U-Turn barabarani: Wakuu hii ni sahihi?!

U-Turn barabarani: Wakuu hii ni sahihi?!

Akili Unazo!

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2009
Posts
3,930
Reaction score
4,937
Wakuu hebu nisaadieni kwa hichi kisa kilichompata rafiki yangu alipokwenda ubalozi wa marekani.




Leo 15/07/09 kati ya saa 9:30AM-11AM asubuhi niliegesha gari langu nje ya ubalozi wa marekani ambako nilikwenda kwa ajili ya Visa. Baada kutoka huko nikawasha gari langu na nikapiga U-turn kurudi mjini.


Baada ya hatua chache tu, nikasimamishwa na askari mmoja wa JWTZ ambaye alikuwa analinda Ubalozi huo. Huyo askari akaniuliza kwanini nimepiga U-turn pale karibu na ubalozi? mie nikamwambia kwasababu ninakwenda mjini. Yeye kaniambia ni kosa kupiga U-turn pale. Mie sikutaka kubishana sana hivyo tukapelekana hadi kituo cha karibu cha polisi cha Oysterbay.


Huko nilikutana na polisi mwenye Kwanja 3, yeye nikamuelezea hayo na nikamwambia kule hakuna kibao cha kusema ni marufuku kupiga U-turn? Huyo askari kaniuliza ati wewe uliona kibao kilichokuruhusu kupiga U-turn pale? Nilishangazwa sana na swali la mkuu huyo na sikuwa na jibu lolote, Hivyo nikakubali kosa langu na niliandikiwa notification namba 1/82810 ambayo nililipa faini ya Shs 20,000 na kupewa risiti namba 35331902.
Swala ninalojiuliza mpaka sasa, Je hilo Kosa na faini niliyolipa lilikuwa la haki?

Maana ya kuandika barua hii ni kuwatahadharisha wengine ili wawe makini wanapoenda Ubalozini.
Ahsante,
 
Hatuchelewi kukuta kibao cha u-turn kimetundikwa pale kesho ili kuhalalisha malipo uliyofanya!!
 
Mkuu pole sana;
Kila mtu anatafuta mahali pa kulia,pale oysterbay amefikaje, ulimbeba au?.Ungemwambia tukutane oysterbay atafute usafiri wake mkutane kule, au uishie zako.Mimi siku hizi niko mjanja walinisumbua akinisimamisha si shuki, na ninamwambia tukutane huko kituoni, make najua, hata huyo hakuwa na gari.Ni njaa tu asubuhi hakuwacha pesa ya mboga.Mimi nakushauri ukipata nafasi shughulikia zaidi peleka hiyo listi mpe mkubwa wao akishindwa sasa hivi bunge linaendelea mpe zitto au slaa.
 
Mkuu pole sana;
Kila mtu anatafuta mahali pa kulia,pale oysterbay amefikaje, ulimbeba au?.Ungemwambia tukutane oysterbay atafute usafiri wake mkutane kule, au uishie zako.Mimi siku hizi niko mjanja walinisumbua akinisimamisha si shuki, na ninamwambia tukutane huko kituoni, make najua, hata huyo hakuwa na gari.Ni njaa tu asubuhi hakuwacha pesa ya mboga.Mimi nakushauri ukipata nafasi shughulikia zaidi peleka hiyo listi mpe mkubwa wao akishindwa sasa hivi bunge linaendelea mpe zitto au slaa.
Usikubali suala hilo lifikishe kwa Kamanda Kombe,si unaona Zitto amesababisha Bunge likubali neno WAZIRI AMETOA MAJIBU YA OVYO OVYO, hivyo fuatilia ijulikane ukweli maana Askari wetu sasa wanaingilia kazi zisizo zao.
 
Back
Top Bottom