VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Katika hili sijifichi nyuma ya pazia wala kujibanza nyuma ya ukuta. Najitokeza na kumpongeza. Niko na Rais na Mwenyekiti wangu wa CCM bega kwa bega bila kutega au kuzuga. Namuunga mkono usio na kikomo. Namuunga kwa moyo kuliko maneno. Nipo na Rais wangu; nipo na Mwenyekiti wangu wa CCM. Sambamba.
Naungana na Rais na Mwenyekiti wangu kuinyooshea kidole chenye kilele na kelele Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG). Kuhusu kuchakachua nyaraka zinazowasilishwa Ofisini hapo. Inaletwa hivi, inatoka vile. Hata sisi TLS tulipeleka Kanuni zetu za Uchaguzi wa AG na zikachakachuliwa. Ingawa Rais hakulaani, maneno yake ya jana yanatuunga mkono.
AG anachakachua kilichoandikwa na kuandika chake. Anawaandikia Wabunge na wanachama wa TLS. Anawalisha maneno. Uchakachuaji katika sheria za mafuta na nyinginezo hauna tofauti na uchakachuaji uliofanyika kwenye Kanuni za Uchaguzi za TLS. Kuandika ya kwake kwa malengo yake. Kumbe Ofisi ya AG imekubuhu na kuzoea kuchakachua. Rais ameliona na kulisema.
Rais na Mwenyekiti wangu, uchakachuaji wa sheria na Kanuni haufanyiki kwa bahati mbaya. Kanuni za TLS zilichakachuliwa ili kuwazuia 'wanaharakati na wanasiasa' kugombea ndani ya TLS. Hata Sheria huchakachuliwa ili madili makubwamakubwa yaendelee kumea na kufanikiwa. Ofisi ya AG imulikwe. Ianikwe. Iwajibishwe. Zilizochakachuliwa zibainishwe. Zirekebishwe.
Bunge lipewe taarifa badala ya kujadili na kuamua kuhusu bajeti!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Naungana na Rais na Mwenyekiti wangu kuinyooshea kidole chenye kilele na kelele Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG). Kuhusu kuchakachua nyaraka zinazowasilishwa Ofisini hapo. Inaletwa hivi, inatoka vile. Hata sisi TLS tulipeleka Kanuni zetu za Uchaguzi wa AG na zikachakachuliwa. Ingawa Rais hakulaani, maneno yake ya jana yanatuunga mkono.
AG anachakachua kilichoandikwa na kuandika chake. Anawaandikia Wabunge na wanachama wa TLS. Anawalisha maneno. Uchakachuaji katika sheria za mafuta na nyinginezo hauna tofauti na uchakachuaji uliofanyika kwenye Kanuni za Uchaguzi za TLS. Kuandika ya kwake kwa malengo yake. Kumbe Ofisi ya AG imekubuhu na kuzoea kuchakachua. Rais ameliona na kulisema.
Rais na Mwenyekiti wangu, uchakachuaji wa sheria na Kanuni haufanyiki kwa bahati mbaya. Kanuni za TLS zilichakachuliwa ili kuwazuia 'wanaharakati na wanasiasa' kugombea ndani ya TLS. Hata Sheria huchakachuliwa ili madili makubwamakubwa yaendelee kumea na kufanikiwa. Ofisi ya AG imulikwe. Ianikwe. Iwajibishwe. Zilizochakachuliwa zibainishwe. Zirekebishwe.
Bunge lipewe taarifa badala ya kujadili na kuamua kuhusu bajeti!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam