Uchaguzi Mkuu October 2015 kutumia Katiba ya 1977 bila mabadiliko, Watanzania bado tumelala!!

shumanice

Member
Jul 21, 2011
64
25
Salaam wanajamvi.

Awali ya yote naomba niwakumbushe kuwa siku si nyingi sana zilizopita tulikuwa na mchakato wa Katiba ambao ulikwama na hakuna ajuae ulipokwamia na "what is next" yake!. Nikikumbuka vizuri wakati mkulu anatoa hotuba zake (ile ya kutangaza mchakato wa kuanza kukusanya maoni na ule wa uzinduzi wa BMK) moja ya kipaumbele ilikuwa ni kuwapa Watanzania Katiba mpya kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Kwa maana nyingine ni kwamba uchaguzi wa mwaka huu ulitakiwa kufanyika chini ya Katiba mpya ambayo miongoni mwa mambo "tuliyopendekeza" sisi wananchi ni pamoja na mabadiliko kwenye vipengere muhimu. Kwa mfano suala kama la kuwa na tume huru ya uchaguzi, kuruhusu mgombea binafsi, matokeo kuhojiwa, nk ni baadhi tu ya yale mambo muhimu tuliyohitaji yaingie kwenye katiba.

Sasa mchakato umekwama kama nilivyosema hapo juu na hakuna ajuaye ulipokwamia!! Lakini harakati za utangazaji wa nia unaendelea; ishara ya kwamba uchaguzi upo pale pale. Sina shaka kuwa uchaguzi utafanyika kwa mujibu wa Katiba ya 1977.

Lakini ikumbukwe kuwa viongozi wengi wakiowemo wa upinzani na wachama tawala walikuwa wakiunga baadhi ya vipengere vya Katiba pendekezwa vikiwemo tajwa hapo juu. Cha ajabu ni kwamba hakuna anaekumbuka tena!!! Woote (watangaza nia na wapiga kura) tumesahau kuwa uchaguzi utafanyika chini ya Katiba ya 1977 ambayo haijafanyiwa mabadiliko na hivyo kutokuwa na tume huru ya uchaguzi, wala hakutakuwa na mgombea huru, nk, badala yake tumekalia kushabikia tuu watangaza nia bila hata kufuatilia hizo nia zao ni dhati kweli?.

Kwanini nasema hakutakuwa na mabadiliko?
Bunge la sasa ndo la mwisho na sijaona mbunge hata mmoja mwenye nia ya kuwasilisha hoja binafsi ya kuomba Katiba kufanyiwa mabadiliko. Kila mmoja yupo busy majimbini na kutangaza nia. Sina hakika bunge likivunjwa kuna namna ya kuliitisha ili lifanye mabadiliko ya Katiba. Kwa maana hiyo tujiandae kwa kila kitakachotokea wakati wa uchaguzi kwani I see "business as usual". Ama kweli watanzania bado tumelala!!!!
 
Moja ya ajenda muhimu ya upinzani ilikuwa ni hii ya mabadiliko ya katiba ya 1977 hasa Tume Huru ya Uchaguzi, cha ajabu wao wenyewe wako kimya mpaka hivi sasa. Kwa Tume hii isiyokuwa Huru uchaguzi utakuwa wa huru na haki kweli?
 
Moja ya ajenda muhimu ya upinzani ilikuwa ni hii ya mabadiliko ya katiba ya 1977 hasa Tume Huru ya Uchaguzi, cha ajabu wao wenyewe wako kimya mpaka hivi sasa. Kwa Tume hii isiyokuwa Huru uchaguzi utakuwa wa huru na haki kweli?
MAKUBALIANO YAO VIONGOZI WA VYAMA CHINI YA TCID KWANI BADO YAPO HAI?...UKAWA JE WAko TAYARI KUPOKEA MATOKEO KTK MAZINGIRA YALEYALE WANAYOYALALMIKIA KILA UCHWAO?....
 
Hakuna kitu ccm wanaweza kufanya mambo mazur katika Nchi hii zaid ya ufisad tu,
Naweza sema serikal hii ya ccm inaweza kuwa Number Moja dunian kwa Rushwa na ufisad,
Ccm hiyo ni ishara kabisa wamechoka kwakwl hata Rais alisema amechoka anataman mda wake uishe akachunge Mbuz huko kwao Chalinze na oct utawala wa ccm ndo unaanguk, UKAWA kushika Nchi hii oct
 
wajanja tunajua kilichokuwa nyuma ya kile akina slaa mbowe na wapambe wao walichokuwa wakipigia kelele. hilo la tume huru ni porojo tu kama porojo zingine.

Salaam wanajamvi.

Awali ya yote naomba niwakumbushe kuwa siku si nyingi sana zilizopita tulikuwa na mchakato wa Katiba ambao ulikwama na hakuna ajuae ulipokwamia na "what is next" yake!. Nikikumbuka vizuri wakati mkulu anatoa hotuba zake (ile ya kutangaza mchakato wa kuanza kukusanya maoni na ule wa uzinduzi wa BMK) moja ya kipaumbele ilikuwa ni kuwapa Watanzania Katiba mpya kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015. Kwa maana nyingine ni kwamba uchaguzi wa mwaka huu ulitakiwa kufanyika chini ya Katiba mpya ambayo miongoni mwa mambo "tuliyopendekeza" sisi wananchi ni pamoja na mabadiliko kwenye vipengere muhimu. Kwa mfano suala kama la kuwa na tume huru ya uchaguzi, kuruhusu mgombea binafsi, matokeo kuhojiwa, nk ni baadhi tu ya yale mambo muhimu tuliyohitaji yaingie kwenye katiba.

Sasa mchakato umekwama kama nilivyosema hapo juu na hakuna ajuaye ulipokwamia!! Lakini harakati za utangazaji wa nia unaendelea; ishara ya kwamba uchaguzi upo pale pale. Sina shaka kuwa uchaguzi utafanyika kwa mujibu wa Katiba ya 1977.

Lakini ikumbukwe kuwa viongozi wengi wakiowemo wa upinzani na wachama tawala walikuwa wakiunga baadhi ya vipengere vya Katiba pendekezwa vikiwemo tajwa hapo juu. Cha ajabu ni kwamba hakuna anaekumbuka tena!!! Woote (watangaza nia na wapiga kura) tumesahau kuwa uchaguzi utafanyika chini ya Katiba ya 1977 ambayo haijafanyiwa mabadiliko na hivyo kutokuwa na tume huru ya uchaguzi, wala hakutakuwa na mgombea huru, nk, badala yake tumekalia kushabikia tuu watangaza nia bila hata kufuatilia hizo nia zao ni dhati kweli?.

Kwanini nasema hakutakuwa na mabadiliko?
Bunge la sasa ndo la mwisho na sijaona mbunge hata mmoja mwenye nia ya kuwasilisha hoja binafsi ya kuomba Katiba kufanyiwa mabadiliko. Kila mmoja yupo busy majimbini na kutangaza nia. Sina hakika bunge likivunjwa kuna namna ya kuliitisha ili lifanye mabadiliko ya Katiba. Kwa maana hiyo tujiandae kwa kila kitakachotokea wakati wa uchaguzi kwani I see "business as usual". Ama kweli watanzania bado tumelala!!!!
 
CCM waliahidi mbele ya TCD kuwa watapitia katiba, na walisema kwa watanzania pia, kwahiyo tunawasubiri watekeleze, hata wasipotekeleza mwaka huu kwa katika hiyohiyo tutawaondoa.
 
wajanja tunajua kilichokuwa nyuma ya kile akina slaa mbowe na wapambe wao walichokuwa wakipigia kelele. hilo la tume huru ni porojo tu kama porojo zingine.
Kwako wewe ujanja ni upi? Fafanua ili sote tulijue hilo.
 
MAKUBALIANO YAO VIONGOZI WA VYAMA CHINI YA TCID KWANI BADO YAPO HAI?...UKAWA JE WAko TAYARI KUPOKEA MATOKEO KTK MAZINGIRA YALEYALE WANAYOYALALMIKIA KILA UCHWAO?....

Mkuu NDOFU hili ndilo swali la kujiuliza. Maana sijaskia Mbunge hata mmoja wa UKAWA mwenye nia ya kupeleka hoja binafsi ya marekebisho ya Katiba!!! Ina maana wameridhika au wanasubiri washindwe kwa hila ndipo waje kulalamika kwa wananchi?
 
Back
Top Bottom