Elections 2010 Tuzo ya Milenia; Hongera Chaguo la Mungu Kikwete,Ushahidi Huu Hapa (PICHA)

Mzalendo_Mwandamizi

JF-Expert Member
Dec 12, 2007
1,117
4,764
Kama ilivyotarajiwa, "ushindi wetu" wa Tuzo ya Milenia (MDG) umeshageuka mtaji kwa Serikali ya Chaguo la Mungu Jakaya Kikwete.Nimeonelea kuandika makala ya habari-picha kutoa pongezi kwake nikiambatanisha picha zinavyoonyesha tulivyostahili Tuzo hiyo.Naamini picha hizo zitamsaidia kila mpiga kura mzalendo kufanya maamuzi sahihi hapo tarehe 31 Oktoba.

2r7vgo7.jpg


2ptqckw.jpg


1yv4zp.jpg


Kutokana na wingi wa picha hizo,ukipata wasaa angalia nyinginezo kwenye kiungo (link) hiki KULIKONI UGHAIBUNI: Tuzo ya Milenia: Hongera Chaguo La Mungu KIKWETE,Ushahidi Huu Hapa (PICHA)
 
Ndugu zangu je tunaweza kutengeneza vipeperushi zenye kuonyesha hali ya watoto wetu na kuvisambaza kwa watu wengi. Ndugu wa Kulikoni Ughaibuni je unatoa ruhusa watu tutumie picha zako na nyinginezo kuonyesha jinsi hali yetu ilivyo mbaya? Ninadhani vipeperushi ambavyo vina pucha kama hizi vitaisaidia kuwaelimisha Watanzania wenzetu kuweza kufanya uamuzi wa kweli. Yeyote mwenye takwimu nzuri katika huduma ya afya, elimu na maji zisaidia sana katika kuandika vipeperushi vya uhakika ili kuweza kuanika ukweli mbagani (hadharani) (Mimi hupenda kutumia maneno ya makabila yetu badala ya yale yenye asili ya kiarabu kama yapo kwani kanuni ya kwanza ya kutohoa Kiswahili ni kutumia neno la lugha yoyote ile ya kibantu kabla ya kutumia maneno ya nje ya lugha hizo. Kwa wenzetu Wahaya neno mbaga humaanisha umati wa watu na hivyo neno mbagani linafaa kwa malengo haya).
 
Ndugu zangu je tunaweza kutengeneza vipeperushi zenye kuonyesha hali ya watoto wetu na kuvisambaza kwa watu wengi. Ndugu wa Kulikoni Ughaibuni je unatoa ruhusa watu tutumie picha zako na nyinginezo kuonyesha jinsi hali yetu ilivyo mbaya? Ninadhani vipeperushi ambavyo vina pucha kama hizi vitaisaidia kuwaelimisha Watanzania wenzetu kuweza kufanya uamuzi wa kweli. Yeyote mwenye takwimu nzuri katika huduma ya afya, elimu na maji zisaidia sana katika kuandika vipeperushi vya uhakika ili kuweza kuanika ukweli mbagani (hadharani) (Mimi hupenda kutumia maneno ya makabila yetu badala ya yale yenye asili ya kiarabu kama yapo kwani kanuni ya kwanza ya kutohoa Kiswahili ni kutumia neno la lugha yoyote ile ya kibantu kabla ya kutumia maneno ya nje ya lugha hizo. Kwa wenzetu Wahaya neno mbaga humaanisha umati wa watu na hivyo neno mbagani linafaa kwa malengo haya).

A wise man would show sucess and failures if you mean you like your country, huu ni ushabiki ambao hauna msaada sana kuijenga nchi yetu. Mimi ningekuelewa kama ungeweka picha moja ya shule nzuri kati ya nyingi zilizopo na hiyo ya shule yenye matatizo ili changamoto iwe ni hizo tofauti. Watanzania wengi wana upeo sasa not to be bulldosed as you suggest.
 
Back
Top Bottom