Tuzungumzie Recognition of Prior Learning (RPL)

Tuzungumzie Recognition of Prior Learning (RPL)

kalipeni

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
1,585
Reaction score
1,348
Habari wana jamvi!

Mimi kuna swala linanichanganya na kama ningekua na mamlaka wala nisingekubali lipite, ni Ili swala la recognition of prior learning.

Yani huwezi kuniambia darasa la saba umpe mitihani mitatu ya kucolify kwenda chuo kikuu alafu yote apige B then aende chuo kikuu mm kwa ushauri wangu nadhani kuna haja kama alivyosema mdau mmoja wa jf vyuo viweke entrance exams nadhani ii itakua njia nzuri kuwapukutisha kenge wote ktk kundi la mamba.

Sijui wana jamvi mnalizungumziaje ilo.
 
Vigezo vya RPL sio kufanya mtihani tu na kufaulu kwa daraja B bali pia ni pamoja na kujua lugha ya kingereza, awe amefanyia kazi taaluma anayotaka kwenda kuisomea kwa muda usiopungua miaka 10 au 15 (sina hakika kwenye miaka). Binafsi nadhani ni jambo zuri kwani kuna wazee wa mahakama hawana shahada ya sheria lakini kutokana na uzoefu wanajua sheria pengine kuzidi baadhi ya wasomi wa sheria. hilo pia ipo katika taaluma zingine.
 
Inawezekana kabisa huyo anayeingia Chuo Kikuu kupitia "Recognition of Prior Learning - RPL" akaandika kwa ufasaha kuliko ulivyoandika, kwa kuzingatia, pamoja na mambo mengine, matumizi (sahihi) ya kituo kikubwa, kituo kidogo, herufi kubwa, ndogo na utohoaji wa maneno ya Kiingereza!

Ninavyofahamu, utaratibu RPL umekuwa ukitumiwa na Vyuo vya hapa Nchini kwa miaka mingi. Mitihani ya sasa ya RPL inaweza kufananishwa na Mitihani iliyokuwa ikiiwa "Malticulation Test/Examinations". Utaratibu huu sio mgeni na huna haja ya ama kuwaogopa, kuwaonea wivu au kuwa na wasiwasi na hao unawaita "kenge" kwa vile wanajiunga na Elimu ya Chuo Kikuu kupitia utaratibu wa RPL.

Fahamu vilevile kuwa utaratibu wa RPL unatambulika, unakubalika na kutumika Kimataifa. Utaratibu huo unatumika katika Mataifa yaliyoendelea mfano Marekani, Kanada, Uingereza, China, Japan, Urusi, n.k. na zinazoendelea kama Tanzania, Kenya, n.k.

Mengine utayapata kupitia "Google Search Engine".
 
Inawezekana kabisa huyo anayeingia Chuo Kikuu kupitia "Recognition of Prior Learning - RPL" akaandika kwa ufasaha kuliko ulivyoandika, kwa kuzingatia, pamoja na mambo mengine, matumizi (sahihi) ya kituo kikubwa, kituo kidogo, herufi kubwa, ndogo na utohoaji wa maneno ya Kiingereza!

Ninavyofahamu, utaratibu RPL umekuwa ukitumiwa na Vyuo vya hapa Nchini kwa miaka mingi. Mitihani ya sasa ya RPL inaweza kufananishwa na Mitihani iliyokuwa ikiiwa "Malticulation Test/Examinations". Utaratibu huu sio mgeni na huna haja ya ama kuwaogopa, kuwaonea wivu au kuwa na wasiwasi na hao unawaita "kenge" kwa vile wanajiunga na Elimu ya Chuo Kikuu kupitia utaratibu wa RPL.

Fahamu vilevile kuwa utaratibu wa RPL unatambulika, unakubalika na kutumika Kimataifa. Utaratibu huo unatumika katika Mataifa yaliyoendelea mfano Marekani, Kanada, Uingereza, China, Japan, Urusi, n.k. na zinazoendelea kama Tanzania, Kenya, n.k.

Mengine utayapata kupitia "Google Search Engine".

na ww ni RPL nn mkuu ndugu yangu,mbona imekugusa sn, then iyo inayozungumziwa apo na matriculation test ni tofauti kwakua matriculation test zinasimamiwa na chuo husika na zinafanywa na wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na chuo husika thats why nikatoa ushauri ni bora na vyuo vikatoa entrance exams ambayo ndio sawa na matriculation test uliyozungumzia. "pamoja tunajenga"
 
na ww ni RPL nn mkuu ndugu yangu,mbona imekugusa sn, then iyo inayozungumziwa apo na matriculation test ni tofauti kwakua matriculation test zinasimamiwa na chuo husika na zinafanywa na wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na chuo husika thats why nikatoa ushauri ni bora na vyuo vikatoa entrance exams ambayo ndio sawa na matriculation test uliyozungumzia. "pamoja tunajenga"

Asante kwa ufafanuzi Mkuu. Hapana, kwa sasa mimi sio RPL. Nilibahatika kupita bila kukwama Darasa la Saba, Kidato cha IV, Kidato cha VI na IFM (ADA na PGD). Ninajiandaa na Msc mwaka huu. Hata hivyo, Elimu haina mwisho, siku zijazo naweza amua kubadili fani, mfano nikapenda kujiunga na SUA kwa Taaluma ya Kilimo, pengine nitatakiwa kupitia RPL! Ni mfano tu!

Kuna vilevile watu wenye uwezo darasani, lakini hawakubahatika kuendelea na Elimu ya Juu kama wewe na mimi, pengine kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao, umasikini, uyatima, ajali, uchache wa Vyuo miaka iliyopita, n.k. je ni haki kuwaita kenge na kuwafungia fursa za kujiendeleza kielimu?

"Pamoja tunajenga"!
 
na ww ni RPL nn mkuu ndugu yangu,mbona imekugusa sn, then iyo inayozungumziwa apo na matriculation test ni tofauti kwakua matriculation test zinasimamiwa na chuo husika na zinafanywa na wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na chuo husika thats why nikatoa ushauri ni bora na vyuo vikatoa entrance exams ambayo ndio sawa na matriculation test uliyozungumzia. "pamoja tunajenga"

Waache wakapige kitabu bwana, wakiwezeshwa wanaweza! Kama wewe pamoja na kupita chuo kikuu bado kuandika kiswahili tu inakuwa shida! Kwa nini nao tusiwabebe pamoja na kushindwa kwao?
 
Asante kwa ufafanuzi Mkuu. Hapana, kwa sasa mimi sio RPL. Nilibahatika kupita bila kukwama Darasa la Saba, Kidato cha IV, Kidato cha VI na IFM (ADA na PGD). Ninajiandaa na Msc mwaka huu. Hata hivyo, Elimu haina mwisho, siku zijazo naweza amua kubadili fani, mfano nikapenda kujiunga na SUA kwa Taaluma ya Kilimo, pengine nitatakiwa kupitia RPL! Ni mfano tu!

Kuna vilevile watu wenye uwezo darasani, lakini hawakubahatika kuendelea na Elimu ya Juu kama wewe na mimi, pengine kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao, umasikini, uyatima, ajali, uchache wa Vyuo miaka iliyopita, n.k. je ni haki kuwaita kenge na kuwafungia fursa za kujiendeleza kielimu?

"Pamoja tunajenga"!

naomba nieleweke kitu kimoja ndugu yangu,mm sina tatizo na hao wanaoenda kufanya iyo mitihani na kufaulu vigezo vilivyowekwa ili kwenda chuo kikuu,ila ni ukweli usiopingika kuwa wengi wao hawatakua na uwezo wa kufanya vizuri iyo mitihani na wapo wengi watakaopita kwa udanganyifu matokeo yake ni kua na wasomi wengi lakini ambao hawako vizuri katika fani walizosomea, na hao ndio kenge ninaowazungumzia.
 
Watanzania roho mbaya zitatumaliza, yani unaona mwenzio kufika ulipo no shda,
Huwez jua MTU hakuendelea kwa sababu gani, waliopitisha hii Elimu co wajinga.
Acha ubnafsi wew,khaaaaaa!
 
Wadau habarini kwanza, hii RPL binafsi nashindwa kuielewa vzur ingawa nimepitia pitia articles kadhaa. Najua humu kuna watu makini naomba kuelimishwa zaidi
 
Habari wana jamvi!

Mimi kuna swala linanichanganya na kama ningekua na mamlaka wala nisingekubali lipite, ni Ili swala la recognition of prior learning.

Yani huwezi kuniambia darasa la saba umpe mitihani mitatu ya kucolify kwenda chuo kikuu alafu yote apige B then aende chuo kikuu mm kwa ushauri wangu nadhani kuna haja kama alivyosema mdau mmoja wa jf vyuo viweke entrance exams nadhani ii itakua njia nzuri kuwapukutisha kenge wote ktk kundi la mamba.

Sijui wana jamvi mnalizungumziaje ilo.
Kweli mtu wa darasa la saba bado sana
 
Naomba kufahamishwa juu ya hiyo RPL, applications zake zinaanza lini, njia gani inatumika ku apply na application ina pelekwa wapi?.
 
Kwan foundation mbona imefutwa c inatumiwa na nchi zlizo endelea hyo naona bora mtu usome online nchi za nje bac tuambiwe hvo bac hayo mambo mengine
 
Ombi lako lilifanikiwa. Huu utaratibu wa Recognition of Prior Learning ulifanyika kwa miaka mitatu tu halafu ukafutwa mwaka 2017. Sasa hivi hakuna tena mitihani ya RPL. Ila Open University of Tanzania (OUT) wameruhusiwa na TCU kuendesha Foundation Courses, ambazo ni mlango wa ziada wa kuingia kwenye shahada.

Hata hivyo Foundation Program ya OUT sio sawa na RPL, maana RPL ilikuwa inaruhusu wenye cheti cha darasa la saba kufanya mitihani ya kujiunga na shahada. Foundation lazima uwe na cheti cha kidato cha nne.
 
Foundation programme ya Out inahitaji mwanafunzi aliyefaulu kidato cha nne na akapungukiwa sifa ya kujiunga chuo kikuu yaani akiwa na principle 1 na S1 ya advanced level yenye jumla ya cut point ya 1.5 ndipo unaruhusiwa kusoma lakini siyo kidato cha nne ndugu.
 
Back
Top Bottom