bigcell
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 219
- 60
Wakati ndo natoka kupiga kura nafika tu home nikafungulia choice fm ambayo bbc idhaa ya kiswahili wanaitumia kurusha matangazo maalum ya uchaguzi wa tanzania, nikasikia wanatangaza kuwa leo asubuhi saa 12 muda ambao wananchi wanakwenda kupiga kura, kuna watu ambao idadi yao hakutajwa wameshtukiwa wakiwa wamebeba masanduku ya kura yakiwa na karatasi za kura zikiwa hazina muhuri wa nec, baada ya kuona mambo mazito wakawachomoka jamaa waliowakamata na kutokomea kusikojulikana.