Uaminifu ndio kinga kuu

Galacha Maestro

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2011
Posts
1,353
Reaction score
2,231
UAMINIFU NDIO KINGA KUU

Simu zimevunja ndoa nyingi za watu. Na mtu akikaa kando ndio anajishangaa. Na kujiuliza ni simu tu au? Kwani simu ni kitu kidogo ambacho ukikidharau hautadumu kwenye ndoa yako au mahusiano yako. Kwa muda mrefu na kumbuka simu sio mlinzi wako ulinzi ni matendo yako kwa mumeo wako au kwa mke wako.

Tuwe waaminifu kwa wale tuwapendao.
 
Nafikiri una jichanganya. Siyo simu ambazo zinavunja ndoa au mahusiano, bali ni kukosekana kwa uaminifu ambo hujulikana kupitia simu. Na tatizo pia sio uaminifu bali ni mtazamo juu ya uaminifu. Wewe unachukuliaje swala la uaminifu ndo jambo la muhimu.

Ukijua tabia za binadamu/wanyama haya mambo hayakupi shida. Nafikiri tatizo ni ubinafsi na siyo uaminifu. Binadamu tumekuwa na ubinafsi mkubwa katika swala la mapenzi. Eti unataka mkeo awe wako peke yako na mmeo awe wako peke yako. Basi Mchonge huyo wako peke yako halafu umjaze pumzi muoane. Lakini ukitegemea huyu binadamu aliye zaliwa na mwanamke kuwa wako peke yako ni kujiumiza kichwa.

Ana feeling zake, ana matamanio yake, kukubali kuoana na wewe hakumuondolei matamanio yake mengine. Muache aji enjoy, ni wako akiwa kwako.
 
Ongezea simu hazivunji ndoa tu na hadi zinatoa uhai pia...Refer taarifa kutoka SAUT mwanza chuo chenye matukioa mengi toka enzi za Nsia Swai..
 
90% ya ndoa zinazovunjika chanzo ni kukosa uaminifu kitendo cha mume au mke kutoka kuchepuka ni sawa na kuanza kuiweka rehani ndoa yako
wakati simu ndio huwa chanzo kikubwa cha kuzua migogoro ktk ndoa
laiti watu wangejua kuwa unapotoka nje ya ndoa kuna mambo ya ajabu unaingiza mwilini basi watu wangetulia tu ktk ndoa zao
 
Kama hakuna upendo na heshima kwenye ndoa ni tatizo.
 
wapo waaminifu ila ukikosa uaminifu ktk ndoa ukatoka nje basi hiyo sio ndoa ni kifungo ambacho kitakutesa mpk utamani kuiacha ndoa
ila maneno yako mengne duh ya ajabu ! ila ni mtazamo wako japo finyu lkn kila mtu ana maamuzi yake na selikari ya kichwa chake tafuta mke OA araf uone uchungu wa kuchapiwa kama ujaja kuediti comment yako
mana hata maana ya neno NDOA hujui na kbla hujaingia ktk ndoa tafuta define ya ndoa then ndo uingie ama sivyo itakuwa kifungo kwako ambapo utajuta kwann umeoa au kuolewa
 



Kwa hiyo mke wako (kama umeoa) ulioa ukijua kabisa umeolea na watu wengine? Kwamba sio wako peke yako, na kwamba hata ukijua anasaliti utachukulia poa,kwa sababu wewe sio mbinafsi..au mimi ndio sijaelewa.

Kama ndivyo hongera..karne hii watu wenye 'Ujamaa' huo nadhani ni wewe tu. Inatakiwa tutafute barabara tuipe jina lako..
 
umeongea vizuri mama endelea kuwashauri wenzio macho juu juu mke wa mtu anahongwa chipsi chali NA YOTE NI KUTOKUTAMINI NDOA NI CHANZO KIKUBWA SANA simu ni kifaaa ni tokeo la baada WASIO JUA UCHUNGU WA NDOA WATAKUJA KUOMBA USHAURI HUMU
 
umeongea vizuri mama endelea kuwashauri wenzio macho juu juu mke wa mtu anahongwa chipsi chali NA YOTE NI KUTOKUTAMINI NDOA NI CHANZO KIKUBWA SANA simu ni kifaaa ni tokeo la baada WASIO JUA UCHUNGU WA NDOA WATAKUJA KUOMBA USHAURI HUMU
Mama tena??? Asante kwa mawazo yako. But i am male.
 
Asante kwa mawazo yako
 
Maoni yako mazuri sana.
 
Mama tena??? Asante kwa mawazo yako. But i am male.

sorry kumbe mwana uume mwenzangu pamoja mkuu KAMA UPO KWENYE NDOA ISHI VIZURI NA MKEO NENO LINATUASA HIVO utamchunguza bila wewe pia kutulia ni bure TUWAAMINI NAO WATATUSIKILIZA ingawa dunia hii ya sasa changamoto ni nyingi sana hasa ndoa changa
 
Simu ni kifaa tu cha kurahisisha mawasiliano. Hakina utashi, hivyo wengi wamekuwa wakisingizia simu mpaka kufikia hatua ya kuwekeana mipaka hasa kwa wapenzi.
Sikubaliani hata kidogo kuwa simu ni chanzo cha mifarakano. Chanzo cha mifarakano ni sisi wenyewe binadamu wenye utashi. Sisi ndio tunaamua huu mchepuko niusave vipi, niutext hivi, wife/husband nimwambie nini n.k. Hiki kifaa ukitumia ktk mema hakina shida ktk mabaya pia.
Hivyo aina ya mawasiliano ya mtu ndio dhamira yake
 
ungejua dhumuni hasa la wadhamini wa watengenezaji simu yaani hii dunia yamejificha mengi sana
nakuombea endelea kuishi kwa maisha marefu zaidi japo simu imerahisisha mambo mengi sana ukiacha hta kimawasiriano na kifedha lkn pia imekuwa darasa linalotembea wengi tumefahamu vingi kupitia simu
lkn ipo siku utakuja juta kwann simu ya mkononi iligunduliwa
OGOPA SANA
 
Dhamira ya mtu ni dhamira ya mtu. Sina cha kuogopa mkuu.
 
Bila shaka wewe ni mwanamke uliyeachwa sababu ikiwa simu.

Unajaribu kuikataa hali halisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…