Tuwasikilize wenye akili kubwa kuiboresha nchi yetu

Mi naonelea kuhusu Majimbo ya uchaguzi tufate Katiba ya Warioba, Tanzania inafaa kuwa na Wabunge 150 tu na Sidhani kama Tunahitaji Rundo la Wabunge 393..

Tutapunguza matumizi ya Fedha sana..

Pili kuondoa wabunge wa Viti maalumu maana hawa hawawajibiki kwa Wananchi zaidi ya Kuwajibika kwa wao wenyewe na matumbo yao..

Tuige Katiba ya kenya Ambapo Mbunge anaweza kuwajibishwa na Raia endapo atakosea au atasema kile ambacho hawakumtuma..
 
Kwa Idadi yoyote ile ya wabunge, uwakilishi wa jimbo ni muhimu uzingatie idadi halisi ya wapiga kura na sio jiografia ya milima, mito, misitu na barabara.

Ni kituko mbunge mmoja anawakilisha wapiga kura laki tatu na mwingine anawakilisha wapiga kura elfu ishirini.
 
Nchi yetu ilipofikia sasa inahitaji Rais ajaye awe Katili sana. Aje awatapishe mafisadi pesa zote walizopora, walizoficha Nje ya Nchi zirejeshwe, wafungwe gerezani au tuwatie ndani, aaachane na Plea Bargain inahamasisha wizi.
Hatuhitaji Rais Katili nali Rais anayeweza kusimamia Sheria na Uwajibikaji kwa dhati.

Sio bla bla za wale waliopita.
 
Kwa mfano Mpiga kura anayewakilisha Jimbo la Ngorongoro anawakilisha Kina Nani?
Na watu wanahamishiwa Msomera?
 
Sahihi
 
Dah hizi takwimu za majimbo na wapigakura wao zinahuzunisha, zinakera na zinatia hasira! Na bado kuna mijitu inaendelea kuunda majimbo ili kuongezeana ulaji
 
Mawazo mazuri sana,
Hata mimi kila siku huwa nafikiria inawezekanaje watu wanaotuongoza hili jambo limekuwa gumu kulifanyia kazi!!!

Eneo kama la kurasini mpaka eneo la keko na kilwa road , limejaza vijumba ambavyo serikali ingeweza kulitwaa wajengewe nyumba maeneo mengine,

Eneo hilo liwe kwa ajili ya shughuli za bandari tu, badala ya kufikiria kuingiza pesa nyingine kule Bagamoyo,

Hiyo pesa ingetosha kujenga barabara nyingine ya Malori tu mpaka kibaha au Vigwaza,

Mpango wa Magufuli kuwa na bandari kavu kule vigwaza sijui hata uliishia wapi , mambo ya ajabu sana haya,

Pale misugusugu kwenye sijui kuna gani pale ya serikali , ni eneo duni sana ambalo truck zote za kwenda nje lazima zistop kwanza pale,

Ni eneo baya , halina miundombinu mizuri kwa malori kupack!! Lakini lipo vilevile miaka na miaka,

Kusema kweli ni aibu kubwa sana kwa nchi kama hii,

Barabara kutoka kibaha mpaka Chalinze ndio kioo cha nchi yetu , lakini hakuna mtu anajali,

Kila siku ni hadithi tu kuwa inajengwa lakini hakuna kitu.

Inasikitisha sana
 
Huyu mama Nkaya anataka kufukuzwa chadema aisee ,inawezekanaje anapinga uwepo wa wabunge wa viti maalum? Hivi hajui kuwa mke wa Naibu Katibu mkuu wa chadema yuko bungeni kwa viti maalumu?
 
Huyu mama Nkaya anataka kufukuzwa chadema aisee ,inawezekanaje anapinga uwepo wa wabunge wa viti maalum? Hivi hajui kuwa mke wa Naibu Katibu mkuu wa chadema yuko bungeni kwa viti maalumu?
Mbona Mpina ni CCM na huwa anapinga mambo yake mengi??
 
Duh hii nchi ujinga ni mwingi sana, watu laki 5 majimbo 50, Donald Trump akiwatukana waafrica wana mnamuona mbaya.
 
Na kama Mbowe angekuwa type ya Cheyo, Lipumba, Mrema au ndumilakuwili wengine kama hao, hungesikia haya makelele.
 
Chadema iitishe uchaguzi haraka sana, mwenyekiti wake amepitiliza kukalia kiti, hii si afya katika chama kinachojitanabai ya kwamba kina demokrasia safi, hili sio demokrasia hilo ni udikteta, hii inareflect nini kitatokea watakapo twaa madaraka.
Na tuna mrudisha kitini huyo huyo msiyempenda....mitano tena kwa mhe mbowe
 
Mbona Mpina ni CCM na huwa anapinga mambo yake mengi??
CCM kuna uvumilivu wa hoja mmbadala ,chadema ukitofautiana nao wanakutumua ,reje kuhusu Zitto na Kitila
 
Akili kubwa, mawazo yakinifu๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘
 
Dah hizi takwimu za majimbo na wapigakura wao zinahuzunisha, zinakera na zinatia hasira! Na bado kuna mijitu inaendelea kuunda majimbo ili kuongezeana ulaji
Yaani kiukweli Nchi yetu inaongozwa na Wezi tupu.

Hakuna Kiongozi mwenye Nia ya Kuleta Maendeleo ataendelea na huu mfumo.

Ikiwa no hivyo basi ni Bosheni tu.
 
CCM kuna uvumilivu wa hoja mmbadala ,chadema ukitofautiana nao wanakutumua ,reje kuhusu Zitto na Kitila
Ccm ipi wanaongoza kupean sumu?

Hata Steve naye mlitaka kumuua

Sasa steve ana nini jamani mlitaka kumtoa roho?

Si kupiga Bomu Mortuary?
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
 
Naona na ccm waige utaratibu wenu, ili mama Samia awe ni mwenyekiti wa kudumu na Rais wa milele!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ