kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,501
- 12,910
Kila kitu kinachosemwa na kufanywa na wanasiasa katika kipindi hiki Cha uchaguzi faida na hasara itakwenda kwa wananchi wa kawaida, hivyo wanasiasa tuchunge ndimi zenu na vitendo vyenu kwenye majukwaa.
Kwa vyovyote vile sisi wananchi tunapenda kusikia wagombea wakisema namna watakavyotupatia haya kama tukiwachagua:
1. Usalama na amani
2. Maji ya kunywa na umwagiliaji.
3. Afya kwa wote
4. Elimu kwa wote
5. Chakula kwa wote
6. Umeme kwa wote
7. Uchumi wa majumbani sio wa takwimu
8. Miundombinu ya Usafiri na usafirishaji
9. Utawala wa sheria
10. Utengamano na nchi jirani na kimataifa.
11. Uboreshaji wa Michezo na Sanaa.
12. Utunzaji wa mazingira na ukuzaji wa utalii
Wananchi tungependa kuwasikia mnasema Nini kuhusu mtakavyotupatia vitu hivyo kwa njia bora zitakazozingatia utu wetu, uhai wetu, mila zetu, utamaduni wetu, Uhuru wetu, muungano wetu, na demokrasia yetu bila kuwasahau nchi majirani.
Hatuhitaji kusikia Sera za kutaja na kulaumu watu, vyama, na taasisi mbalimbali.
Mwanasiasa atakaefanya siasa za maji taka bila shaka atashindwa uchaguzi kabla ya uchaguzi haujafanyika
Kwa vyovyote vile sisi wananchi tunapenda kusikia wagombea wakisema namna watakavyotupatia haya kama tukiwachagua:
1. Usalama na amani
2. Maji ya kunywa na umwagiliaji.
3. Afya kwa wote
4. Elimu kwa wote
5. Chakula kwa wote
6. Umeme kwa wote
7. Uchumi wa majumbani sio wa takwimu
8. Miundombinu ya Usafiri na usafirishaji
9. Utawala wa sheria
10. Utengamano na nchi jirani na kimataifa.
11. Uboreshaji wa Michezo na Sanaa.
12. Utunzaji wa mazingira na ukuzaji wa utalii
Wananchi tungependa kuwasikia mnasema Nini kuhusu mtakavyotupatia vitu hivyo kwa njia bora zitakazozingatia utu wetu, uhai wetu, mila zetu, utamaduni wetu, Uhuru wetu, muungano wetu, na demokrasia yetu bila kuwasahau nchi majirani.
Hatuhitaji kusikia Sera za kutaja na kulaumu watu, vyama, na taasisi mbalimbali.
Mwanasiasa atakaefanya siasa za maji taka bila shaka atashindwa uchaguzi kabla ya uchaguzi haujafanyika