Tuwe macho; mfuko uitwao "ukwasi" una tofauti na deci?

Tuwe macho; mfuko uitwao "ukwasi" una tofauti na deci?

Kimagege

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2010
Posts
283
Reaction score
88
Nimeona wakiutangaza huu mfuko katika kituo cha ITV na wanadai kuwa unapata mahela mengi fasta ndani ya kipindi kifupi sana.

Binafsi sioni tofauti yake na deci iliyowatapeli watu na kutokomea kusikojulikana huku kesi iliyofunguliwa pale Kisutu ikiwa imetoweka kiaina.

Kwa wanaofahamu zaidi watujuze ili watanzania wenzetu wasitapeliwe tena na wahuni wachache wanaofungiwa macho na serikali.
 
UKWASI!! Wanafanua unaendeshwa vipi? Wanakibali kutoka BoT? Ipo chini aya nani? Mhhh... "eti unapata mahela...". Mbona hata huyo mwenye ITV anapambana na TCRA juu ya gharama za kuhamia digitali, si ajiunge kisha atupe ving'amuzi bure. Aisee baba angu ee linapokuaj swala la hela za promosheni, nakuwa na maswali mengi. Sis wengine hizo taarifa za habari hatujuio tuliangalia lini. Pia si kote kuna ITV au Radio One (IPP Media kwa ujumla).
 
Mahela
mapesa
airtel milionea
amka milionea
deci
ukwasi
*************hawa watakuwa ndugu*************
 
Mwanzo Mlipanda Pesa safari hii mtapanda Akili! Mtu anaependa pesa za burebure kama hizo huishia kubaya,Mengi kala sana pesa za Jackpot Bingo sasa wanakuja kivingine!
 
Mimi sijui inaoperate vipi lakini nadhani ni vyema tukafanya utafiti wa kina kwanza kabla ya kulaumu na kuifananisha na DECI
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom