Elections 2010 Uchaguzi Mkuu na sera ya jumuiya ya Afrika Mashariki

PatPending

JF-Expert Member
Aug 17, 2007
491
102
Wadau kama mnavyofahamu leo hii ndio itifaki ya soko la pamoja la Afrika Mashariki inaanza kufanya kazi. Kuna maengi ambayo yamejadiliwa na kuandikwa humu humu kuhusiana na hili swala na haya yako katika jukwaa husika (za Kimataifa n.k).

Swali langu kuu ni moja, kutokana na maoni ya wengi humu ndani na hata huko mitaani, inaashiria ya kwamba waTanzania walio wengi hawajapendezwa aidha na uharakishwaji wa huu "ushirikiano" au vipengele vya itifaki hii na sera nzima kwa ujumla, au vyote viwili. Sasa je inakuwaje mpaka leo hii hakuna chama chochote cha siasa kitakacho kulizungumzia suala hili nyeti sana katika mustakabali wa taifa hili? Hili ni suala ambalo laweza kuwa moja la mikakati mikuu katika kampeni za uchaguzi wa wabunge na rais mwaka huu na miaka ijayo (kama zitakuwepo).

Katika nchi nyingi ambazo zimejikuta katika njia panda kama hii wananchi na wanasiasa husika wamekuwa mstari wa mbele katika kutetea maslahi ya taifa lao. Tumejionea katika nchi mbalimbali kama Uingereza (misimamo ya vyama vya UKIP na Conservative kuhusiana na Umoja wa Ulaya unaeleweka) na wengineo, wananchi wakiwa mstari wa mbele katika kutetea maslahi yao.

Sasa iweje leo hii hapa Tanzania watu mnakaa kimya ilihali kuna manung'uniko mengi tu ya chini chini ya nchi kuuzwa au kuburuzwa kuhusiana na hili suala la "ushirikiano" na mataifa mengine ya Afrika Mashariki?

Jamani amkeni sasa, mkishindwa kujitetea sasa msije mkalaumu au kutupa ngumi baadae !!!
 
Ahsante mdau kwa kuja na hii topic! mimi nikiwa mmojawapo mwenye dukuduku moyoni! kwanza hili swala cjui wamelikubali vp hawa viongozi wetu! wameamua wenyewe na c wananchi cc kama kawaida yetu tuu kupelekwa na viongozi huko wanakotaka kwenda na cc twende! wengine wanalichukulia tofauti kwamba eti wakenya wamesoma mara wanajua kufanya kazi kuliko cc huo ni upambavu na utumbo kwa wanaongea namna hyo! kujua kingereza au lugha yeyite cyo kuwa na elimu! tunafanya kazi kuliko wakenya.. kitu ninachoofia ni kwamba hawa ndugu zetu tutashindwana nao kitu hiki,hawana tabia ya ushirikiano hata kwa wao kwa wao leo unamwambia shirikiana na mtanzania,ruanda,burundi, watanzania tunaweza shirikiana mpaka hata na wasomali,ila sisi watanzania pia hatutaki kuoneshwa madharau wal ubaguzi wa aina yeyote.JE? haya yakitokea kwetu hapo baadae ni nini kitafuata? MKENYA anakuja kwa style yake,MGANDA anakuja kwa style yake, Kila mmoja anaenda kwa style yake hatuko wote lengo moja kubali msikubali huyu anamuona huyu hv yule hv!
Any wayz ni mtazamo wangu tu wandugu tusitafutane na pia mambo yanaweza yakawa mazuri na ya kuvutia EE MUNGU BARIKI! EMEN!
 
Asante mdau kwa maoni yako. Kusema kweli jambo la kuunganisha watu au nchi ni muhimu na la maendeleo. Ndio maana wahenga walisema "UMOJA NI NGUVU..." Hata hivyo kuunganisha watu ni lazima kutanguluiwe na uzingativu wa mambbo kadhaa ya msingi. Kubwa ni KUJUA FIKA UTAMAUNI wa wahusika. Ni lazima pia wanaounganishwa wawe naa taarifa muhimu kuhusu watu wa upande mwingine. Mfano mdogo, kama mtoto akipeleka taarifa kwa wazazi kuwa anaoa/anaolewa na mtu fulani wazazi watataka kujua taarifa fulani fulani kuhusu huyo mchumba k.m ni kabila gani na je hilo kabila lina utamaduni gani ukilinaganisha na utamaduni wao.Mara nyingine wazai wanaweza kuonyesha wasiwasi.
Tuaweza kufananisha muungano wa Afrika mashariki na hali hii. Watu kuwa na wasiwasi ni lazima. Watanzania walipaswa kueleweshwa kuwa watu tunaofunga nao ndoa wakoje, tunafanana au kutofautiana kwa yepi na nimambo yapi Watanzania wajiandae nayo katka ndoa hii. Je hao wanaokuja wataleta nini tofauti na hivi tulivyonavyo. Ndio, soko la pamoja! sawa, liwe la ajira au la bidhaa, sisi tuaingia na bidhaa ipi! na Ni ajira zipi tutapata huko. watu wana mashaka kwa vile wameanza kuona tayari watu wameanza shule hapa wanawaajiri watu wa nchi jirani eti wanajua zaidi kiingereza! foolish! Kwani ukiiajiri matanzania atachukua muda gani ku- master na kutumia hicho kiingereza kufundihishia? Kwa hiyo basi hata mahoteli, nyuma za wageni, vyombo vya habari na kadhalika vitaajiri hao wageni kwa sababu finyu ya lugha? Mambo kama haya ndiyo yanawapa wasiwasi watanzania na mengine kama ardhi n.k. NI MUHIMU KATIKA MCHAKATO WA UCHAGUZI WA 2010 WATANZANIA WAKAELIMISHWA FURSA MUHIMU NA NAMMNA WANAVYOWEZA KUFAIDIKA NA SOKO LA PAMOJA LA AFRIKA MASHARIKI NA JE WAFANYE NINI SASA? SERIKALI IKO TAYARI KUWAWEZESHA WATU WAKE KWA HILI?
 
Back
Top Bottom