Environmental Security
Senior Member
- May 21, 2020
- 181
- 261
Habari wanajamvi
Katika kithibitisha mwitikio wa dhati kwa maono na uongozi wa chama cha mapinduzi CCM chini ya uongozi wa m/kiti Dk. John Magufuli wa kutoa fursa kwa vijana kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama na serikali, tayari hilo limedhihirika kwa vijana hasa wanawake kujitokeza ili kugombea nafasi za kuwawakilisha wananchi kwa kupitia nafasi za ubunge wa viti maalum,
Mathalan katika mkoa wa Dodoma tayari mchuano unaonekana kuwa mkali kati ya wagombea vijana, ambapo hadi sasa tathmini inaonesha mwanamama kijana jasiri na mchapakazi anayefahamika kwa jina la STELLA JASTON MKISI anaonekana kukubalika sana miongoni mwa akinamama wa CCM Dodoma, na hii ni kutokana na jinsi anavyotumia rasilimali zake katika kuihudumia jamii lakini hasa kinachowavutia wengi ndani ya CCM ni aina ya siasa anazofanya, ambapo amejikita katika kufanya siasa za kistaarabu zisizohusisha rushwa, matusi wala kuwagawa wanachama.
Pia, wanawake wengi wanavutiwa naye kutokana na kuchoka uongozi na siasa za mazoea na za kuwagawa wanawake ndani ya chama zinazofanywa na wagombea wakongwe hasa wabunge wa viti maalum waliopita ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakiamini katika kutegemea kutoa fedha ili kushawishi wachaguliwe, na kushawishi wanawake wa CCM mkoa wa dodoma wasiwasikilize wagombea wengine.
Naona siasa safi ndani ya CCM ikianza kushika kasi na vijana wakiongoza katika kulithibitisha hilo kitu kinachofanya watu wenye siasa za kistaarabu kama STELLA JASTON MKISI kuwafanya wakongwe wakose usingizi wakihaha huku na kule na wapambe wao.
Viva vijana wa CCM; Viva STELLA JASTON MKISI
CCM imara
Katika kithibitisha mwitikio wa dhati kwa maono na uongozi wa chama cha mapinduzi CCM chini ya uongozi wa m/kiti Dk. John Magufuli wa kutoa fursa kwa vijana kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama na serikali, tayari hilo limedhihirika kwa vijana hasa wanawake kujitokeza ili kugombea nafasi za kuwawakilisha wananchi kwa kupitia nafasi za ubunge wa viti maalum,
Mathalan katika mkoa wa Dodoma tayari mchuano unaonekana kuwa mkali kati ya wagombea vijana, ambapo hadi sasa tathmini inaonesha mwanamama kijana jasiri na mchapakazi anayefahamika kwa jina la STELLA JASTON MKISI anaonekana kukubalika sana miongoni mwa akinamama wa CCM Dodoma, na hii ni kutokana na jinsi anavyotumia rasilimali zake katika kuihudumia jamii lakini hasa kinachowavutia wengi ndani ya CCM ni aina ya siasa anazofanya, ambapo amejikita katika kufanya siasa za kistaarabu zisizohusisha rushwa, matusi wala kuwagawa wanachama.
Pia, wanawake wengi wanavutiwa naye kutokana na kuchoka uongozi na siasa za mazoea na za kuwagawa wanawake ndani ya chama zinazofanywa na wagombea wakongwe hasa wabunge wa viti maalum waliopita ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakiamini katika kutegemea kutoa fedha ili kushawishi wachaguliwe, na kushawishi wanawake wa CCM mkoa wa dodoma wasiwasikilize wagombea wengine.
Naona siasa safi ndani ya CCM ikianza kushika kasi na vijana wakiongoza katika kulithibitisha hilo kitu kinachofanya watu wenye siasa za kistaarabu kama STELLA JASTON MKISI kuwafanya wakongwe wakose usingizi wakihaha huku na kule na wapambe wao.
Viva vijana wa CCM; Viva STELLA JASTON MKISI
CCM imara