PostGE2025 Ubalozi wa Denmark watoa pole kwa waliopoteza wapendwa wao wakati wa uchaguzi mkuu 2025

PostGE2025 Ubalozi wa Denmark watoa pole kwa waliopoteza wapendwa wao wakati wa uchaguzi mkuu 2025

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania umetuma salamu za pole kwa familia na jamii kwa ujumla ambazo zimepoteza wapendwa wao kutokana na matukio yaliyotokea wakati wa uchaguzi.

Kupitia taarifa iliyotolewa leo, ubalozi huo umeeleza kuwa unaenzi maisha ya wote waliotangulia mbele ya haki, pamoja na wale wanaoendelea kuuguza majeraha ya kimwili na kiakili katika kipindi hiki kigumu.

Aidha, ubalozi umetoa wito wa kuendelea kujenga maridhiano na umoja wa kitaifa kupitia uelewano na uwajibikaji wa pamoja, ili kuimarisha misingi ya haki na amani kwa Watanzania wote.

Kwa heshima ya waliopoteza maisha, ubalozi wa Denmark umesimama kwa dakika moja leo kuwaomboleza.
1762773739224.png


1762773819987.png
 
Hii issue watu wanaichukulia poa, mauaji ya tanzania yameshangaza jumuhia ya kimataifa, Msoga anajulikana sana kwa kusababisha huo upuuzi kwa kumshauri chief Hangaya vibaya. Hizi ndo zinazovuma kwenye viunga vya jumuiya za kimataifa.
 
Tunapata pole kutoka ubalozi wa Denmark wakati serikali yetu ipo kimya.
 
Wafanyakazi wa ubalozi wamerudi kazini leo

Kwa heshima ya waliopoteza maisha, leo tulisimama kwa dakika moja ya kuwakumbuka na kuwaomboleza.

Tunatoa pole kwa familia na jamii kwa ujumla ambao wamepoteza wapendwa wao kutokana na matukio yaliyojitokeza wakati wa uchaguzi.

Tunaenzi maisha ya wote waliotangulia mbele za haki, pamoja na wale ambao wanaendelea kuuguza majeraha ya kimwili na kiakili katika kipindi hiki kigumu.

Tunatoa wito wa kuendelea kujenga maridhiano na umoja wa kitaifa, kupitia uelewano na uwajibikaji wa pamoja, ili kujenga misingi ya haki na amani kwa watanzania wote.

_________________

Embassy staff are back in the office today.

As a mark of respect, the Embassy observed a minute of silence in remembrance of all those who lost their lives.

We extend our deepest condolences to the families and communities affected by the recent events during the elections.

We share in the sorrow of all Tanzanians who have lost loved ones during this difficult time.

In this moment of grief, we echo the call for healing and national reconciliation, built on mutual understanding and a collective commitment to true peace and justice.
denmarkintanzania-20251111-0001.webp
 
Aisee ni hatari dunia nzima inajua kuwa raia waliuawa na ccm halafu mafisiemu yenyewe yanajaribu kuficha moto kwenye nguo
 
Aisee ni hatari dunia nzima inajua kuwa raia waliuawa na ccm halafu mafisiemu yenyewe yanajaribu kuficha moto kwenye nguo
Yako bize kugawana vyeo hayana muda,wenzetu wanasimama dakika 1 kuombea waliofariki Serikali ya asilimia 98 hata kutoa pole wameshindwa
 
Alafu anasimama mtu anasema waliokufa ni maigizo
 
Back
Top Bottom