Uanzishaji wa Mikoa mipya ni gharama kubwa kwa Serikali.

Ng'wanza Madaso

JF-Expert Member
Oct 21, 2008
2,268
333
Ndugu wa jamvi habarini za Masiku na Poleni kwa shughuli za maandalizi ya uchaguzi,
Nimekuwa nje kwa matibabu kwa muda sasa nimerudi.Asanteni kwa mlionitumia salaam.

Binafsi naona kuanzishwa kwa mikoa hii ambayo haina hadhi ya kuwa mikoa kama Geita na Njombe,ni gharama kubwa kwa taifa hasa wakati huu ambapo dunia inapita kwenye wakati mgumu wa kuanguka kwa uchumi ambapo na hapa nyumbani hali bado ni tete kiuchumi.

Kuanzisha mkoa mpya ni gharama kubwa,na pesa hutoka Serikali kuu ambako nako kiuchumi hali ni tete.Ofisi za wakuu wa mikoa,gharama za kumlipa mkuu na watumishi wake,wakuu wa wilaya na watumishi wake,ugawanywaji wa vijiji ili kupata wilaya ndani ya mikoa hiyo mipya,wakuu wa polisi Mkoa(RPC) na ma (OCD) wilaya na viongozi wengineo.

Hiyo mikoa mipya haijafanikia kupata maendeleo yoyote ikiwa wilaya na je ikibadilishwa na kuwa mikoa kutakuwa na Mabadiliko yoyote?.Kwa nini tusisubili hizi wilaya zipate maendeleo kama wilaya kwanza na ndipo ibadilishwe na kuwa Mikoa?
Tujadili .
 
Back
Top Bottom