DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Your browser is not able to display this video.
================
Mahakama Kuu imeahirisha kesi hiyo hadi Septemba 15, 2025 kwaajili ya kutoa uamuzi wa Tundu Lissu kuachiwa huru ama vinginevyo.
==========
Jopo la Majaji watatu wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam ambao ni Jaji Dunstan Nduguru, Jaji James Karayemana na Jaji Ferdinand ambao wanasikiliza kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Antipas Lissu linatarajia kutoa uamuzi Jumatatu ijayo juu ya mapingamizi ya kesi hiyo yaliyotolewa na mashtakiwa aliyekuwa na hoja tano na kuwepa mapingamizi kesi isiendelee kwa hatua ya usilikilizwaji wa mashahidi katika kesi hiyo ya uhani ambayo haina dhamana.
Katika kesi hiyo Lissu anakabiliwa na shtaka moja la uhaini kinyume na kifungu cha 39(2) (d) cha sheria ya kanuni ya adhabu linalotokana na maneno aliyotamka kuhusiana na kuzuia kufanyika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Chanzo: ITV