Mchambuzi nashukuru sana kwa uchambuzi wako mzuri na unajitahidi sana kutokuwa na upande. Hata hivyo, kuna kitu hujakiona ambacho ni muhimu sana. Kwanza nakubaliana na wewe kuhusu aina 3 za wapiga kura. Hata hivyo, natofautiana na wewe kuhusu uwezekana wa pregmatic na common sence kuisaidia ccm 2015. Sijashawishika, kimantiki (am very objective hapa) kwamba kwenye ngazi ya urais chadema itategemea rational votes peke yake. Kwa nini nasema hivyo?
Mosi, pregmatic votes inaangalia masuala ya dini ya mgombea, kabila, ukanda, jinsia, uswahiba, urafiki nk. Ni mambo ambayo siyo ya msingi na yasiyofaa kabisa. Sasa basi, kama hivyo ndivyo, kura za pregmatics zitategemea mgombea aliyesimamishwa na ccm na anaingia ktk kundi gani la pregmatic vile vile Mgombea wa Chadema ni yupi anaingia ktk kundi gani la pregmatic. Kwa hiyo, pregmatic inaweza kuisaidia chadema au ccm ila tu inategemea mgombea aliyesimamishwa na vyama hivyo.
Tatu, kuna waziri moja wa ccm alisema shule za kata ndizo zitakazoiua ccm, nakubaliana naye 100%. Common sence group iko vijijini na hawa siyo vijana ni wazee. Kwa hiyo, kundi ni kweli ndio msaada wa ccm, hata hivyo kundi linakumbwa na changamoto kadhaa.
Mosi, kwa kuwa ni wazee, hili ni kundi linalopungua na vijana wanaongezeka.
Pili, vijana wa shule za kata wanawabadilisha kimtazamo wazee hawa wachache waliobaki.
Rational votes kama ulivyosema mwenyewe ni kura za chadema kutokana hali ya kisiasa ilivyo, kwa hiyo, nashawishika kuamini kwamba, kama uchaguzi wa 2015 utakuwa huru,Chadema itashinda kwa kishindo.