Uchokozi: Rais Magufuli unajua haya?

Uchokozi: Rais Magufuli unajua haya?

Ngojea tuangalie nyendo za huyu mkwepa kodi Bin Slum, yupo karibu na nani mpaka kutolipia kontena 20 "kama yeye alivyosema".
 
hahaha umenifurahisha mkuu...duh ukweli upo kwako unaujua au wana ccm....japo hapa sa hivi ishue ni kurekebisha nchi si suala la ccm wala chadema wala nini sijui
 
Magufuli piga kazi achana na ccm ijifie yenyewe jitahidi tu tupate katiba mpya inayokubali uwepo wa mgombea huru,vibaka wa Lumumba wakizingua unaachana nao.
 
Laiti wangejua ukweli uliojificha katika secta flaniflani, wasingekaa kubisha kila neno wanaloambiwa ama kushauriwa.
Nadhani ule msemo wangu wa Ngoja kidogo tu fulani aingilie anga la fulani ndo hapo hasa mbichi na mbivu zitajulikana. Stay tuned bothersand sisters.
 
Napongeza juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya kupambana na rushwa,ufisadi na uhujumu uchumi. Napongeza pia kukatwa kwa matumizi yasiyo ya lazima ya Serikali. Hongera Rais Magufuli na Serikali yako. Tunazidisha maombi juu yenu.

Lakini,unajua mambo haya? Unajua kuwa TRA na Bandari-TPA ndiko kwenye mizizi ya CCM? Unajua kuwa wanufaika wa huko ni wanufaika wa keki ya Taifa na ni wamwaga sifa kwa chama na Serikali tawala?
Rais Magufuli,unajua kuwa matajiri wa huko ndiyo wapenda chama tawala kuliko hata maskini ambao wao hudanganywa tu wakati wa kampeni?

Rais Magufuli,unajua kuwa matajiri wa TRA na Bandari ndiyo wachangiaji wakubwa wa chama tawala na hata wagombea bora wa chama uchaguzini? Kugusa huko,ni kugusa mfupa wa CCM. Chama kitahisi maumivu muda si mrefu.

Truly,the ongoing reforms and fighting pain the ruling party than anyone else!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Siku zote Mzee Tupa Tupa nakukubali kwa kuongea ukweli....Ngoja tusubiri
 
Laiti wangejua ukweli uliojificha katika secta flaniflani, wasingekaa kubisha kila neno wanaloambiwa ama kushauriwa.
Nadhani ule msemo wangu wa Ngoja kidogo tu fulani aingilie anga la fulani ndo hapo hasa mbichi na mbivu zitajulikana. Stay tuned bothersand sisters.
Mkuu tupe ubuyu mkuu, umetuacha njia pandaaisee, japo seems una pwenti nzito sana
 
Back
Top Bottom