Uchambuzi: Shirika la ujasusi la Uisraeli Mossad

Operation dhidi ya kundi la Black September chini ya Golder Meir.

kwa ujumla Mossad imeua wanasayansi wa kiarabu wengi sana nje ya asia, kama Norwei na Australia
 
Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Chapter 6
“BRING EICHMANN DEAD OR ALIVE!”
Mwandishi anasema kuwa mwaka 1957 walipokea ujumbe kutoka Frankfurt kuwa mjerumani mmoja aliyeheshimika sana Dr Fritz Bauer alitaka kutoa taarifa nyeti kwa Mossad.Fritz alikuwa mjerumani mwenye asili ya Israel ambaye aliwekwa kwenye kambi za mateso kabla ya kutoroka,baadae akawa mpinzani mkubwa wa sera za chama cha Nazi
Huyu dr Fritz alirejea Ujerumani baada ya anguko la Hitler na alikuwa msitari wa mbele katika kuhakikisha wote walioshiriki wanafikishwa mbele ya sharia,hata hivo hakuridhishwa na jinsi mamlaka za ujerumani zilivoshughulikia swala zima.
Sasa basi huyu Dr Frits alikuwa na taarifa nyeti,ambayo aliiwasilisha Mossad kuhusu bwana Eichmann,bwana Eichman alikuwa mchinjaji na muuaji maarufu wakati wa Hitler,na baada ya anguko la Hitler alikimbilia Argentina.Ni kwamba baada ya Hitler kujiua Israel ilianzisha operesheni ya siri sana kwa lengo la kulipiza kisasi kwa wahusika wote walioshiriki kuwaua wayahudi wenzao.Na wengi wa wafuasi wa Nazi walikimbilia Argentina wakabadili majina na mfumo mzima wa maisha.Hivo basi bwana Frits alitoa taarifa za sehemu anakoishi Eichman kufuatia kujulishwa nab inti yake ambaye alikuwa anaishi huko sasa Mossad wakaanzisha rasmi operesheni ya kumkamata na kumrejesha Eichman nchini kwao akiwa hai au mfu.Mossad walianza operesheni hii kutafuta hasa kama kweli Eichman alikuwa bado anaishi baada ya upepelezi wa muda mrefu waligundua kitongoji ambacho alikuwa anaishi akiwa na jina lingine na utambulisho tofauti kabisa ambao ilikuwa sio rahisi kugundulika
Sasa basi Mossad walimpa kazi jasusi mmoja aliyeitwa Ahoron alikuwa kijana mdogo mwenye akili nyingi,alifika Argentina katika jiji la Buenos Aires,hapa aliweza kupata taarifa za sehemu bwana Eichman alikokuwa anaishi,na jina jipya alilojibadilisha alikuwa anaitwa Ricardo Klement,baada ya kufika mtaa walikoelekezwa walikuta nyumba ikiwa haina mtu ni gofu,hapa ilibidi sasa wao Mossad waende kwenye wakala wa kupeleka vifurushi wakatengeneza zawadi ya na kumtaka wakala awasilishe kwa muhusika,hii kampuni ya uwakala ikaanza kazi ya kutafuta makazi ya Bwana Eichman (Ricardo) na baada ya siku mbili wakafanikiwa kupapata na kumkabidhi mzigo wake,wakati wote agenti wa siri wa Mossad alikuwa nyuma kumfuatilia yule wakala wa kusambaza zawadi.Sasa baada ya kupata nyumbani kwa bwana Ricardo yule Jasusi alifika hapo kesho yake akiwa amevalia suti ya kimarekani ambako alijitambulisha kama mfanyabiashara kutoka kampuni moja kutoka USA na wanataka kuwekeza kiwanda hapo,hivo wanataka kununua eneo lote hilo kwa matumizi yao,wakati akijieleza alikuwa na camera ndogo ambayo haikuonekana akawa anapiga picha mbalimbali maeneo hayo,yule jirani akajibu kuwa hawatauza ila ngoja aongee na familia yake kesho yake angetoa majibu.Bwana Ahoron Jasus wa Mossad alirejea alikofikia na kwa kutumia uzoefu wake aliingiza zile picha kwenye mfumo wa masjila ya mji wa Buenos Aires ambako ilionyesha kuwa ni eneo binafsi mali ya Ms.Vera Liebl de Eichmann,huu ubini ukawa moja ya kielelezo muhimu kuwa mwenye nyumba ni ndugu na Ricardo mtu wanayemtafuta>Baadae walikuja kugundua kuwa Vera ni mke wa Eichman ingawa walishaachana kitambo ila kwa tamaduni za Argentina bado mke ataendelea kutumia ubini wa mumewe.
Mwandishi anasema kuwa baada ya kugundua makazi haya ilitumwa timu ya watu 12,ili kumkamata na ilipendekezwa akamatwe na apelekwe Israel akiwa hai yaani alikuwa na dhamani kubwa akiwa hai kuliko akiwa mfu.Mossad wana tabia ya kuingia kwenye nchi nyingine kijasusi na mar azote hutokea nchi jirani…huwa na paspoti za mataifa mengine ili kuficha utambulisho wao,na huingia kama watalii au wawekezaji.Sasa hawa watu 12 wote waliingia Argentina kila mmoja kutoka sehemu tofauti na wakiwa na paspoti tofauti,walipofika Argentina walikutana na kutengeneza NGOME na kugawana majukumu ya namna bora ya kumteka Eichman..Sasa basi Mossad wakaweka mtego na ikatokea bahati nzuri kulikuwa na maadhimisho ya kitaofa nchini Argentina ambako Serikali ya Israel ilikuwa inawakilishwa na waziri wake wa Elimu,hii ilikuwa fursa kubwa kwa Mossad hivo wakaazimia kuwa waziri asafiri na ndege binafsi,hili jambo lilifanywa bila waziri kujulishwa msingi wake,kuanzia rubani hadi wahudumu wa ndege walichaguliwa na Mossad na wengi walikuwa majasusi.Kule nchini Argentina kile kikosi cha watu kumi na mbili kiliendelea na mipango na walikodisha apartment ambayo iliwekewa mfumo wote wa ulinzi na uokozi,ikiwepo hadi handaki la kutoroka ikitokea polisi wa Argentina wamegundua kuhusu mpango kabla
Sasa mpango kamili ukawa kama ifuatavyo siku ya kutekwa Eichman angekamatwa akiwa anaingia nyumbani kwake,Mossad walikodisha gari mbili moja ya kumteka na moja kwa ajili ya ulinzi,ile ya kumteka ingeegeshwa nje kidogo ya nyumbani kwa Eichman alafu ingefanywa kama vile imeharibika na moja ya Mossad angeingia chini kama anaitengeneza(Kumbuka walishamfuatilia Eichman kwa muda mrefu na walikuwa wanajua muda wa kuingia nyumbani jioni)siku ya tukio walipanga kumsubiri hadi saa mbili kamili usiku awe amefika na ikatokea kuwa hajatokea basi waondoke,wale jamaa wakasubiri hadi saa mbili na robo Eichman alikuwa hajatokea,wakaongeza dakika kumi Zaidi wakiwa katika kukata tamaa ghafla wakaona basi limeshusha abiria kumbe ni Eichman sasa yule jasusi aliyepangwa akamsemesha Eichman alipogeuza shingo akarukiwa chapu na kuingizwa kwenye gari wakamtaka atii sharia bila shuruti…gari zikaondoka mwendo wa kasi hadi kwenye ile Apartment…baada ya kumgagua kwa kina wakajiridhisha kwa kina kuwa ndie muhusika wao..baadae alihojiwa majina yake,na namba yake ya Nazi,namba ya kiatu etc,bwana Eichman alitoa ushirikiano mkubwa kujibu maswali yote.Eichmann alieleza yote baada ya kugundua kuwa ametiwa nguvuni na watu ambao alikuwa amewatoroka kwa miaka mingi,alieleza jinsi alivojibadilisha majina na kupata Uraia wa Argentina na jinsi ambavo chama cha Nazi kilikuwa kinawaunga mkono kupitia taasisi zao za siri,alifikiri kuwa sasa angemalizia maisha yaliyobaki kwa Amani
Sasa ikatokea kitu ambacho hakikutarajiwa ile sherehe iilikuwa ifanyike May 10 ikasogezwa mbele hadi Mei 19,hivo walilazimika kukaa na mteka kwa siku tisa jambo ambalo ni hatari sana.Kiongozi wa hii operesheni akalazimika kuwaelekeza wale majasusi waliomshikilia Eichman kuwa ikatokea wakakamatwa na polisi basi wajitambulishe kwa utambilisho rasmi kuwa wao ni Waisrael wamemkamata mtuhumiwa namba moja wa Nazi(kumbuka hawa majasusi walikuwa na utambulisho tofauti tofauti)..pia ikatengeneza document feki inayoonyesha kuwa Eichman amekiri makossa yake na ameomba kupelekwa Israel ili akashtakiwe mahakamani
I, the undersigned Adolf Eichmann, of my own free will hereby declare: now that my real identity has been discovered, I recognize that there is no further use in trying to evade the course of justice. I agree to be taken to Israel and stand trial before a qualified tribunal. It is understood that I shall be given the assistance of an advocate and that I shall be permitted to lay before the court, without travesty of the facts, an account of the last years of my service in Germany, so that a truthful description of those events may be passed on to the future generations.I am making this declaration of my own accord. Nothing has been promised to me and I have not been threatened. My desire is to find inner peace at last. As I am unable to remember all the details,and may become confused when stating the facts, I ask that the relevant documents and testimonies be placed at my disposal to help me in my efforts to establish the truth. Adolf Eichmann, Buenos Aires,May 1960.
This declaration, of course, had no legal validity.
Mei 20 ndege ilipangwa kuondoka,hivo Mossad walimvalisha Eichman kama muhudumu wa ndege na wakatengeneza ripoti feki ya kitabibu kuwa muhudumu ameugua na yupo hoi kwenye kiti cha kubebea wagonjwa.Eichman aliingizwa uwanjani kwa utaratibu huo(Mossad walikuwa wanatembea na kila kitu ikiwepo mtambo maalum wa kutengeneza kila aina ya nyaraka iliyohitajika ikiwepo vitambulisho,pamoja na pasi mbalimbali).Mwaka 1961 Eichman alifikishwa kortini kujibu tuhuma zake mahakama ilimkuta na hatia na alihukumiwa kunyongwa hadi kufa,haya ndio maneno yake ya mwisho
: “We’ll meet again …I have lived,believing in God …I obeyed the laws of war and was loyal to my flag …”
 
Daaah uzi mzuri ila kuna namna maneno yamekosewa mtu inabidi utumie sana ugali kusoma
 
Back
Top Bottom