Fisadi Mtoto
JF-Expert Member
- Jan 7, 2008
- 639
- 79
Matokeo ndio yamemaliza kutolewa Mama Nagu kapata kura mia sita na alobaini na mh waziri mkuu mstaafu na mgombea urais mtarajiwa kapata kura mia nne ishirini.
TAKUKURU yawafuata Sumaye, Nagu Hanang
na Mwandishi wetu, Katesh
Tanzania Daima
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imeingia kwa siri wilayani Hanang' kukabiliana na vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa kutafuta wajumbe wa halmashauri kuu yake ya Taifa (NEC), wilayani humo, imefahamika.
Hatua hiyo ya TAKUKURU imekuja baada ya kuwepo kwa taarifa za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika kampeni, vinavyodaiwa kufanywa na mmoja wa wanaowania nafasi ya mjumbe wa NEC kutoka wilayani Hanang'
CCM imewapitisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dkt. Mary Nagu na Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye kuwania nafasi ya mjumbe wa NEC katika wilaya hiyo.
Kumekua na madai mazito kuhusiana na ugawaji fedha unaofanywa na mgombea huyo na kwamba anatumia mbinu ya kugawa fedha hizo kwa njia ya mtandao.
Akizungumzia madai hayo ya rushwa, Kaimu Kamanda wa TAKUKURU wilaya ya Hanang' Samson Sanga alikataa kuzungumzia kuhusu taasisi yake kufanya kazi zake kwa siri kwa maelezo kwamba kwa sasa ofisi yake haiwezi kuzungumzia suala hilo.
Wiki hii, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Dk. Edward Hoseah alinukuliwa akisema taasisi yake inafuatilia kwa karibu uchaguzi huo ndani ya CCM ili kubaini watu wanaotumia rushwa.
Dk. Hoseah alitoa kauli hiyo akijibu hoja mbalimbali za washiriki wa kongamano la kujadili utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango wa kupambana na rushwa nchini na mapendekezo yanayopaswa kuzingatiwa katika utekelezaji wa mpango wa awamu ya tatu (2012 – 2016).
"Tatizo ni kwamba wagombea wengi wa nafasi ya uongozi wamekuwa wakijiandaa kutoa rushwa wakati wa uchaguzi na kwa bahati mbaya hata wananchi ambao ni wapiga kura ni kama wanajiandaa kupokea rushwa kila uchaguzi unapokaribia, hili ni tatizo kubwa," alisema Dk Hosseah na kuongeza:
"Tunaendelea kufuatilia, lakini ni kazi kubwa kwelikweli kwa mfano, sasa tunafuatilia uchaguzi wa ndani wa CCM na tunafanya hivi ili kuhakikisha kwamba hatupati viongozi wanaotokana na rushwa, maana tukiwa na viongozi wa aina hii hatuwezi kushinda vita hivi."
Katika kikao kilichofanyika Jumapili ya Septemba 2, mwaka huu na kuongozwa na katibu wa CCM Wilaya ya Hanang' Allan Kingazi, wajumbe wa kikao hicho walipitisha jina la Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye na Leonsi Marmo huku Dkt Nagu akitoswa kufuatia kudaiwa kuwa na majukumu mengi ya kikazi ikiwemo ubunge na uwaziri.
Wakizungumzia maamuzi ya vikao vya juu vilivyopitisha jina la Dk. Nagu kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo, baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa ya Wilaya ya Hanang' walioomba kutotajwa majina yao gazetini walisema kamati hiyo haikuwatendea haki.
"Kamati kuu haikutenda haki kabisa, kwa kuwa imepuuza maamuzi yetu, haiwezekani sisi tufanye maamuzi tena kwa kufuata kanuni za CCM ilizotunga yenyewe halafu maamuzi yetu yabadilishwe na kuonekana sio sahihi, huku ndio kunakopeleka pabaya hiki chama,"alisema mmoja wa wajumbe waliodaiwa kupigia kura jina la Dkt.Nagu kutopitishwa katika kikao kilichofanyika Septemba 2 mwaka huu.