TV Program Alert: Msidanganywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,718
Wanabodi,

Hii ni TV Program Alert, ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi, inashiriki katika maonyesho ya kilimo ya Nane Nane katika uwanja wa Mwl. J.K Nyerere mjini Morogoro.

Ushiriki huo wa Tume ya Uchaguzi kwenye Maonyesho, ni fursa nzuri kwa wale wote wenye madukuduku kuhusu Tume kama ni tume huru, na uchaguzi, kama ulikuwa huru na wa haki.

Kwa vile sii wote wataweza kutembelea banda hilo huko Morogoro, kwa faida ya wengi, nimetembelea banda hilo, na nitarusha vipindi maalum vya banda hilo ndani ya Nane Nane na PPR.

Leo Waziri Mkuu ametembelea banda la Tume, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, Makamisha Mary Longway na Athina Omari, pamoja na msimamizi mbobezi, Spora Liana, watazungumzia uchaguzi uliopita.

Usikose kuangalia mfululizo wa vipindi vya Tume ya Uchaguzi kwenye Maonyesho ya Nane Nane, kipindi cha kwanza kinaanza leo saa 1:00-1:30 Star TV.

Kesho ni Channel Ten, keshokutwa ITV kisha TBC.

Karibuni msikie na kushuhudia jinsi ambavyo huwezi kudanganya matokeo ya uchaguzi wa rais, hivyo msidanganywe na viongozi wa vyama vya siasa kuhusu bao la mkono kwenye matokeo ya urais!, hakuna kitu kama hicho!.

Paskali

UPDATE.
Kwa ambao hawakukiona kipindi hiki kiliporushwa kwa mara ya kwanza, leo na kesho, kuna fursa ya kuangalia marudio.

Leo Ijumaa, 05/08/2016, kipindi kitarudiwa Channel Ten, saa 2:30 usiku huu.
Kesho Jumamosi, 06/08/2016, kipindi kitarudiwa ITV saa 12:30 jioni!.

Wewe kama mwana jf, be the first to know!.

Paskali
 
Kwenye hili bora wangekaa kimya na kuliacha lipite,kuendelea kulizungumzia wakati sote tulishuhudia namna Demokrasia ilivyokanyagwa,ni dhihaka kwa Watanzania.

Alaaniwe yule aliyekuwa anatangaza matokeo kadri alivyokuwa anayapokea,bila kufahamu matokeo hayo yalipitia wapi kabla ya kumfikia!!
 
Wao wenyewe wanajua walishindwa
Huwezi kula matapishi yako ukaonekana mzima
Lazima upelekwe kupimwa.

Watanzania wanalifahamu hilo
Uchaguzi ule ulijawa na mihemuko na mbwembwe lakini kwa uhalisia
Upinzani haukuwa na hoja za maana kuchaguliwa
 
Mliambiwa toeni matokeo na onyesheni huko yalikopokelewa hayo ambayo hayakufika kwa aliyekuwa anatangaza midomo yenu ikaota gundi, na sasa fungeni vinywa vyenu visiseme tena.
 
Tanzania bara na visiwani, chaguzi zote zitaendelea kuwa huru na haki iwapo tume zinazosimamia chaguzi hizo zitaendelea kuwa chini ya rais!! Mungu ihurumie Tanzania!!
 
Mliambiwa toeni matokeo na onyesheni huko yalikopokelewa hayo ambayo hayakufika kwa aliyekuwa anatangaza midomo yenu ikaota gundi, na sasa fungeni vinywa vyenu visiseme tena.




Ni mpumbavu pekee,tena mwenye kiwango cha PhD ndiye anayeweza kukubaliana na sanaa ile iliyouingiza utawala huu madarakani,hata hao waliotangazwa washindi,hadi leo wanatumia mtutu wa bunduki na mabomu ya machozi kuulinda ushindi wao halamu.

Kama wanaamini kwa dhati kuwa walishinda,iweje leo hii wanatumia nguvu kubwa inayokiuka hadi misingi ya kidemokrasia na katiba yetu kuwadhibiti wale wanaotuaminisha kuwa waliwashinda katika uchaguzi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…