Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Kila kunapokucha tunasikia makelele mengi sana kuhusu matumizi ya hela ya CHADEMA na mapungufu mengine mengi ya viongozi wa chama. Tulianza kuyasikia haya tangu wakati wa akina Mtela, na sasa akina Mwigamba. Lakini hatujawahi kusikia hata mtu mmoja anahoji matumizi ya hela na mapungufu ya kiuongozi yaliyopo kwenye vyama vingine. Wakati huo huo watanzania wote ni mashahidi kwamba ni CHADEMA pekee hapa nchini ndiyo inayofanya vema katika shughuli za kisiasa na kuwapa wakati mgumu sana CCM. Wote tunajua kwamba ni CHADEMA inayojishughulisha na harakati/program mbalimbali zinazogharimu mamilioni ya fedha katika harakati za kujijenga.
Ni kwanini hivi vyama vingine haviulizwi kama vinapeleka wapi ruzuku ilihali hatuoni harakati zozote za kujenga chama kama zinazofanywa na CHADEMA? Ni kwanini viongozi wa vyama vingine hawaulizwi hata pale vyama vyao vinapopoteza umaarufu na kuteketea. Hivi ni nani aliyewahi kuhoji uhalali wa Mtikila, Mrema au Cheyo kuendelea kuwa viongozi wa vyama vyao, pamoja na vyama vyao kuteketea kabisa kisiasa? Ni nani aliyehoji uhalali wa Lipumba na Seif kuendelea kuwa viongozi wa CUF huku wote tukishuhudia CUF inavyopoteza umaarufu na kupotea kwenye ramani ya siasa nchini? Ni kwanini kila kuchapo ni wafuasi wa CHADEMA tu wanaibuka na kujifanya wasamalia wema wenye nia ya kukiokoa chama kwa kueleza mapungufu lukuki ya uongozi wa CHADEMA, huku wote tukishuhudia kazi nzuri inayofanywa na CHADEMA Katika siasa za Tanzania?
Kwahakika mimi kama mwanaCHADEMA mwenye akili timamu, na ninayefikiri kwa kina, siwezi kutilia shaka matumizi yoyote ya fedha ndani ya chama hiki kwa kuwa outputs za kazi ya hiyo fedha zinaonekana. Hata kama kuna makombo ambayo yanaokotwa na kuliwa si kitu, kwa kuwa naamini kiasi kikubwa kinatumiwa kwa kazi za siasa. Hata mimi ningepewa nafasi kama za viongozi wa CHADEMA hivi sasa, naamini kuna mahali ningejipendelea. Mimi ni binadamu lazima ningefanya hivyo, kwanini wakifanya wengine liwe ni jambo kuubwa la kupita kupiga kelele mitaani ilihali hata mimi katika mapungufu yangu naweza kufanya hayohayo?
Hebu tufikirie hili: CCM wanapokea ruzuku kubwa zaidi kushinda ya CHADEMA kwa karibu mara tatu kama si nne, lakini hatuoni chochote wanachokifanya? Je kuna yeyote amewahi kujifanya ni mwanaCCM mkereketwa wa kutetea matumizi ya fedha ndani ya CCM na kuhoji mahali zinakopelekwa fedha zote za ruzuku na za misaada kutoka vyama rafiki wa CCM? CUF kikiwa kama chama kikuu cha upinzani Zanzibar, na chama chenye wabunge wengi next to CHADEMA, kinapokea kiasi kikubwa cha ruzuku, lakini hakijishughulishi na harakati za kukijenga chama kama ambavyo CHADEMA inafanya kwa ruzuku zake kidogo, mbona huko hatuoni yeyote anajitokeza na kujifanya msamalia mwema mwenye nia ya kukiokoa CUF na matumizi mabaya ya fedha?
Nitamshangaa sana mwanaCHADEMA yeyote atakayeinuka na kusema eti ameshawishika vya kutosha na propaganda za akina Mwigamba na vibaraka wengine wa CCM na kuanza kukichukia au kuwachukia viongozi wakuu wa chama. Kwa akili ya kawaida kabisa, unaweza kutambua kuwa hapa pana kitu kinaendelea; kuna watu ndani ya CHADEMA wananunuliwa na CCM na kukubali kutumika katika harakati za kukichafua na kukivuruga chama ili kipoteze uwezo wa kutoa ushindani wa kutosha kwa CCM. Ni dhahiri kwamba vita yetu inazidi kuwa pana na ngumu. Ni wakati wa kila mwanachadema sasa kusimama na kuwapinga hawa vibaraka wa CCM waliopo ndani ya CHADEMA.
Ni kwanini hivi vyama vingine haviulizwi kama vinapeleka wapi ruzuku ilihali hatuoni harakati zozote za kujenga chama kama zinazofanywa na CHADEMA? Ni kwanini viongozi wa vyama vingine hawaulizwi hata pale vyama vyao vinapopoteza umaarufu na kuteketea. Hivi ni nani aliyewahi kuhoji uhalali wa Mtikila, Mrema au Cheyo kuendelea kuwa viongozi wa vyama vyao, pamoja na vyama vyao kuteketea kabisa kisiasa? Ni nani aliyehoji uhalali wa Lipumba na Seif kuendelea kuwa viongozi wa CUF huku wote tukishuhudia CUF inavyopoteza umaarufu na kupotea kwenye ramani ya siasa nchini? Ni kwanini kila kuchapo ni wafuasi wa CHADEMA tu wanaibuka na kujifanya wasamalia wema wenye nia ya kukiokoa chama kwa kueleza mapungufu lukuki ya uongozi wa CHADEMA, huku wote tukishuhudia kazi nzuri inayofanywa na CHADEMA Katika siasa za Tanzania?
Kwahakika mimi kama mwanaCHADEMA mwenye akili timamu, na ninayefikiri kwa kina, siwezi kutilia shaka matumizi yoyote ya fedha ndani ya chama hiki kwa kuwa outputs za kazi ya hiyo fedha zinaonekana. Hata kama kuna makombo ambayo yanaokotwa na kuliwa si kitu, kwa kuwa naamini kiasi kikubwa kinatumiwa kwa kazi za siasa. Hata mimi ningepewa nafasi kama za viongozi wa CHADEMA hivi sasa, naamini kuna mahali ningejipendelea. Mimi ni binadamu lazima ningefanya hivyo, kwanini wakifanya wengine liwe ni jambo kuubwa la kupita kupiga kelele mitaani ilihali hata mimi katika mapungufu yangu naweza kufanya hayohayo?
Hebu tufikirie hili: CCM wanapokea ruzuku kubwa zaidi kushinda ya CHADEMA kwa karibu mara tatu kama si nne, lakini hatuoni chochote wanachokifanya? Je kuna yeyote amewahi kujifanya ni mwanaCCM mkereketwa wa kutetea matumizi ya fedha ndani ya CCM na kuhoji mahali zinakopelekwa fedha zote za ruzuku na za misaada kutoka vyama rafiki wa CCM? CUF kikiwa kama chama kikuu cha upinzani Zanzibar, na chama chenye wabunge wengi next to CHADEMA, kinapokea kiasi kikubwa cha ruzuku, lakini hakijishughulishi na harakati za kukijenga chama kama ambavyo CHADEMA inafanya kwa ruzuku zake kidogo, mbona huko hatuoni yeyote anajitokeza na kujifanya msamalia mwema mwenye nia ya kukiokoa CUF na matumizi mabaya ya fedha?
Nitamshangaa sana mwanaCHADEMA yeyote atakayeinuka na kusema eti ameshawishika vya kutosha na propaganda za akina Mwigamba na vibaraka wengine wa CCM na kuanza kukichukia au kuwachukia viongozi wakuu wa chama. Kwa akili ya kawaida kabisa, unaweza kutambua kuwa hapa pana kitu kinaendelea; kuna watu ndani ya CHADEMA wananunuliwa na CCM na kukubali kutumika katika harakati za kukichafua na kukivuruga chama ili kipoteze uwezo wa kutoa ushindani wa kutosha kwa CCM. Ni dhahiri kwamba vita yetu inazidi kuwa pana na ngumu. Ni wakati wa kila mwanachadema sasa kusimama na kuwapinga hawa vibaraka wa CCM waliopo ndani ya CHADEMA.