Salum Sanane
Member
- Apr 14, 2013
- 30
- 4
Nimekuwa najiuliza bila kupata majibu yaliyo sahihi,ndiyo maana leo naileta hoja yangu hii ili nisaidiwe.
Suala la ubinafsishaji nimekuwa nalilinganisha na unyanyasaji mkubwa kwa watanzania hasa wa hali ya chini. Si vibaya nikisema kuwa ni juhudi za makusudi zilizoandaliwa kwa lengo la kumjengea maisha yasiyo na matumaini.
Mashirika mengi ya umma kabla hayajabinafsishwa yalikuwa yametoa ajira ya kutosha,na mara baada ya kubinafsishwa yalikufa au kupoteza muelekeo na hivyo kuwalazimu watumishi kuhangaika kutafuta mbinu mbadala za kuwawezesha kujikimu. Hali hii ni tatizo kubwa kwa mtanzania wa kawaida.
Mbali na mashirika ya umma, wavumbuzi wa migodi ya madini ni wananchi wenyewe. Kutokana na hali yao mbaya ya maisha wanajitahidi kutafuta ufumbuzi na hatimae kubahatisha kuangukia maeneo yanayopatikana madini. Badala ya kuwaboreshea ili nao wanufaike na ajira yao,serikali ikibaini tu kuwa madini yanapatikana inabinafsisha na kuwaacha wakiendelea kutaabika.
Maswali yangu ni haya:
1. Serikali inamjali mwananchi wake?
2. Mwananchi afanye kazi gani itakayoishawishi serikali kuuthamini utu wake?
3. Kuna sababu yoyote ya msingi ya kuendeleza dhulma hii?
Naomba ndugu zangu wenye uelewa mkubwa mnisaidie majibu ya maswali haya. Lakini pia hoja yangu ni hii: HAKUNA MSINGI WOWOTE WA SERIKALI KUDHIBITI NJIA ZOTE ZA MAPATO NA KUMWACHA MWANANCHI AKITAABIKA.
Suala la ubinafsishaji nimekuwa nalilinganisha na unyanyasaji mkubwa kwa watanzania hasa wa hali ya chini. Si vibaya nikisema kuwa ni juhudi za makusudi zilizoandaliwa kwa lengo la kumjengea maisha yasiyo na matumaini.
Mashirika mengi ya umma kabla hayajabinafsishwa yalikuwa yametoa ajira ya kutosha,na mara baada ya kubinafsishwa yalikufa au kupoteza muelekeo na hivyo kuwalazimu watumishi kuhangaika kutafuta mbinu mbadala za kuwawezesha kujikimu. Hali hii ni tatizo kubwa kwa mtanzania wa kawaida.
Mbali na mashirika ya umma, wavumbuzi wa migodi ya madini ni wananchi wenyewe. Kutokana na hali yao mbaya ya maisha wanajitahidi kutafuta ufumbuzi na hatimae kubahatisha kuangukia maeneo yanayopatikana madini. Badala ya kuwaboreshea ili nao wanufaike na ajira yao,serikali ikibaini tu kuwa madini yanapatikana inabinafsisha na kuwaacha wakiendelea kutaabika.
Maswali yangu ni haya:
1. Serikali inamjali mwananchi wake?
2. Mwananchi afanye kazi gani itakayoishawishi serikali kuuthamini utu wake?
3. Kuna sababu yoyote ya msingi ya kuendeleza dhulma hii?
Naomba ndugu zangu wenye uelewa mkubwa mnisaidie majibu ya maswali haya. Lakini pia hoja yangu ni hii: HAKUNA MSINGI WOWOTE WA SERIKALI KUDHIBITI NJIA ZOTE ZA MAPATO NA KUMWACHA MWANANCHI AKITAABIKA.