Uangalizi wangu [my observation] kuhusu urais wa Rais Magufuli

Rais Magufuli keshamaliza miaka miwili kamili tokea ashike madaraka mwaka 2015.

Katika miaka hiyo miwili amekuwa akipingwa sana, akikosolewa vikali, na kudhihakiwa kwa kila namna hususan humu JamiiForums.

Kama ulimwengu ungekuwa ni huu huu wa JF basi mtu ungeweza kudhani kuwa wanaomuunga mkono Rais Magufuli ni idadi ndogo sana ya watu.

Lakini ukweli wa mambo, kwa mtazamo wangu, ni tofauti kabisa na taswira ijengwayo humu JF dhidi yake.

Huku uraiani Rais Magufuli anakubalika sana, hususan na watu wa kawaida wenye maisha ya chini na kati.

Ndiyo, wanaompinga wapo. Hawawezi kabisa kukosekana. Ila mtu ukiitumia JF kuwa ndo kipimo cha kukubalika au kutokukubalika kwake, hakika itakula kwako.

Kwa mfano, naamini kabisa ikiwekwa kura ya maoni humu JF kuhusu ‘approval’ au ‘disapproval’ ya urais wa Magufuli, atashindwa vibaya sana. Walio wengi wata ‘disapprove’.

Jambo hilo linanizidishia imani yangu kuwa kuna ‘disconnect’ kubwa tu kati ya uhalisia wa JF na uhalisia wa uraiani na mashinani.

Kwa mtaji huo, mimi naamini kabisa kuwa 2020 Rais Magufuli atashinda ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu. Itakuwa kinyume na ilivyokuwa kwa Kikwete....alishinda kwa kishindo kwenye awamu yake ya kwanza na kwenye awamu ya pili akapata ushindi mdogo sana kulinganisha na ule wa awali.
Mimi naamini kwamba JF ni jukwaa lenye manufaa mengi sana. kuna mengi yanafanyika humu ambayo tunaweza tusiyaone. hata katika kumbi za Siasa, kuna elimu inatolewa, mijadala ni mikali na kuna wanaopinga na wanaounga mkono. hiyo hali ya wengi kupinga ilikuwa zamani. naona siku hizi pengine kuna mikakati ya kuweka maprofesheno wa kujibu hoja za watu wanaoipinga serikali. lakini kuna pia wale ambao misimamo yao ni independent. wanampenda tu JPM kwa sababu anashughulikia hoja za msingi ambazo zimewakera miaka nenda miaka rudi. Ila kusema kwamba JF haina connection na uhalisia, siyo relevant sana. wanaokwenda JF ni watu wa aina fulani, lakini ina a sample, inatoa representation ya watu hao. kundi la wale wakulima nao wana JF zao. hivyo unapochambua inabidi uzingatie hilo

Lakini pia there is a catch. JPM anazo ajenda zake anazozipitisha humo humo pamoja na mambo mengine. na hili linajadiliwa hata mitaani, japo kwa tahadhari kubwa. kuna wengi wanaumia kwa sera zake kiuchumi, kuna wanaoumia kwa kubomolewa. ni kweli JPM ni mjanja sana kwa kucheza na hisia za watanzania, kiasi kwamba wale wa kawaida walio wengi watamuona ni mtu mzuri sana. kitendo cha kuwaumiza matajiri kinampa sifa sana kwa walala hoi, ambao wanaasume kwamba ule utajiri utatiririka kwao. kwamba akitumbuliwa fulani, zile hela alizokuwa anafuja na kufisidi, zitawashukia wananchi. tatizo linakuja pale hao wanaosubiri mvua ya fedha ije, isipokuja ndio yale ya kikwete ya leo kupata 85% na baada ya miaka mitano kuambulia 61% au chini zaidi ya hapo.

kama unayosema ni kweli, basi tungeona kwenye zile chaguzi za marudio, ambao wapinzani walisusia. kama kungekuwa na kale kafreedom angalau ka enzi za Kikwete tu, basi tungepata picha halisi ya maoni ya watanzania vs uchambuzi wako. lakini kwa kuwa kulikuwa na matumizi makubwa ya vyombo vya dola, hiyo pia inaonesha kwamba JPM naye hana uhakika kama anapendwa mtaani, na hayuko tayari kujiweka kwenye mizani. ukiangalia anayofanya kama kufunga bunge live, kuzuia wapinzani wasifanye siasa wakati CCM wanafanya siasa, ni namna kuonesha kwamba wanatambua jinsi CCM ilivyokuwa unpopular na wanataka wapinzani warudi nyuma ili wao wasonge mbele, angalau kwa idadi ya watu, hata kama ni kwa kuwanunua.
 
Shida kubwa ni elimu..... Huwezi linganisha wapiga kura wa kenya na wapiga kura watanzania ndio maana unakuta mikoa kama dodoma na tabora imechoka haswaaaa ila wanaipigia kura CCM kwa miaka 20 sasa ya vyama vingi hivyo unaweza kuwa umeongea ukweli ila kwa mikoa yenye wasomi na miji mikubwa huwezi kuta wakamuunga mkono maana wanadadisi vitu vingi sana kabla hawajavikubali

Kikubwa upinzani uhakikishe voter turnout mijini inakuwa kubwa na huko vijijini wapeleke elimu ya uraia otherwise hao ILLITERATES watamrudisha huyu magu ikulu 2020
 
It is the same disconnect that befell liberals of America when Trump got elected. Even today, they are still struggling to understand why they lost and still they can't figure it out. The disconnect that exist in Tanzania I'll argue is more emotional than substantial. Ni kama Wamarekani wasiomkubali Trump kwa sababu hawampendi tu; hata kama wananufaika na sera zake!
Lakini trump alizidiwa popular vote kwa hiyo hoja yako haina mashiko na kma sio wamarekani kutumia proportional representation system trump angeisikia ikulu kwenye redio

Wapinzani wakiweza kuleta voter turnout kubwa kwenye miji yenye 1m+ voters ambako wana reason kimjini mjini na mara nyingi population huwa kubwa yanaweza tokea msiyotegemea..... Wanaotuangusha ni ile mikoa kma dodoma wakipewa tu kaambulance kamoja wanamwaga kura mkoa mzima kana kwamba hawalipi kodi

Uchaguzi halisi ni pale wananchi wakiwa na elimu kama vipi rais achaguliwe na bunge hivyo mwenye majimbo mengi ndio anatoa rais ila hizi kura za uraiani kwa aina ya ujinga baadhi ya mikoa ilionao sioni tukipata viongozi sahihi maana watu wanaahidiwa mambo yale yale miaka 20 sasa ila bado hayatekelezwi na wanachagua chama kilekile so funny
 
Lakini trump alizidiwa popular vote kwa hiyo hoja yako haina mashiko na kma sio wamarekani kutumia proportional representation system trump angeisikia ikulu

Trump alizidiwa popular votes kutokana na majimbo ya California, New York, na Illinois ambayo ndo yana miji mikubwa mikubwa zaidi kwa Marekani.

Lakini alishinda idadi kubwa zaidi ya majimbo. Alishinda majimbo 30 kati ya 50. Hillary akaambulia majimbo 20 tu.

Maana yake ni kwamba Trump alishinda popular votes za hayo majimbo 30.

Kwa hiyo kilichopaisha national popular votes za Hillary ni miji ya New York, Los Angeles, na Chicago tu. Miji ambayo ni ngome za liberals.

Zaidi ya hapo aligaragazwa kwingine kote. Mtu kaambulia majimbo 20 kati ya 50.....come on now.
 
Rais Magufuli keshamaliza miaka miwili kamili tokea ashike madaraka mwaka 2015.

Katika miaka hiyo miwili amekuwa akipingwa sana, akikosolewa vikali, na kudhihakiwa kwa kila namna hususan humu JamiiForums.

Kama ulimwengu ungekuwa ni huu huu wa JF basi mtu ungeweza kudhani kuwa wanaomuunga mkono Rais Magufuli ni idadi ndogo sana ya watu.

Lakini ukweli wa mambo, kwa mtazamo wangu, ni tofauti kabisa na taswira ijengwayo humu JF dhidi yake.

Huku uraiani Rais Magufuli anakubalika sana, hususan na watu wa kawaida wenye maisha ya chini na kati.

Ndiyo, wanaompinga wapo. Hawawezi kabisa kukosekana. Ila mtu ukiitumia JF kuwa ndo kipimo cha kukubalika au kutokukubalika kwake, hakika itakula kwako.

Kwa mfano, naamini kabisa ikiwekwa kura ya maoni humu JF kuhusu ‘approval’ au ‘disapproval’ ya urais wa Magufuli, atashindwa vibaya sana. Walio wengi wata ‘disapprove’.

Jambo hilo linanizidishia imani yangu kuwa kuna ‘disconnect’ kubwa tu kati ya uhalisia wa JF na uhalisia wa uraiani na mashinani.

Kwa mtaji huo, mimi naamini kabisa kuwa 2020 Rais Magufuli atashinda ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu. Itakuwa kinyume na ilivyokuwa kwa Kikwete....alishinda kwa kishindo kwenye awamu yake ya kwanza na kwenye awamu ya pili akapata ushindi mdogo sana kulinganisha na ule wa awali.
Jamii forum 85%ni walimu.
Ndio ambao wana muda mwingi wa kuitumia technology ya mtandao. Sasa hiyo haitoshelezi kukupa uhakika wa maoni kuhusu jambo fulani sababu ni 0.0000000%ya population ya watanzania.
 
Sijui umetumia utafiti gani kusema hvyo..
ila tambua kuwa lack of informations kwa wananchi wengi ndio inapelekea kuona anafanya vizur hii ikijumlisha na publicty anazozi air kwenye tv kila sku basi wananchi wakiona wanajua kweli.. Ila laiti wangeujua ukwel wasingekuwa hvo..
 
Mimi naona mambo ni tofauti. Magufuli anakubalika kuliko anavyopewa credit humu.
Sampuli yako ni watu wangapi?kutoka rika gani, elimu zao na maeneo wanakoishi .ili tujue kama kweli umefanya observation bila kuegemea upande mmoja
 
Rais Magufuli keshamaliza miaka miwili kamili tokea ashike madaraka mwaka 2015.

Katika miaka hiyo miwili amekuwa akipingwa sana, akikosolewa vikali, na kudhihakiwa kwa kila namna hususan humu JamiiForums.

Kama ulimwengu ungekuwa ni huu huu wa JF basi mtu ungeweza kudhani kuwa wanaomuunga mkono Rais Magufuli ni idadi ndogo sana ya watu.

Lakini ukweli wa mambo, kwa mtazamo wangu, ni tofauti kabisa na taswira ijengwayo humu JF dhidi yake.

Huku uraiani Rais Magufuli anakubalika sana, hususan na watu wa kawaida wenye maisha ya chini na kati.

Ndiyo, wanaompinga wapo. Hawawezi kabisa kukosekana. Ila mtu ukiitumia JF kuwa ndo kipimo cha kukubalika au kutokukubalika kwake, hakika itakula kwako.

Kwa mfano, naamini kabisa ikiwekwa kura ya maoni humu JF kuhusu ‘approval’ au ‘disapproval’ ya urais wa Magufuli, atashindwa vibaya sana. Walio wengi wata ‘disapprove’.

Jambo hilo linanizidishia imani yangu kuwa kuna ‘disconnect’ kubwa tu kati ya uhalisia wa JF na uhalisia wa uraiani na mashinani.

Kwa mtaji huo, mimi naamini kabisa kuwa 2020 Rais Magufuli atashinda ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu. Itakuwa kinyume na ilivyokuwa kwa Kikwete....alishinda kwa kishindo kwenye awamu yake ya kwanza na kwenye awamu ya pili akapata ushindi mdogo sana kulinganisha na ule wa awali.
Rais Magufuli yashamshinda?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom