GE2025 Uamuzi wa mapingamizi kesi ya Tundu Lissu kutolewa Septemba 15, 2025

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Your browser is not able to display this video.

================
Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Wakili Rugemeleza Nshala hii leo Septemba 11, 2025 akiongea na Wanahabari nje ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam amesema Tundu Lissu ameiomba Mahakama kumuachia huru kwa madai kwamba yale yote yaliyofanyika katika Mahakama ya Hakimu Mkaazi Kisutu yalikuwa batili,

Mahakama Kuu imeahirisha kesi hiyo hadi Septemba 15, 2025 kwaajili ya kutoa uamuzi wa Tundu Lissu kuachiwa huru ama vinginevyo.

==========

Jopo la Majaji watatu wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam ambao ni Jaji Dunstan Nduguru, Jaji James Karayemana na Jaji Ferdinand ambao wanasikiliza kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Antipas Lissu linatarajia kutoa uamuzi Jumatatu ijayo juu ya mapingamizi ya kesi hiyo yaliyotolewa na mashtakiwa aliyekuwa na hoja tano na kuwepa mapingamizi kesi isiendelee kwa hatua ya usilikilizwaji wa mashahidi katika kesi hiyo ya uhani ambayo haina dhamana.

Katika kesi hiyo Lissu anakabiliwa na shtaka moja la uhaini kinyume na kifungu cha 39(2) (d) cha sheria ya kanuni ya adhabu linalotokana na maneno aliyotamka kuhusiana na kuzuia kufanyika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Chanzo: ITV
 

Kutegemea haki kwenye hiyo kesi, heri kusubiria dodo kwenye mnazi.
 
Jopo la Majaji watatu wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam ambao ni Jaji Dunstan Nduguru, Jaji James Karayemana na Jaji Ferdinand ambao wanasikiliza kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Antipas Lissu linatarajia kutoa uamuzi Jumatatu ijayo juu ya mapingamizi ya kesi hiyo yaliyotolewa na mashtakiwa.

Lissu aliweka mapingamizi kwamba Mahakama Kuu aina nguvu ya kisheria kusikiliza shauri hilo, adai kuwa mamlaka hayo yanakoseka na kutokana na mchakato wa committal court kuwa dosari kwa kutofuata sheria

Katika kesi hiyo Lissu anakabiliwa na shtaka la uhaini kinyume na kifungu cha 39(2) (d) cha sheria ya kanuni ya adhabu linalotokana na maneno aliyotamka kuhusiana na kuzuia kufanyika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Sasa jopo hilo la Majaji limepanga kutoa uamuzi Jumatatu tarehe 15, 2025.
 
Wana mtandao wanataka kutuharibia TZ yetu nzuri mungu waondoshe hao
 
Mahakama Kuu imeahirisha kesi hiyo hadi Septemba 15, 2025 kwaajili ya kutoa uamuzi wa Tundu Lissu kuachiwa huru ama vinginevyo.
 
Mahakama Kuu imeahirisha kesi hiyo hadi Septemba 15, 2025 kwaajili ya kutoa uamuzi wa Tundu Lissu kuachiwa huru ama vinginevyo.
 
Jumatatu mbali sana lazima watapewa maelekezo tu.
Usifanye mchezo na mtu aliye na hofu kubwa sana nawe.
Samia na Genge lake wanayo hofu kubwa sana na Mh. Tundu Lissu; tena wakati 'critical' kwelikweli kama huu kabla ya kumaliza mipango yao iliyo sababisha wamweke ndani!
Kwa hiyo, huko kwa "watoa maelekezo" usipape uzito wowote kwa sasa.

Tumaini tu pekee ni hii dalili nzuri/mpya inayoanza kujitokeza (hata kama ni kwa matamshi tu kwa sasa) kutokana na uongozi mpya huko kwenye mahakama.
Wakiamua kusimama kidete, bila kutishwa, inawezekana sana HAKI ikaanza kuonekana huko.
Na huo utakuwa ni mwanzo mzuri sana kuirekebisha nchi yetu hii.
 
There’s an iota of hope! Jopo la majaji kidogo liko insulated. Linaweza kuwa na balls za kutenda haki dhidi ya Serikali.
And the new boss at the top appears to have given the signal towards that direction (kutenda HAKI). That's more than an iota! .
 
Nilikuwa nafuatilia Toka Jumatatu..

Hii issue imekaa vibaya kwa upande wa Jamuhuri..
Na kwa bahati mbaya...wamewekwa majaji watatu...

Ninachoona ni kesi kufutwa...shida itakuwa nje...Lissu watamkamata tena
 
Mambo mengine ni ujinga tu. Hakuna uhaini wa kufanywa na mtu mmoja tu! Narudia tena kusema hakuna!
According to Katunga na Kaswaga inawezekana kwa mtu mmoja kupindua serikali.
Hata mwanafunzi wa chuo cha sheria hapa Lushoto nadhani angefanya vizuri kuliko Kaswaga na Katunga.
 
Bado muda wa kutenda haki wanao. Jumatatu wamwachie huru Lissu kabla mambo hayajaharibika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…