VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
CCM imedhamiria. Imepania kwelikweli. Kuifanya Dar es Salaam kuwa UPINZANI FREE ZONE.Kama ilivyo Dodoma. Mikakati imesukwa na imesukika. Majimbo ya Ubungo na Kawe sasa yako chini ya CHADEMA. CCM imeapa kuyarejesha majimbo hayo kwa njia ya sanduku la kura hapo Oktoba mwaka huu. Bwana John John Mnyika na Bibi Halima Mdee wakae chonjo. Majimbo yote ya Ilala,Kinondoni,Kawe,Ubungo, Segerea,Ukonga,Temeke na Kigamboni yanapaswa kuwa ya CCM.
Wametafutwa na kupatikana wagombea wa kuyanyakua majimbo yote ya Dar es Salaam. Tunazo taarifa kuwa wapinzani wetu nao wamejidhatiti kunyakua majimbo kadhaa humu Dar es Salaam. Lakini,tutaibuka kidedea kama chama tawala na chama komavu. Tukutane Oktoba tutakapotaka kuyakomboa majimbo ya Ubungo na Kawe na kuyatetea mengineyo.
Oktoba, mtoto hatumwi dukani!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Wametafutwa na kupatikana wagombea wa kuyanyakua majimbo yote ya Dar es Salaam. Tunazo taarifa kuwa wapinzani wetu nao wamejidhatiti kunyakua majimbo kadhaa humu Dar es Salaam. Lakini,tutaibuka kidedea kama chama tawala na chama komavu. Tukutane Oktoba tutakapotaka kuyakomboa majimbo ya Ubungo na Kawe na kuyatetea mengineyo.
Oktoba, mtoto hatumwi dukani!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam