babumapunda
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 4,644
- 3,288
Uchaguzi katika majimbo haya unafanyika leo kuchagua Wabunge kufuatia kufariki kwa Wagombea wa nafasi ya Ubunge wa CCM Ludewa na NLD Masasi.
Masasi alifariki Dkt. Emmanuel Makaidi na kwa Ludewa alifariki Deo Haule Filikunjombe
Twende pamoja
========================
Update
CCM - 16597
CUF - 14069
CDM - 512 ACT - 347
NLD - 70
CCM YATETEA JIMBO LAKE LA MASASI KWA KURA 2528
=========================
UPDATE
Wakati CUF ilionekana kuongoza katika vituo vya awali kwenye uchaguzi wa ubunge Jimbo la Masasi, CCM imeonekana kuamba katika hatua hiyo katika uchaguzi mwingine kama huo Jimbo la Ludewa.
Matokeo ya awali Masasi
Kituo cha Machinjio namba 1 katika Kata ya Mkuti, CUF ilikuwa mbele kwa kura 187 dhidi ya 98 za CCM huku Chadema ikiwa na kura nne, ACT na NLD kura mojamoja. Kituo namba 2, CUF ilikuwa na kura 188, CCM 90, Chadema tatu na NLD moja. Kituo namba 3, CUF pia iliongoza kwa kura 184, CCM 102, Chadema moja. Kituo namba 4, CUF ilipata kura 178, CCM 91, NLD 21 na ACT 0.
Kituo cha Maji namba 1 katika Kata ya Napupa, CCM ilipata kura 37 na kuachwa mbali na CUF iliyopata kura 122. Kituo namba 2, ilipata kura CCM 73 huku CUF ikizoa kura 114. Katika Kituo cha Msufini namba 1, CCM iliibuka kidedea kwa kura 108, dhidi ya 77 za CUF. Kituo namba 3 CCM 78, CUF 101.
Matokeo katika Kata ya Nyasa, Kituo cha Hoteli Halmashauri namba 1, CCM 98, CUF 105, Kituo namba 2, CCM 94 na CUF 107.
Kituo cha Shule ya Masasi Sekondari Kata ya Migongo, CCM 84, CUF 118, ACT 2, Chadema 4 na NLD 0. Kituo cha Meff namba 1 Kata ya Jida, CCM 140, CUF 154, ACT 3, Chadema 0 na NLD 0. Kituo cha Jamhuri namba 1 Kata ya Jida CCM 85, ACT 2, CUF 145 na NLD 0.
Kituo cha Zahanati namba 1 Kata ya Jida CCM 105, CUF 107. Kituo cha Zahanati namba 2 CCM 105, CUF 107
Matokeo ya awali Ludewa
Wakati CUF ikitamba Masasi, Ludewa hali ilionekana kuwa ngumu kwa upinzani kwani matokeo katika Kituo cha Kijiji cha Ludewa Mjini A, CCM iliongoza kwa kura 152 huku Chadema ikifuatia kwa kura 57. Kituo cha Ludewa Mjini B, CCM ilipata kura 164, Chadema 43. Kituo cha Shule ya Msingi Kimbila A, CCM iliendelea kuiburuza Chadema kwa kupata kura 144 na Chadema 55. Shule ya Msingi Kimbila B, CCM 147 na Chadema 52.
Kituo cha Kilimahewa CCM 123, Chadema 23. Kituo cha Ligumbiro CCM 108, Chadema 17.
Wafuasi mbaroni
Awali, watu saba wanaodaiwa kuwa wafuasi wa CCM wanashikiliwa na polisi Njombe kwa tuhuma za kuwashambulia wafuasi watatu wa Chadema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Wilbroad Mtafungwa alisema tukio hilo lilitokea juzi jioni saa moja usiku katika Kijiji cha Lugarawa, Ludewa.
Alisema tukio hilo lilitokea baada ya wafuasi wa Chadema kuwahoji wenzao wa CCM waliokuwa ndani ya gari, kuwa wanafanya nini katika eneo hilo usiku ndipo waliposhuka na kuanza kuwashambuli. Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (Bavicha), Patrick Ole Sosopi alisema: "Tuliona hilo tukio ni kutaka kutuhamisha kwenye uchaguzi."
Katibu wa CCM Wilaya ya Ludewa, Lusiana Mbosa alisema hilo lilisababishwa na mgombea ubunge wa Chadema, Bathoromeo Msambichaka kufika Lugarawa kwa kile alichodai kuwa ni kutaka kuhujumu uchaguzi.
Akijibu madai hayo Msambichaka alisema: "Kama anasema mimi nilikuwa nataka kuhujumu uchaguzi, ungemuuliza muda huo wa saa mbili usiku jana (juzi) kulikuwa na uchaguzi gani unafanyika?"
Chanzo:Mwananchi
Masasi alifariki Dkt. Emmanuel Makaidi na kwa Ludewa alifariki Deo Haule Filikunjombe
Twende pamoja
========================
Update
CCM - 16597
CUF - 14069
CDM - 512 ACT - 347
NLD - 70
CCM YATETEA JIMBO LAKE LA MASASI KWA KURA 2528
=========================
UPDATE
Wakati CUF ilionekana kuongoza katika vituo vya awali kwenye uchaguzi wa ubunge Jimbo la Masasi, CCM imeonekana kuamba katika hatua hiyo katika uchaguzi mwingine kama huo Jimbo la Ludewa.
Matokeo ya awali Masasi
Kituo cha Machinjio namba 1 katika Kata ya Mkuti, CUF ilikuwa mbele kwa kura 187 dhidi ya 98 za CCM huku Chadema ikiwa na kura nne, ACT na NLD kura mojamoja. Kituo namba 2, CUF ilikuwa na kura 188, CCM 90, Chadema tatu na NLD moja. Kituo namba 3, CUF pia iliongoza kwa kura 184, CCM 102, Chadema moja. Kituo namba 4, CUF ilipata kura 178, CCM 91, NLD 21 na ACT 0.
Kituo cha Maji namba 1 katika Kata ya Napupa, CCM ilipata kura 37 na kuachwa mbali na CUF iliyopata kura 122. Kituo namba 2, ilipata kura CCM 73 huku CUF ikizoa kura 114. Katika Kituo cha Msufini namba 1, CCM iliibuka kidedea kwa kura 108, dhidi ya 77 za CUF. Kituo namba 3 CCM 78, CUF 101.
Matokeo katika Kata ya Nyasa, Kituo cha Hoteli Halmashauri namba 1, CCM 98, CUF 105, Kituo namba 2, CCM 94 na CUF 107.
Kituo cha Shule ya Masasi Sekondari Kata ya Migongo, CCM 84, CUF 118, ACT 2, Chadema 4 na NLD 0. Kituo cha Meff namba 1 Kata ya Jida, CCM 140, CUF 154, ACT 3, Chadema 0 na NLD 0. Kituo cha Jamhuri namba 1 Kata ya Jida CCM 85, ACT 2, CUF 145 na NLD 0.
Kituo cha Zahanati namba 1 Kata ya Jida CCM 105, CUF 107. Kituo cha Zahanati namba 2 CCM 105, CUF 107
Matokeo ya awali Ludewa
Wakati CUF ikitamba Masasi, Ludewa hali ilionekana kuwa ngumu kwa upinzani kwani matokeo katika Kituo cha Kijiji cha Ludewa Mjini A, CCM iliongoza kwa kura 152 huku Chadema ikifuatia kwa kura 57. Kituo cha Ludewa Mjini B, CCM ilipata kura 164, Chadema 43. Kituo cha Shule ya Msingi Kimbila A, CCM iliendelea kuiburuza Chadema kwa kupata kura 144 na Chadema 55. Shule ya Msingi Kimbila B, CCM 147 na Chadema 52.
Kituo cha Kilimahewa CCM 123, Chadema 23. Kituo cha Ligumbiro CCM 108, Chadema 17.
Wafuasi mbaroni
Awali, watu saba wanaodaiwa kuwa wafuasi wa CCM wanashikiliwa na polisi Njombe kwa tuhuma za kuwashambulia wafuasi watatu wa Chadema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Wilbroad Mtafungwa alisema tukio hilo lilitokea juzi jioni saa moja usiku katika Kijiji cha Lugarawa, Ludewa.
Alisema tukio hilo lilitokea baada ya wafuasi wa Chadema kuwahoji wenzao wa CCM waliokuwa ndani ya gari, kuwa wanafanya nini katika eneo hilo usiku ndipo waliposhuka na kuanza kuwashambuli. Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (Bavicha), Patrick Ole Sosopi alisema: "Tuliona hilo tukio ni kutaka kutuhamisha kwenye uchaguzi."
Katibu wa CCM Wilaya ya Ludewa, Lusiana Mbosa alisema hilo lilisababishwa na mgombea ubunge wa Chadema, Bathoromeo Msambichaka kufika Lugarawa kwa kile alichodai kuwa ni kutaka kuhujumu uchaguzi.
Akijibu madai hayo Msambichaka alisema: "Kama anasema mimi nilikuwa nataka kuhujumu uchaguzi, ungemuuliza muda huo wa saa mbili usiku jana (juzi) kulikuwa na uchaguzi gani unafanyika?"
Chanzo:Mwananchi