Uaminifu ni muhimu kama unataka kuwa web developer

chilubi

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
8,182
6,216
Habari wadau,

Nimekuja hapa kupost my experience with a fraud web developer na kama kuwapa caution wengine.

Kuna watu wanajifanya ma web developer lakini ukimpa kazi anaanza mizungusho. Kuna huyu anaitwa mathew kapela au humu JF anajiita matthew12345. Ukweli sikutaka kufikia hatua mpaka nikayaanika hapa, huwa napenda kuwa patience lakini sasa patience yangu imfika kikomo. Huyu jamaa nilimpa kazi ya kuntengezea website yangu cocovoyage.com, website ya mambo ya tours kwa ajili ya Zanzibar. Mwanzoni alinifanyia kazi yangu, japokuwa alikuwa akisua sua kutokana na kutoweza kumodify to my needs. Ilifikia stage aliweza kidogo, nikaona ah haina haja ya kupush more kwa sababu tayari niliona ni shida kwake. Kwa sababu biashara hii niko na mwenzangu, yule mwenzangu hakupendezeshwa na muonekane wa ile site, nikawasiliana na Matthew Kapela, tukabadili theme ambayo mwenzangu aliikubali, akaanza kuifanyia kazi lakini ilimshinda, akanambia kuwa atabadilisha theme. Nikamkubalia ombi lake hilo. akachukua mda bila kufanya chochote kwenye ile theme hata hakuiondoa, mpaka nakumbuka siku ya alhamisi au ijumaa kama ntakuwa sikosei nikawasiliana nae na kunambia kuwa ataifanyia kazi weekend hio. sikutaka kumsumbua hadi siku ya jumanne ivi nampigia simu ikawa haipokelewi, nikajua yuko bize, basi nikawa nampigia sana lakini bila mafanikio. Nikawa namtext lakini sipati majibu. huku kwenye site yangu kashaiondoa theme, then ameniekea ile page ya kuonesha bado siku ngap website itakuwa online. akaweka 6 days. mi nikamchukulia kuwa ndio muda wake alojiekea kuimaliza, nikawa nampigia kutaja kujua progress lakini hapokei. mpaka dakika hii hapokei simu yangu, nikilogin kweny wordpress site yangu, hakuna page nyengine zaidi ya hello world, hii ni wiki ya pili tangu anambie ataifanyia kazi wikiendi, nikiingia sasa ivi nakuta tena bado 6 days eti imalize.

Kutokana na kitendo chake hichi cha kutopokea simu wala kujibu sms wala kurespond kwa njia yoyote ile, huyu jamaa ni tapeli tu. Hana cha udeveloper wala nini, sijui kama alikuwa anatafuta pesa za kumaliza shida zake ama vipi.

Ushahidi wa mawasiliano yetu kupitia email upo kama huyu jamaa nimmpa project yangu. Isitoshe kuna project nyengine nimempa ambayo ingkamilika naamini basi ingefikia mbali na kutambulikana. Kuna site inaitwa pesaportal.com ambayo pia nilimpa, nayo imekwama na picha ya obama na mwanae.

Kwa wateja wengine,
huyu jamaa si wa kumpa kazi naeka picha za mawasiliano


matthew12345

 

Attachments

  • Screen Shot 2017-03-13 at 19.45.31.png
    Screen Shot 2017-03-13 at 19.45.31.png
    50.3 KB · Views: 37

Similar Discussions

Back
Top Bottom