Wana JF nemekuwa nikiangalia hali ya kisiasa hapa nchini inavyokenda na jinsi CCM walivyopoteza umaarufu na mbinu wanazotumia kuiuwa CHADEMA zinakwama siku hadi siku na kwasasa wanatafuta silaha za maangamizi kwa kukihusisha na uhaini. Nimepata hisia kuwa ujanja utakaofuata wakishindwa kuiuwa CHADEMA itakuwa nikuchelewesha kiufundi suala la kuwa na tume huru (katiba mpya) ili uchaguzi 2015 ufanyike bila katiba mpya kwa sababu zozote zile ikitokea hivyo tufanyeje? tuelimishane.