Tuwasaidie waliopatwa na maafa arusha.

Sadagada

Member
Dec 9, 2011
76
37
Binafsi nimehuzunishwa sana na maafa yaliyotokea Arusha.
Nahisi hata mimi ningeweza kukumbwa na matatizo kama hayohayo kwani huwa nahudhuriaga mikutano ya hadhara ya vyama vyote.
Nashauri iundwe timu yenye uaminifu kwa ajili ya kukusanya michango ya kuwasaidia wale wote waliojeruliwa vibaya ili waweze kupatiwa matibabu. Kumbukeni gharama za matibabu siku hizi zipo juu sana.
Hima watanzania wenzangu, tuwasaidie ndugu zetu waliokumbwa na mkasa mbaya uliosababishwa na watu ambao wana uchu wa madaraka.
EWE MWENYEZI MUNGU TUNAOMBA UTUJALIE TUMTAMBUE HUYU ANAYEUMIZA WATU WAKO WASIOKUWA NA HATIA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Taarifa zilidai kuwa kuna mtu alionekana akirusha kitu kinachodaiwa bomu kwenye eneo la jukwaa karibu na gari la matangazo la chama hicho, lakini alipokuwa akifuatiliwa baada ya kutokea mlipuko huo, polisi nao walikuwa wameanza kudhibiti watu kwa kulipua mabomu ya kutoa machozi na kupiga risasi za moto hali iliyozidisha taharuki.
 
Back
Top Bottom