Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,847
- 2,669
Nape katangaza kuwania ubunge kupitia jimbo la ubungo. Kati ya wagombea watano wa ccm waliotangaza nia ni wazi kuwa nape atapenyeza na hatimaye kukutana na kijana mwenzie, mnyika kwenye mchuano wa kuwania jimbo la ubungo. Ni wazi kuwa vijana wote wawili wanakubalika. Kwa nini huyu nape asingechagua jimbo jingine kama ilala (ambapo kuna washindani wawili tu ikilinganishwa na majimbo mengine?), segerea, ukonga ama temeke? Kwa nini wanyang'anyane hii nafasi ilhali wote wanahitajika bungeni? Haoni busara za mzee sabodo? Kilichotakiwa ni kuwa mdee akamate kawe, mnyika ubungo na nape kati ya hayo yaliyotajwa juu. Binafsi kwa wakati huu nisingependa kumpoteza mnyika wala nape. Vinginevyo vijana wenzangu msitake tutake kuamini maneno ya cheyo kuwa mjipange kiuchumi na kijamii kwanza ndipo mfikirie ubunge wakati umri umesonga kiasi. Ningependa sana kuwaona wote wawili bungeni Dodoma