Tuwakatae Maaskofu wa aina ya Gwajima

Tuwakatae Maaskofu wa aina ya Gwajima

singidadodoma

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2013
Posts
4,394
Reaction score
1,538
Sikubaliani na baadhi maaskofu wa aina ya Gwajima kwa kuwa baadhi yao wameshiriki kuvunja ndoa nyingi na kuzifilisi baadhi ya familia huku wao wakijitajirisha kwa kutumia migongo ya ujinga wa baadhi ya waumini wao.

Sikubaliani nao kwa kiasi kikubwa watu waliojipachika uaskofu na unabii wakati nafsi zao zimejaa mambo machafu.

Pia nawachukuia watu waojipachika majina ya uaskofu kwa lengo la kuwaghilibu Watanzania wenzao, ambao wamekumbwa na misongo ya maisha, shida za kila aina ambao hujikuta wakiangukia mikononi mwa hawa matapeli wanaojifanya wana uwezo wa kuwaondolea shida zao.

Wanajiita Maaskofu, manabii, mitume, mitume wa fedha, n.k. ni kejeli na fedheha kwa Mungu! Wanajifanya watumishi wa Mungu lakini kumbe wamejaa roho ya kutumikiwa. Wanasema wao ndio wafuasi wa Kristo lakini hawafuati mafundisho na maisha ya Kristo.

Wanasema wanachunga kondoo wa Bwana wakati wao ndio mbwa mwitu wakali wanaotafuna kondoo za Bwana na kuwalazimisha watu kutoa kila kitu walichonacho hadi wanafilisika lakini kumbe wao wanaishi kwa ufahari mkubwa! Wanalaumu serikali kwa ufisadi kumbe wao ndio mafisadi wa mali za kanisa na waumini wao. Hawana huruma hata kidogo, nia yao ni kula na kushibisha matumbo yao kwa vijisenti vya maskini!

Umewahi kuwasikia hata siku moja wakiweka mikakati makanisani mwao ya jinsi ya kuwasaidia maelfu ya maskini na yatima tuliono? Kati ya vitu wasivyopenda kusikia watu hawa ni huduma kwa watoto yatima, wajane na walemavu.

Kwa tabia hiyo ya maaskofu hao hujipatia fedha nyingi kwa njia ya sadaka, mavumo makubwa kutoka waumini wao ambayo huwapa kiburi na kujiona miungu watu na kutoona haya kuwasema maaskofu wa ukweli, walioupata uaskofu wao darasani na kwa uwezo wa Mungu muumba mbingu na ardhi.

Sikubaliani na maakofu hawa matapeli kwa sababu baadhi yao tunafahamu vizuri historia zao na maisha yao kwa ujumla, historia ya maisha machafu na tabia za kishetani ndio maana wanakimbilia katika ulokole ili kusafisha historia zao ndani ya jamii, huku baadhi yao wakifanikiwa kuanzisha hata makanisa lakini ukiangali kwa ukweli hayana hata hadhi ya kuitwa makanisa.

Naamini makanisa kama haya ya kina Gwajima na maaskofu wengine kama kina Gwajima ndio yale ya manabii wa uongo walioelezwa na Yesu Kristo, mbele ya wanafunzi wake kwamba watatokea mwisho wa dunia na wengi watajifanya wana uwezo wa kuponya.

Makanisa haya yanayoibuka kama uyoga hayana tofauti na yale yaliyotokea Uganda ambako Kibwetere aliwafungia ndani waumini wake na kuwateketeza kwa moto.

Rai yangu kwa Serikali: Upo umuhimu mkubwa sasa, pamoja na uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa katiba yetu lakini mamlaka ya usajili wa makanisa na misikiti iwe makini kwa watu wanaojianzishia madhebu kila kukicha kwani mengine yamekuwa yakiwatia umasikini Watanzania na kuleta uchochezi hapa nchini.
 
..magamba mnavyo hangaika kuleta uzi mpya kila dakika maskini.. nani aliwatuma mkamchokoze? #mkome!
 
Mlimleta Slaa akaanzisha siasa za kipuuzi, sasa wengine wameamua kujibu mapigo kwa njia ileile mnaanza kulialia. Jiheshimuni na mshindane kwa hoja uone kama kuna tatizo lolote. Na safari hii mkithubutu kuiba kura tutawatia adabu.
 
Unamkataa Gwajima kwa kuwa amesema yale ambayo masikio yako hayataki kuyasikia. Lakini ulimkubali Dr. Slaa kwa kuwa alisema yale ambayo masikio yako yalikuwa tayari kuyasikia. Umasahau..!! Huwezi kila siku kupata kile unachokitaka. Uwe mvumilivu kusikia usichokitarajia. Sawa mkuu?
 
Maskini ccm! Hivi mlipo mtuma slaa kudhalilisha watu mlifikiri wao hawasikii uchungu?Slaa amewavuruga wengi hasa kitendo cha kutuaminisha ufisadi ulioko ccm ni bora kulioko waliotoka.Kawatuhumu watu na leo kajibiwa nyinyi mnalia nini? Mbona leo mnahaha hivi?Eti askofu uchwara kati ya Gwajima na Slaa nani amevunja misingi ya kazi ya kiroho?Tulieni kama sisi leo ni zamu yenu ya kusononeka.
 
Alipozungumza Dr. Slaa mlifurahi sana na mkataka aendelee kusema na mengine. Sasa wanaojua ukweli wa mambo wamesema mumeona haitakiwi hapa sijawaelewa kabisa!

Dr.Slaa katika mazungumzo yake alimtaja Gwajima na ndiye kamjibu ili naye kujisafisha kwa umma tatizo lake nini Watanzania?
 
Gwajima angepiga mawe chadema angekuwa bonge la Askofu
 
Wacha kabisa chuki binafsi,hujalazimishwa lazima ujue kuwa imani ya mtu huwezi kuibadilisha kwa kuandika, huna haki ya kumshambulia askofu wetu kwa kuwa wewe hukubaliani naye, uvumilivu wa kiimani unatakiwa, kama huna imani naye sisi tuna imani naye, tena ukome kabisa kuwachagulia watanzania nini dini wafuate
 
Maskini ccm! Hivi mlipo mtuma slaa kudhalilisha watu mlifikiri wao hawasikii uchungu?Slaa amewavuruga wengi hasa kitendo cha kutuaminisha ufisadi ulioko ccm ni bora kulioko waliotoka.Kawatuhumu watu na leo kajibiwa nyinyi mnalia nini? Mbona leo mnahaha hivi?Eti askofu uchwara kati ya Gwajima na Slaa nani amevunja misingi ya kazi ya kiroho?Tulieni kama sisi leo ni zamu yenu ya kusononeka.

Mkuu ni kweli kabisa hawa watu wasitufanye kuwa sisi ni makondoo,wasitufanye tuamini wanachotaka wao,mchungaji gwajima ni kiongozi wa kiroho wa mamilioni kama huyo slaa wao,nasi tuna muamini Gwajima pia,huu siyo wakati wa kuchaguliana kiongozi wa kiroho,sisi tunamwamini Gwajima
 
Tuna kulaani kabisa kwa kumshambulia kiongozi wetu wa kiroho, ni vizuri tukaheshimu imani zetu za kidini, hata kama hukubaliani na kiongozi fulani siyo lazima kumpinga na kumtolea maneno yasiyo faa, hivi unaamini kila mtu atafurahia unacho amini wewe? chunga sana ulimi wako hasa kipindi kama hiki na ujue kuwa uvumilivu ndio ngao yetu watanzania.
 
Unamkataa Gwajima kwa kuwa amesema yale ambayo masikio yako hayataki kuyasikia. Lakini ulimkubali Dr. Slaa kwa kuwa alisema yale ambayo masikio yako yalikuwa tayari kuyasikia. Umasahau..!! Huwezi kila siku kupata kile unachokitaka. Uwe mvumilivu kusikia usichokitarajia. Sawa mkuu?

Napenda sana watu kama wewe humu jf haha.
 
Kwenye kudai uhuru mwaka 61 kuna swala la church movement wachungaji walihusika sana kuleta mabadiliko so gwajima ni muhimu
 
Mkuu ni kweli kabisa hawa watu wasitufanye kuwa sisi ni makondoo,wasitufanye tuamini wanachotaka wao,mchungaji gwajima ni kiongozi wa kiroho wa mamilioni kama huyo slaa wao,nasi tuna muamini Gwajima pia,huu siyo wakati wa kuchaguliana kiongozi wa kiroho,sisi tunamwamini Gwajima

Period.
 
Back
Top Bottom