Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Mkuu Jasusi habari. Vipi umeshamsikia mwanajamvi mwenzetu Zomba. Ni siku nyingi sijamsikia.

Nimefurahi unapitia kitabu cha J. Illife. Tupe utakachobahatika nacho.
Mimi nilipitia kitambo kidogo.
 
Naona mnakasha umeshageuka kutoka wazee wa Gerezani hadi mapinduzi ya Zanzibar.
Watoto wa hasidi Mohamed Said wameamua kumuokoa mzee wao kwenye kibano. Walipoona kabanwa na ile longolongo ya balozi wa Marekani kuhutubia bunge, hawakuwa na jingine zaidi ya kuupotosha mjadala!
 
Cha kudebate tena hakuna kwani uovu wa Nyerere hata Mungu muumba wa mbingu na ardhi ametuonesha.
Halafu nasikia kaburi lake lilikuwa likitoa sauti za vitisho vya ajabu.Walinzi wa kaburi ile wiki ya mwanzo walitimua mbio kwa sauti mbaya sana kama ya mbwa
Woooooooooooooooooh!,Woooooooooooooooh!
Duh! sasa hizo ndio hofu za kishirikina. Unasababu gani wewe kujiita Great Thinker kwa ushirikina huu?
 
Jasusi.

Waarabu tuna usemi mmoja IN ORDER TO BUILD SOMETHING STRONG, IT HELPS TO START WITH BEST AND POSSIBLE MATERIALS. Na waswahli wanasema kila kitu ni msingi. kama umeweka msingi mbovu hata ufanyeje huwezii jenga kitu imara.

Sasa wa TZ ndio mupo hapo msingi mboovu mliojengewa na JKN ndio huo unaowasibu mpaka leo.

Kuhusu mzee Bomani naona tusiongee mengi kwani namfahamu vizuri sana sana sitaongea mengi bali mpe salam zangu atakwambia mengi kuhusu Mimi. Muulize tu Hamza Yousuf (alizoea kuniita Mwarabu au Mznz) kisha utanieleza.

Pole ndugu yangu
Barubaru, mbona hujibu swali uliloulizwa na Jasusi? umeulizwa "mlitaka kumwambia nini Nyerere?"
 
Nyie mbona mmeungana kumshambulia Mohamed Said kutoka na dini yake. Umeishajiuliza kwa nini mmeungana Wakiristo wote na watu wa Musoma kumtetea Nyerere.
Ritz, wacha uongo, Mohamed Said hashambuliwi kwa sababu ya dini yake, bali anakosolewa hapa jamvin kwa mambo makubwa mawili, moja ni kutumia uislam kupotosha historia ya Tanganyika, ya pili ni kuandika uwongo kwa malengo ya uchochezi. Yote mawili yameoneshwa waziwazi hapa. Kwamba balozi wa Marekani alihutubia bunge ni uongo! kwamba Nyerere alikuwa adui wa waislam huo ni uongo na uchochezi!
 
Jasusi,
Wewe umepokea kwa Judith Listowel.

Mimi nimekaa na Sheikh Haidar Mwinyimvua.
Sheikh Haidar Mwinyimvua ni mmoja wa wajumbe wa Baraza la Wazee.



Wazungu waijue historia ya TANU kunishinda mie mjukuu wa mashujaa hawa?
Huo ni muhali.



Si Listowel wala Iliffe anaweza kuwajua watu hawa kunishinda.
Mie nimeishi na wazee hawa toka udogo wangu hadi hawa wazee walipoondoka duniani.

Walinipa mengi kuhusu TANU na Nyerere.
Sahihisho kwa Lady Listowel.

Mwaka 1965 Sheikh Takadir alikuwa hayupo duniani.
Huu ni utetezi dhaifu sana katika nyanja za kisomi! "historical facts" zinabakia kuwa "fact" bila kujali zimesemwa au kuandikwa na nani, mzungu au mweusi. Kinachobadirika ni uchambuzi wa "facts" hizo. Kwamba Nyerere na watanganyika wenzake waliunda TANU na kudai uhuru ni "historical fact" iandikwe na Mohamed au Illife itabakia kuwa historical fact. Lakini kwamba katika mapambano hayo ya uhuru waislam ndio waliomsaidia zaidi Nyerere kuliko watu wengine na hivyo wanasitahili sifa na heshima kuliko watanganyika wengine, hiyo ni "Opinion" ambayo Mohamed na Illife watatofautiana. Na ni hapo ndipo Mohamed hatakubali kushindwa na Illife kwa sababu yeye ni muislam na Illife sio muislam!
 
Wickama,
Ahsante nimefahamu.

Mimi huingia katika mjadala kusoma na ikibidi nisomeshe.

Sheikh wangu kaniusia anasema,"Ingia katika mnakasha usome
au usomeshe. Usiingie kutafuta ubishi kwani ilm ya ubishi haina
baraka."

Mie simo humu kutafuta ushindi.
Nataka nikupeni yale yaliyokuwa mageni kwenu.
Unajuaje kama yalikuwa mageni kwetu?Kwani wewe ndio mumiliki wa taaluma ya historia?
 
Tuna miezi minne kwenye huu mnakasha ukimtoa Mkandara ambaye anajulikuna jamvini alivyokuwa na mahaba na Nyerere hebu nitajie Muislam yeyote kwenye huu uzi ambaye anakubaliana na "nyie" kama siyo huyo jamaa wa Musoma ambaye anamuona Nyerere ni nabii.

gombesugu, Ami, Zali la Mentali, Kadogoo, THE BIG SHOW,
Kwani hujui kwamba watu wamejificha kwenye majina ambayo sio halisi? Kwani Ritz ni jina lako halisi? kwa hiyo ulitegemea watu watataja kilahisi imani zao? kama wapo ni mimi na wewe tu.
 
Wickama, katika bandiko lako#13364 umeandika mengi muhimu sana, nakushukuru sana.
Hoja ambayo Mohamed hajaweza kuiongelea ni kuwa endapo EAMWS ilipigwa marufuku huko kwingine ilizuiliwa na nani?

Kuna hoja ya sheikh kupewa wadhaifa na kuukataa, kwa upande wa kumuonyesha Nyerere alivyo mbaya Mohamed anadai wazee wote walitupwa na vyeo kupewa wakristo. Sasa hili lipo wazi na amekaa kimya kwa kutambua kuwa kuligusa kutazua mambo mengine.

Katika mgogoro wa Issilamiya fil Tanganyika washiriki wake ndio wale waliounda AMNUT.
Hoja ambayo Mohamed hajathubutu kuiongelea ni kwanini katika chaguzi AMNUT ilishindwa.

Kuna tatizo moja kubwa sana ambalo wengi hawapendi kulisikia lakini ni vema kulisema.
Leo BAKWATA ikizikwa kabisa bado kutakuwa na migogoro ndani ya chombo kingine.

Hii inatokana na ukweli kuwa waislam wa Tanzania hasa wasomi wa kiislam wameacha mambo yanayowahusu kwa ima wasio na ufahamu au half baked kama tunaoona hapa.
Narudia tena wasomi na watu wenye weledi wamechukua back seat.

Endapo kungekuwa na wasomi walio mbele basi wangeshampiga break Mohamed na wafuasi wake kwa kumwambia aseme na awaambie watu ukweli wa matatizo yao na wala si kueneza usengenyaji, uongo na chuki.
Kwa bahati mbaya wanaogopa pengine kufanya hivyo ni kukufur.

Ujenzi wa hoja wa kundi hili la Mohamed ni wa kiwango cha kusikitisha ndugu Wickama.
Hili wanalomlaumu Nyerere kuhusu Mapinduzi utashangaa kuwa lina sura tatu.
Kundi la kwanza ni hili la Mohamed linalomuandama Nyerere. Kundi la pili ni lile linalosema Mapinduzi daima na kundi la tatu ni la wale wasiokubali kuhusu Nyerere na wasiokubaliana na kundi la pili.
Hoja inajiua hata kabla haijajadiliwa. Pengine utafunguliwa uzi tujadili

Kwahiyo kuna tatizo la kiuongozi na hili linatokana na kukosekana kwa wasomi. Wasomi nina maana watu wenye weledi uwe wa dini au elimu nyingine. Imekuwa proved kuwa Ponda ambaye ni swahiba yake Mohamed hana elimu ya dini wala ya kawaida(dunia). Lakini ndiye yupo katika steering wheel.

Watu wanaonekana kuwa na weledi ndio hawa ambao mstari mmoja unaua hoja nzima. Hapo hamuoni tatizo.
Hawafikiri kwa upana zaidi ya kujifungia na kutunga hadithi! Hao ndio wasengenyaji wakubwa, wenye farki na chuki na ni hao hao wanaoongelea dhulma kana kwamba kuna kadhambi kadogo na dhambi kuubwa!
Bravo mkuu.
 
Kwani hujui kwamba watu wamejificha kwenye majina ambayo sio halisi? Kwani Ritz ni jina lako halisi? kwa hiyo ulitegemea watu watataja kilahisi imani zao? kama wapo ni mimi na wewe tu.
Ni kweli bwana mkubwa hata wewe inawezekana umevaa ngozi ya kondoo kumbe ni chui,wewe ni "ATHIEST KUMBE NI PADRI" Ha ha haa... mkuki kwa nguruwe.
 
Jasusi,
Hapana tabu.

Nakuongezea kitu.
Judith Listowel alikuja Tanganyika 1962 kuja kufanya utafiti wake.

Aliyempokea ni Ally Sykes kwa kuelekezwa na Peter Colmore.

Nimesoma barua za ''aerogram'' ambazo Listowel alikuwa akimuandikia
Ally Sykes kutoka London katika nyaraka za Sykes.

Hizi zipo pamoja na barua za Chief Thomas Marealle na Rashid Kawawa.
Barua hizi zina mengi.

Jasusi najua ungependa kujua vipi Chief Thomas Marealle alivyokuwa
akimchukulia Nyerere.

Zipo habari za Nyerere katika moja ya barua hizi ambapo Chief Marealle
alimtakidi Ally Sykes kuwa rafiki kipenzi wa Nyerere.

Hii ilikuwa miaka michache kabla ya uhuru.

Katika barua hii alimwambia Ally Sykes kuwa ipo siku tukipata uhuru aitataka
aje azunguze habari zile.

Historia ya TANU ina wachezaji wengi, ina visa vingi vya dhahir na vingine
vilivyojificha.

Mzungu hawezi akavipata na ndiyo maana unaona Iliffe na Listowel wana
mambo hawakuweza kuyajua.

Kuna rafiki yangu hapa anataka kunibeza ati siwezi kujua habari za wazee
wangu hata kama niliishinao.

Ati mimi nimemuiga Iliffe.
Mie nimuige Iliffe...

Ama akutukanae...

Namshauri asome kisa cha Abdulwahid Sykes na Dockworkers Union nilichoandika
mimi kisha asome kisa hicho hicho kama alivyokiandika Iliffe aone tulivyoghitilafiana.

Iliffe kamtoa Abdulwahid katika kisa kile.
Mimi nimemrudisha tena kwa taarifa nyingi sana.

Kile kisomo cha Shamba kwa Mohamed Abeid kapuruzia mie nimeeleza hadi
maana kwa nini Waislam wakati wa harakati dhidi ya ukoloni walikuwa hawafanyi
jambo sharti watawasul.

Isomwe Qur'an kwanza ndipo waingie vitani.

Mimi nimemueleza Hamilton jinsi alivyokuwa ndumila kuwili yeye hilo hakulipata.
Yote haya kanihadithia mzee wangu Islam Barakat aliyekuwa bega kwa bega na
Abdu Sykes katika ''labour movement'' kuanzia 1948 hadi 1950 na kashuhudia
migomo yote.

Wanajamvi kisa hicho nimekiweka chote hapa jamvini.
Kisomeni.

Ninayo mengi.

Si kitu Ritz kanishauri nijaribu kuandika riwaya za mapenzi.
Naufikiria ushauri wake kwa bidii sana.

Naanza kupitia vitabu vya Barbara Cartland kwa kuanzia huenda nikapata
vitu vya kunisaidia.

Mohamed Said,

Wewe habari ingine kiboko umewafanya watu wazima waachane na historia ya kivukoni waanze kubukuwa vitabu vya kina Illife na Listowel leo hii.

Cha kuchekesha hawa watu wanataka eti wewe uwaamini hawa wazungu kuliko wazee wetu ambao tulikuwa tunakunywa nao gahawa na kashata huku tunacheza dhumna.

Siku zote walikuwa wanaamini kila kitu Nyerere.
 
Last edited by a moderator:
Hailet maan..UNDER 18 WANAZINI WATAKAVYO HAD WENGINE KUPATA MIMBA NA UKIMWI,LAKIN HAWAKATAZ ZINAA,WANANAHAMASISHA KUTUMIA KONDOM.UKITAKA KUMUA UNDER 18 UMEBAKA..MIAKA 30..DIGRII NYENGINE HIZI.....PUMBA
 
Ndugu Mohamed Said na wafuasi wako,

Kimsingi hoja yako ya Balozi kulihutubia bunge la Tanzania imethibitishwa kuwa ni UONGO tena ni uchochezi mbele ya uso wa kimataifa.


Sasa hebu jisomeeni hapo chini.




UGAIDI WA IRAQ.
Kwa wale wenye kufuatilia historia wataamini kuwa Iraq ni nchi iliyounga mkono vikundi vya kigaidi ulimwenguni na kwamba iliutumia ugaidi kama silaha ya kuwa kandamiza wananchi wake. Matumizi ya ugaidi wa taifa wa serikali ya Saddam Hussein yalikuwa ni suala kila siku la maisha ya Iraq, ambako uhuru wa kutoa maoni ulipingwa bila sababu maalum. Katika ripoti ya mwaka 2002 ya shirika la Amnesty International ilisema watu mbalimbali walikamatwa ikiwa ni pamoja na waliotetea haki za binadamu na maafisa wa jeshi waliotuhumiwa kutaka kuipindua serikali ya Saddam walinyongwa. Wapinzani wengi wa serikali ikiwa ni pamoja na vikundi vya upinzani vilivyo uhamishoni walikamatwa na kufungwa.

Hatima na mahali walipo wote waliokamatwa ni kitendawili. Watu kadha waliongezewa vifungo baada ya mwendo mrefu wa mashtaka katika mahakama. Mateso makubwa wafungwa wa kisiasa waliyapata. Hukumu ya kifo ilitiwa mkazo zaidi, Makosa yaliyostahili hukumu ya kifo ni pamoja na ukahaba, ushoga, mapenzi ya wanandugu na ubakaji. Sheria ya mwaka 2001 inasema wale watakao patikana na hatia ya kumiliki madanguro watauawa kwa upanga. Mateso yameenea! Amnesty inaripoti kwamba wafungwa wa kisiasa na mateka walikabiliwa na mateso makali, miili ya waliokufa ilionyesha alama za mateso makubwa. Mbinu rahisi ya mateso ya kimwili ni pamoja na kutumia umeme, kung'oa kucha au meno, kuchapwa, nk. Yote haya yalifanywa chini ya Saddam Hussen,

Mnamo September, 1971, makumi elfu walitimuliwa na kupelekwa Iran. Mapema mwaka 1973 jeshi la Iraq lilianza kuwahamisha Wakurd kutoka katika vijiji kwenye eneo la Kirkur na katika sekta mbalimbali katika mipaka ya Iraq, Uturuk na Iran. Katika mwaka 1971 na 1972 vyanzo vya usalama wa Taifa vya Iraq vilimuua kiongozi wa wakurd Mullah Mustapha Barzani. Taarifa zinasema kuwa Wakurd karibu 6,000 walikamatwa kufuatia kauli ya Saddam Hussen mwaka 1975, kwa kushukiwa kuwa ni wanachama wa Demokrasia cha Kikurd (Kurdish Democratic Part) na wakapelekwa kwenye kambi maalmu kusini mwa Iraq.

Mnamo mwaka 1976 Wakurdi 7,200 walikamatwa kwa tuhuma kwamba walijihusisha na vikundi vya upinzani na zaidi ya Wakurdi 786 waliripotiwa kukamatwa mwaka 1978. Hayo yote yalifanyika wakati Saddam hajashika hatamu za uongozi nchini Iraq lakini akiwa mstari wambele kuyatenda akiwa kama Luteni jenerali hadi kupewa nishani ya Rafidani (Rafidanian Order First Class) ya kijeshi. Sasa tuangalie alipokuja kushika madaraka na ndipo uthibitisho halisi kuwa utawala wa Sadam Hussein ulikuwa unamiliki silaha za kikemia, Biolojia na nyuklia.

Mwaka 1983 wakati Iraq ilipokuwa inakabiliwa na matatizo kutokana na vita dhidi ya Iran utawala wa chama hicho ukaamua kukaza kamba kuwabana Wakurdi, wakati vita dhidi ya Iran ilipopamba moto serikali iliona hakuna haja ya kuwaleta wakurdi na kuamua kuchukua miji na vijiji vyao hali iliyopelekea wakazi wengi kukimbia. Mnamo Aprili 1987 Wakurdi wengi waliokuwa chini ya Sheik Wasan waliuawa na wengine kujeruhiwa kutokana na gesi ya sumu. Mnamo Jun 1987 sehemu kubwa ya kusini mwa Iraq ambayo watu wengi walikuwa wamekimbilia ilishambuliwa kwa mabomu ya gesi yaliyoporomoshwa na midege ya Iraq.

Mnamo Machi 16/ 1988 mji wa Wakkurd wa Halabja ulishushiwa mvua ya mabomu ya gesi na kusababisha watu 50,000 kufa na wengine 1000 kujeruhiwa kwa mujibu wa taarifa mbalimbali zilizotolewa na mashirika ya kimataifa. Mnamo Agosti 1980 majeshi ya serikali ya Saddam yaliripotiwa kuvamia vijiji kadhaa vya Wakurdi karibu na mji wa Duhok na kuwakamata watu 10,000 baadhi yao walikuwa na majeraha yaliyotokana na milipuko ya mabomu ya kikemikali na kibaiolojia.



Kutoka katika kitabu cha Vita Dhidi ya Ugaid

Na Yericko Nyerere
 
Kikwete ulimtoa wapi Hutu mtoto bwabwa? Au ulimuadapt? Maana anakutesa mno, madawa yeye , ufisadi yeye.. pia ni nanilii..ya waarabu..
 
Ni kweli bwana mkubwa hata wewe inawezekana umevaa ngozi ya kondoo kumbe ni chui,wewe ni "ATHIEST KUMBE NI PADRI" Ha ha haa... mkuki kwa nguruwe.
Boko, ni lini utaipa akili yako nafasi kufanya kazi japo kidogo tu? Padri atakuwaje Atheist? au hujui Atheism ni kitu gani! hakika Mohamed Said hasidi mkubwa atakuua roho na akili mtoto wewe.
 
"Kuna tatizo moja kubwa sana ambalo wengi hawapendi kulisikia lakini ni vema kulisema.
Leo BAKWATA ikizikwa kabisa bado kutakuwa na migogoro ndani ya chombo kingine.

Hii inatokana na ukweli kuwa waislam wa Tanzania hasa wasomi wa kiislam wameacha mambo yanayowahusu kwa ima wasio na ufahamu au half baked kama tunaoona hapa.
Narudia tena wasomi na watu wenye weledi wamechukua back seat.

Endapo kungekuwa na wasomi walio mbele basi wangeshampiga break Mohamed na wafuasi wake kwa kumwambia aseme na awaambie watu ukweli wa matatizo yao na wala si kueneza usengenyaji, uongo na chuki.
Kwa bahati mbaya wanaogopa pengine kufanya hivyo ni kukufur"

hapa nguruvi1 kaelezea core ya tatizo-tutazunguka kote but hapa ndio alfa na omega Mohamed Said umewahi fikiria hii kitu??
 
Last edited by a moderator:
Boko, ni lini utaipa akili yako nafasi kufanya kazi japo kidogo tu? Padri atakuwaje Atheist? au hujui Atheism ni kitu gani! hakika Mohamed Said hasidi mkubwa atakuua roho na akili mtoto wewe.
Tatizo lako ukisoma post zangu unazisoma kwa ushabiki wewe umesema watu wameingia jf kwa majina ambayo sio halisi kwahiyo huwezi kujua imani yake na mimi nikakwambia hata wewe inawezekana unajifanya ni ATHIEST kumbe ni PADRI hebu jitahidi kuwa muungwana kuwa mstaarabu hivyo ufanyavyo sivyo :nono::nono::nono:
 
Back
Top Bottom