu type za kina Robert Kisena wangekuwa washakalishwa kwenye kiti cha umeme.

execution.png

c92b8a40468c10463c7ed247f724502e.jpg
 
Kawaida tu,hata hao UKAWA hawana jipya.
Watu tutalipa tu,sie sio watuwa siasa,tunatafuta pesa ili kutumia.
We piga kelele na ukawa wako usibiri muokozi wako Lema aje akusaidie,uache kufanyakazi
Fanyakazi acha issue hizo za siasa kijana utapotea wakati wenzio wanaingiza siku[/QU
we m.s.e.n.g.e sana asa ukawa imefuata nini hapa!? Sie tunajadili nauli wewe unaleta urojo
 
Pia tetesi, kuingia mjini (posta and kkoo) wenye private car itakuwa kwa vibali...
 
naona nililokuwa nalifikiria na kuliwaza Sasa naona linatimia kwa kasi hakika suala la usafiri hasa wa daladala nadhani UDA pekee ndio wanaotakiwa kubakia jijini dar wakitoa Huduma ya usafiri huwa nahisi kama wapo juu ya sheria vile wanapakia na kukata Kara ruti watakavyo.unaweza ukatoka nao gongo la mboto wakakwambia mwisho buguruni ukishuka buguruni utasikia wanapakia tena ubungo mwisho ubungo wakifika ubungo wanapakia MWENGE mwisho wakifika MWENGE wanapakia TEGETA utaona safari 1 wanapiga 1 kwa 4. kwahiyo ukitoka g mboto mpaka MWENGE utatumia sh 1200.

kwanini nao wasipigiwe mkorogo?? sasa hivi wao wanapeta tuu magari mengine hayapitii MWENGE ila uda pekee ndio anapitia MWENGE.

Kama ulivyosema,subiri wapigwe mkanda. Ndio utakuwa mwarobaini wao
 
naona nililokuwa nalifikiria na kuliwaza Sasa nakona linatimia kwa kasi hakika suala la usafiri hasa wa daladala nadhani UDA pekee ndio wanaotakiwa kubakia jijini dar wakitoa Huduma ya usafiri huwa nahisi kama wapo juu ya sheria vile wanapakia na kukata Kara ruti watakavyo.unaweza ukatoka nao gongo la mboto wakakwambia mwisho buguruni ukishuka buguruni utasikia wanapakia tena ubungo mwisho ubungo wakifika ubungo wanapakia MWENGE mwisho wakifika MWENGE wanapakia TEGETA utaona safari 1 wanapiga 1 kwa 4. kwahiyo ukitoka g mboto mpaka MWENGE utatumia sh 1200.

kwanini nao wasipigiwe mkorogo?? sasa hivi wao wanapeta tuu magari mengine hayapitii MWENGE ila uda pekee ndio anapitia MWENGE.

Ni swali kila siku najiuliza sipati jibu. Siyo sahihi kabisa na hakuna fair play na daladala za kawaida. Iweje wengine wana route maalumu lakini wao ni kuvamia route tena bila utaratibu? Biashara ya daladala ni kama biashara nyingine bila kujali ni serikali au mtu binafsi lazima kuwepo fair competition.
 
Nimesikia toka mjengoni (mbunge Abas Mtemvu) kwamba UDA imeshapigwa bei (13 billion?). Dah nchi hii bana, yaani unatoa milioni 200 unapewa shirika zima (mabasi, yadi and many other asserts), then after a while unauza na kuvuta 13 billion kiulaaaiini (Joti alikuwa na kamsemo..''kama unanawaaa...'')
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom