Uchaguzi Mkuu ni Kipindi Cha Neema kwa Media!. Ni Kipindi cha Mavuno!. Jee Bahasha Hizi Ni Halali?!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,494
113,590
Wanabodi,

Kwanza naomba nikiri kuwa nimeandika uzi huu kwa kuwa inspired na mwana jf huyu,
Milion mia saba kila baada ya miezi miwili? Na watu wa media waongezewe posho? Huu ni muda wa brother wangu Pasco kupiga hela.

Mkuu, Steven Robert Masatu, kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, na mafanikio kwenye kilimo yanategemea msimu, kuna msimu wa mvua, ni kipindi cha kulima, kupanda na kupalilia, kuna msimu wa kiangazi ni wakati wa kuvuna, ila pia kuna wakati kunatokea ukame, hakuna mvua, hakuna mazao hakuna kuvuna na kinachofuatia ni baa la njaa!. Pia kuna wakati kunanyesha mvua kubwa zaidi kupitiliza, hadi kuleta maafa ya mafuriko, kama elnino, lakini mavuno ya maeneo ya mabondeni baada ya elnino ni mavuno makubwa ajabu, kutokana na kurutubishwa kwa siltation ya elnino!.

Kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu, ndio kipindi cha neema kwa media na waandishi!, huu ndio wakati wetu wa mavuno, kama ni mvua hizi sasa mvua za elnino!.

Zamani enzi za chama kimoja, kwa media kuripoti uchaguzi mkuu, ilikuwa bure!, media ndio zilikuwa zinawagharimia waandishi wake kuripoti uchaguzi. Vyama vingi vilipoanza, bure ikaendelea ila ili chama kipate preferential coverage rupia ilianza kupenyezwa kidogo kidogo kwa siri and unofficial.

Kuanzia uchaguzi wa 2005, media campaign zilianza kuwa official na waandishi kulipwa sasa ilikuwa rasmi, mfano gazeti la Mtanzania lilitake side na kumsaidia mgombea mmoja tuu fulani ndani ya CCM na lilifanya kazi kubwa kuwaangamiza wagombea wengine wowote tishio, hata ikibidi kuwatungia story za uongo hadi kutengeneza picha za photoshop!, kazi hii nzuri ya media campain ilizaa matunda mema, baadhi ya wale viongozi wa kampeni hizi kuzawadiwa kuanzia ukurugenzi, hadi ukuu wa wilaya!.

Uchaguzi wa 2010, sasa ikawa sio CCM pekee bali hadi Chadema nayo ikalipa waandishi kuzunguka na mgombea wao kwenye chopa!.

Uchaguzi wa mwaka huu, neema sasa ni kubwa zaidi, CCM yenye pesa nyingi zaidi ndio itaongoza kwa kuwalipa waandishi wengi na kununua media nyingi!. CCM itanunua airtime na kununua waandishi officially from the media houses kuzunguka na wagombea wake wa urais. Ukawa nao this time watalipa media kwa media kuzunguka na mgombea wake!.

Vyama vipya kwa ACT vinavyotambua the power of media, nao, watawalipa waandishi kuzunguka na mgombea wake!.

Baadhi ya wagombea individually wenye ukwasi mkubwa wa fedha kama kina Nimrod Mkono, Mohamed Dewji, Edward Lowassa etc, nao wataunda mitandao yao ya media officially or unofficially kuwaripotia na kote huku ni fedha tuu ndio itazungumza!.

Hongereni sana wana media, hiki ni kipindi chenu cha mavuno, tukae mkao wa kula!, huwezi jua, hata mimi labda hali ya kale ka usafiri kangu ka boda boda kalikopata ajali, huenda kanaweza kufufuka au hata kubadili kutoka boda boda hadi bajaj!.

Swali la msingi la kujiuliza ni Jee, bahasha hizi wanazolipwa media na wana siasa au vyama vya siasa ni halali?, Jee ni sahihi kwa vyama na wagombea wenye pesa, kutumia pesa zao, kununua media na kuwalipa waandishi?!.

Hili suala la waandishi wa habari na bahasha, nimeishalizungumza sana hapa
Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa.

Pasco
 
Ndio taifa lilipofikia hapa, wengine tunachosubiri ni timing tu tuone nini tugawane maana wakubwa wameshatuzingua vya kutosha............punde si punde walalahoi tutaanza msako wa mkubwa kwa mkubwa........ili tuheshimiane vizuri!
 
Hii nchi wanasiasa wamezidi sana dharau..........wao ndo waseme tuandikiwe nini kwenye news, kisa ujeuri wa kodi zetu shabaash! Iko siku yao!
 
tunasubiri bahasha za ccm tupige hela ...ila uamuzi uko kwenye sanduku la kura....kama kuna mgombea alitumia media na matangazo na kumwaga rupia za kutosha basi alikuwa Masha aliekuwa waziri wa mambo ya ndani...jamaa alimwaga hela huyu ...ila kura hazikutosha
 
Lakin haya hata Ulaya yapo sana tuu kwenye chaguzi zao

Mie ninachojiuliza ivi wewe kama mwandish wa habari unakwenda kutunga story ya uongo juu ya unayempamba ivi kweli unakuwa uko fair kwa wale unaowapelekea taarifa??

Mie huwaga naona wenzetu wanatangeneza documentary za wagombea wao, ambazo ni true events alizo fanya, lkn sisi apo adi wewe mwenywe umekiri kuwa huwa mnatunga uongo............hii ni aibu sana

Hebu tujiulize Pasco mtu kama mie apa nakuja kwamba nataka kugombea ubunge nakupa bahasha, sina la maana ata moja nililowah kufanya ata tu kuanzisha kikundi cha vikoba afu wee unakuja kufake ni mlezi mzuri wa wanawake mwanzilish wa kikund vikoba cha wanawake na mpaka sasa kikundi hili kina miliki shule (ambayo kimsingi haipo) na chuo cha ufundi stadi ambacho nacho hakipo.....
taarifa kama hii inaenda kwa watu wangapi, wangapi ambao unawapa matumaini ya uongo kumbe mtu mwenyew ata tu kumiliki akaunti yangu ya benki imenishinda manake ninakazi ya kujiibia mwenyewe kila siku...............wont you feel shame of it??

pokeen bahasha lkn msituhadae na nataman ile sheria iwe imepita ili ikibainika nyie na mnaowapamba mwende kwa pilato kwanza
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi, Kwanza naomba nikiri kuwa nimeandika uzi huu kwa kuwa inspired na mwana jf huyu, Mkuu, Steven Robert Masatu, kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, na mafanikio kwenye kilimo yanategemea msimu, kuna msimu wa mvua, ni kipindi cha kulima, kupanda na kupalilia, kuna msimu wa kiangazi ni wakati wa kuvuna, ila pia kuna wakati kunatokea ukame, hakuna mvua, hakuna mazao hakuna kuvuna na kinachofuatia ni baa la njaa!. Pia kuna wakati kunanyesha mvua kubwa zaidi kupitiliza, hadi kuleta maafa ya mafuriko, kama elnino, lakini mavuno ya maeneo ya mabondeni baada ya elnino ni mavuno makubwa ajabu, kutokana na kurutubishwa kwa siltation ya elnino!. Kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu, ndio kipindi cha neema kwa media na waandishi!, huu ndio wakati wetu wa mavuno, kama ni nvua hizi sasa ni elnino!. Zamani enzi za chama kimoja, kwa media kuripoti uchaguzi mkuu, ilikuwa bure!, media ndio zilikuwa zinawagharimia waandishi wake kuripoti uchaguzi. Vyama vingi vilipoanza, bure ikaendelea ila ili chama kipate preferential coverage rupia ilianza kupenyezwa kidogo kidogo kwa siri and unofficial. Kuanzia uchaguzi wa 2005, media campaign zilianza kuwa official na waandishi kulipwa sasa ilikuwa rasmi, mfano gazeti la Mtanzania lilitake side na kumsaidia mgombea mmoja tuu fulani ndani ya CCM na lilifanya kazi kubwa kuwaangamiza wagombea wengine wowote tishio, hata ikibidi kuwatungia story za uongo hadi kutengeneza picha za photoshop!, kazi hii nzuri ya media campain ilizaa matunda mema, baadhi ya wale viongozi wa kampeni hizi kuzawadiwa kuanzia ukurugenzi, hadi ukuu wa wilaya!. Uchaguzi wa 2010, sasa ikawa sio CCM pekee bali hadi Chadema nayo ikalipa waandishi kuzunguka na mgombea wao kwenye chopa!. Uchaguzi wa mwaka huu, neema sasa ni kubwa zaidi, CCM yenye pesa nyingi zaidi ndio itaongoza kwa kuwalipa waandishi wengi na kununua media nyingi!. CCM itanunua airtime na kununua waandishi officially from the media houses kuzunguka na wagombea wake wa urais. Ukawa nao this time watalipa media kwa media kuzunguka na mgombea wake!. Vyama vipya kwa ACT vinavyotambua the power of media, nao, watawalipa waandishi kuzunguka na mgombea wake!. Baadhi ya wagombea individually wenye ukwasi mkubwa wa fedha kama kina Nimrod Mkono, Mohamed Dewji, Edward Lowassa etc, nao wataunda mitandao yao ya media officially or unofficially kuwaripotia na kote huku ni fedha tuu ndio itazungumza!. Hongereni sana wana media, hiki ni kipindi chenu cha mavuno, tukae mkao wa kula!, huwezi jua, hata mimi labda hali ya kale ka usafiri kangu ka boda boda kalikopata ajali, huenda kanaweza kufufuka au hata kubadili kutoka boda boda hadi bajaj!. Swali la msingi la kujiuliza ni Jee, bahasha hizi wanazolipwa media na wana siasa au vyama vya siasa ni halali?, Jee ni sahihi kwa vyama na wagombea wenye pesa, kutumia pesa zao, kununua media na kuwalipa waandishi?!. Hili suala la waandishi wa habari na bahasha, nimeishalizungumza sana hapa Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa. Pasco
pasco ACT ndio wanafahamu sana umuhimu wa media?wengine pia tunafahamu hadi hasara zake na jinsi zinavyokuja.
 
Wanabodi,

Kwanza naomba nikiri kuwa nimeandika uzi huu kwa kuwa inspired na mwana jf huyu,

Mkuu, Steven Robert Masatu, kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, na mafanikio kwenye kilimo yanategemea msimu, kuna msimu wa mvua, ni kipindi cha kulima, kupanda na kupalilia, kuna msimu wa kiangazi ni wakati wa kuvuna, ila pia kuna wakati kunatokea ukame, hakuna mvua, hakuna mazao hakuna kuvuna na kinachofuatia ni baa la njaa!. Pia kuna wakati kunanyesha mvua kubwa zaidi kupitiliza, hadi kuleta maafa ya mafuriko, kama elnino, lakini mavuno ya maeneo ya mabondeni baada ya elnino ni mavuno makubwa ajabu, kutokana na kurutubishwa kwa siltation ya elnino!.

Kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu, ndio kipindi cha neema kwa media na waandishi!, huu ndio wakati wetu wa mavuno, kama ni mvua hizi sasa mvua za elnino!.

Zamani enzi za chama kimoja, kwa media kuripoti uchaguzi mkuu, ilikuwa bure!, media ndio zilikuwa zinawagharimia waandishi wake kuripoti uchaguzi. Vyama vingi vilipoanza, bure ikaendelea ila ili chama kipate preferential coverage rupia ilianza kupenyezwa kidogo kidogo kwa siri and unofficial.

Kuanzia uchaguzi wa 2005, media campaign zilianza kuwa official na waandishi kulipwa sasa ilikuwa rasmi, mfano gazeti la Mtanzania lilitake side na kumsaidia mgombea mmoja tuu fulani ndani ya CCM na lilifanya kazi kubwa kuwaangamiza wagombea wengine wowote tishio, hata ikibidi kuwatungia story za uongo hadi kutengeneza picha za photoshop!, kazi hii nzuri ya media campain ilizaa matunda mema, baadhi ya wale viongozi wa kampeni hizi kuzawadiwa kuanzia ukurugenzi, hadi ukuu wa wilaya!.

Uchaguzi wa 2010, sasa ikawa sio CCM pekee bali hadi Chadema nayo ikalipa waandishi kuzunguka na mgombea wao kwenye chopa!.

Uchaguzi wa mwaka huu, neema sasa ni kubwa zaidi, CCM yenye pesa nyingi zaidi ndio itaongoza kwa kuwalipa waandishi wengi na kununua media nyingi!. CCM itanunua airtime na kununua waandishi officially from the media houses kuzunguka na wagombea wake wa urais. Ukawa nao this time watalipa media kwa media kuzunguka na mgombea wake!.

Vyama vipya kwa ACT vinavyotambua the power of media, nao, watawalipa waandishi kuzunguka na mgombea wake!.

Baadhi ya wagombea individually wenye ukwasi mkubwa wa fedha kama kina Nimrod Mkono, Mohamed Dewji, Edward Lowassa etc, nao wataunda mitandao yao ya media officially or unofficially kuwaripotia na kote huku ni fedha tuu ndio itazungumza!.

Hongereni sana wana media, hiki ni kipindi chenu cha mavuno, tukae mkao wa kula!, huwezi jua, hata mimi labda hali ya kale ka usafiri kangu ka boda boda kalikopata ajali, huenda kanaweza kufufuka au hata kubadili kutoka boda boda hadi bajaj!.

Swali la msingi la kujiuliza ni Jee, bahasha hizi wanazolipwa media na wana siasa au vyama vya siasa ni halali?, Jee ni sahihi kwa vyama na wagombea wenye pesa, kutumia pesa zao, kununua media na kuwalipa waandishi?!.

Hili suala la waandishi wa habari na bahasha, nimeishalizungumza sana hapa
Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa.

Pasco
Huu ni msimu mwingine wa mavuno kwa waandishi wa habari, mara baada ya kipenga cha kuanza kampeni kupulizwa, neema ya fedha za kampeni zinaishukia sekta yetu ya media.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki Media
P
 
Huu ni msimu mwingine wa mavuno kwa waandishi wa habari, mara baada ya kipenga cha kuanza kampeni kupulizwa, neema ya fedha za kampeni zinaishukia sekta yetu ya media.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki Media
P
Mkuu sisi ni nchi ya kijamaa, na kwa mema ambayo chama kimetufanyia hauoni huu ni wakati muafaka wa vyombo vya habari kuwa wazalendo na kuungana na chama kinachotetea wanyonge na kuwapa airtime bure ili ujumbe mwema umfikie kila mwananchi?
 
Mkuu sisi ni nchi ya kijamaa, na kwa mema ambayo chama kimetufanyia hauoni huu ni wakati muafaka wa vyombo vya habari kuwa wazalendo na kuungana na chama kinachotetea wanyonge na kuwapa airtime bure ili ujumbe mwema umfikie kila mwananchi?

Kama chama kimekutendea mema, una haja gani kuwaelezea wananchi!!
 
Wanabodi,

Kwanza naomba nikiri kuwa nimeandika uzi huu kwa kuwa inspired na mwana jf huyu,

Mkuu, Steven Robert Masatu, kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, na mafanikio kwenye kilimo yanategemea msimu, kuna msimu wa mvua, ni kipindi cha kulima, kupanda na kupalilia, kuna msimu wa kiangazi ni wakati wa kuvuna, ila pia kuna wakati kunatokea ukame, hakuna mvua, hakuna mazao hakuna kuvuna na kinachofuatia ni baa la njaa!. Pia kuna wakati kunanyesha mvua kubwa zaidi kupitiliza, hadi kuleta maafa ya mafuriko, kama elnino, lakini mavuno ya maeneo ya mabondeni baada ya elnino ni mavuno makubwa ajabu, kutokana na kurutubishwa kwa siltation ya elnino!.

Kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu, ndio kipindi cha neema kwa media na waandishi!, huu ndio wakati wetu wa mavuno, kama ni mvua hizi sasa mvua za elnino!.

Zamani enzi za chama kimoja, kwa media kuripoti uchaguzi mkuu, ilikuwa bure!, media ndio zilikuwa zinawagharimia waandishi wake kuripoti uchaguzi. Vyama vingi vilipoanza, bure ikaendelea ila ili chama kipate preferential coverage rupia ilianza kupenyezwa kidogo kidogo kwa siri and unofficial.

Kuanzia uchaguzi wa 2005, media campaign zilianza kuwa official na waandishi kulipwa sasa ilikuwa rasmi, mfano gazeti la Mtanzania lilitake side na kumsaidia mgombea mmoja tuu fulani ndani ya CCM na lilifanya kazi kubwa kuwaangamiza wagombea wengine wowote tishio, hata ikibidi kuwatungia story za uongo hadi kutengeneza picha za photoshop!, kazi hii nzuri ya media campain ilizaa matunda mema, baadhi ya wale viongozi wa kampeni hizi kuzawadiwa kuanzia ukurugenzi, hadi ukuu wa wilaya!.

Uchaguzi wa 2010, sasa ikawa sio CCM pekee bali hadi Chadema nayo ikalipa waandishi kuzunguka na mgombea wao kwenye chopa!.

Uchaguzi wa mwaka huu, neema sasa ni kubwa zaidi, CCM yenye pesa nyingi zaidi ndio itaongoza kwa kuwalipa waandishi wengi na kununua media nyingi!. CCM itanunua airtime na kununua waandishi officially from the media houses kuzunguka na wagombea wake wa urais. Ukawa nao this time watalipa media kwa media kuzunguka na mgombea wake!.

Vyama vipya kwa ACT vinavyotambua the power of media, nao, watawalipa waandishi kuzunguka na mgombea wake!.

Baadhi ya wagombea individually wenye ukwasi mkubwa wa fedha kama kina Nimrod Mkono, Mohamed Dewji, Edward Lowassa etc, nao wataunda mitandao yao ya media officially or unofficially kuwaripotia na kote huku ni fedha tuu ndio itazungumza!.

Hongereni sana wana media, hiki ni kipindi chenu cha mavuno, tukae mkao wa kula!, huwezi jua, hata mimi labda hali ya kale ka usafiri kangu ka boda boda kalikopata ajali, huenda kanaweza kufufuka au hata kubadili kutoka boda boda hadi bajaj!.

Swali la msingi la kujiuliza ni Jee, bahasha hizi wanazolipwa media na wana siasa au vyama vya siasa ni halali?, Jee ni sahihi kwa vyama na wagombea wenye pesa, kutumia pesa zao, kununua media na kuwalipa waandishi?!.

Hili suala la waandishi wa habari na bahasha, nimeishalizungumza sana hapa
Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa.

Pasco
MEI 3 ya kila mwaka ni Siku ya Kimataifa ya Uhuru wa vyombo vya habari, Mimi Pascal Mayalla, kwa niaba yangu kama mwanahabari ambaye ni mwandishi wa habari huru na wa kujitegemea kwa kujitolea na kwa niaba ya kampuni yangu ya PPR as chombo huru cha habari, niwatakie wanahabari wenzangu wote, maadhimisho mema ya siku hii, huku nikidurusu, niliwahi kusema nini kuhusu uhuru wa habari kwa media zetu za Tanzania yetu.

Nawatakia maadhimisho mema ya siku yetu hii ya leo na uhuru wa habari mwema.
Paskali.
 
Inaonesha vile media zetu sio za kuaminika, zinamtazama mwenye mfuko uliojaa ndio zinampamba hata kama mchafu.
 
Back
Top Bottom