Twafaa: Bei ya mboga kuu ya Taifa yapaa juu mara dufu

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
6,067
10,936
Habari waJF kwenu mlio na raha,

Hali ya maisha inaendelea kuwa ngumu kila uchwao. Gharama za maisha zinazidi kupanda na uchumi bado uko pale pale.

Vyakula vinagusa familia zote, mmoja mmoja au kundi la wengi. Bei za vyakula kila siku zinazidi kupanda. Ukame nao unazidi kutamalaki. Siku hizi kusema Tanzania kuna njaa ni kosa la jinai, labda useme kuna upungufu kidogo wa chakula.

Baada ya bei ya mchele,unga na sukari kupanda sasa ni zamu ya mboga kuu ya Taifa tuliyoachiwa na Hayati Mwalimu Nyerere, mboga hiyo ni Maharage.

Maharage imekuwa mboga yetu ya kila siku, iwe mashuleni, gerezani, kambi za wakimbizi.Katika hali ya kushangaza bei imepaa kutoka Tsh. 2300 hadi 3000 (ongezeko la Tsh. 700). Bei ya Jumla ilikuwa Tsh. 2100 na sasa ni ths 2800.

Hii ni bei ya eneo ninalokaa Sinza la watu wa kawaida.

Huko kwenu sijui bei imekaaje?
 
Sasa sijui itakuwaje maana mbiga mbadala zote zimepanda.

Huku dagaa zilisha panda bei kitambo tu.
 
sio kosa la serikali,serikali iko busy na mambo mengine ya msingi kama kununua ndege,kama hauli ufe tu
 
Aisii , ilikuwa kg 1 ya maharage sawa na US dollar 1, sasa thamani ya kg 1 inazidi dollar 1, lkn si kwa sana kivile
 
Habari waJF kwenu mlio na raha,

Hali ya maisha inaendelea kuwa ngumu kila uchwao. Gharama za maisha zinazidi kupanda na uchumi bado uko pale pale.

Vyakula vinagusa familia zote, mmoja mmoja au kundi la wengi. Bei za vyakula kila siku zinazidi kupanda. Ukame nao unazidi kutamalaki. Siku hizi kusema Tanzania kuna njaa ni kosa la jinai, labda useme kuna upungufu kidogo wa chakula.

Baada ya bei ya mchele,unga na sukari kupanda sasa ni zamu ya mboga kuu ya Taifa tuliyoachiwa na Hayati Mwalimu Nyerere, mboga hiyo ni Maharage.

Maharage imekuwa mboga yetu ya kila siku, iwe mashuleni, gerezani, kambi za wakimbizi.Katika hali ya kushangaza bei imepaa kutoka Tsh. 2300 hadi 3000 (ongezeko la Tsh. 700). Bei ya Jumla ilikuwa Tsh. 2100 na sasa ni ths 2800.

Hii ni bei ya eneo ninalokaa Sinza la watu wa kawaida.

Huko kwenu sijui bei imekaaje?
Kaulizie na njegere mdau inafukuziana na nyama
 
Hali inazidi kuwa tete .... dah.. sasa watu wataish kama mashetan.. sio matajir tu.. hata wa hali ya chini
 
Kaulizie na njegere mdau inafukuziana na nyama
Mwaka jana Disemba nikiwa likizo Bukoba niliulizia bei ya njegere ambazo zishamenywa, aisee kilo ilikuwa sh. 8000 , sikutaka kuuliza tena nikatoka ndukiii. Huku Dar bei zilishanishinda, kwangu sasa hivi njegere ni anasa.
 
Back
Top Bottom