Tuwaambieni ukweli viongozi wetu!

Tuwaambieni ukweli viongozi wetu!

Jibu swali unadhani katiba mpya itakusaidia jambo gani moja tuu unaloona ni la muhimu kwako?
Kupunguza madaraka ya Urais, mahakama kumshitaki rais anapohujumu nchi,tume huru ya uchaguzi ...hili nila muhimu sana maana tunaongozwa na viongozi wa ajabu ajabu
 
Kupunguza madaraka ya Urais, mahakama kumshitaki rais anapohujumu nchi,tume huru ya uchaguzi ...hili nila muhimu sana maana tunaongozwa na viongozi wa ajabu ajabu
Umeisoma katiba ya sasa na ukaielewa vizuri?
 
Kuna wakati huwa natafakari na kufanya tathmini; nadhani kuna ukweli kwa kile ninachotafakari!

Viongozi wengi wa kisiasa hudhani kwamba watanzania hawajui chochote. Wanadhani kwa kuwa wao hawakuwa na fursa ya kujua mambo mengi enzi hizo wanaishi vijijini, basi wanadhani hata sasa hali ni ileile!

Siku fulani nilikuwa kwenye gari ya umma tunasafiri huku (mkoani), nikawa nazungumzia masuala ya kisiasa, baba mmoja akasema kwa kustaajabu "kumbe hata watanzania wa kawaida wanajua kinachoendelea!"
Alionekana kama vile ni mtumishi fulani wa serikali kwa haiba yake. Sikutaka kujieleza sana!

Kwahiyo kama viongozi wanadhani wananchi waliowafahamu hapo kabla ndio hawa wa leo, basi wanajidanganya!

Kuna wasomi wa vyuo vikuu wako huku vijijini wanasubiri ajira. Kuna vijana waliomaliza elimu ya sekondari (shule za kata) wapo mtaani na wanafuatilia kila kinachoendelea.

Ingawaje serikali inawarubuni kucheza kamari kwa kuruhusu biashara ya kubet, na kuhamasisha unywaji wa pombe; bado wapo wachache wanaojitambua!

Nchi ni yetu sote!
Watu bana wakibahatika kupa pesa nyingi hubadirika kwa wale wabeba dhamana nawao wanakuwa na tabia ya unyumbu ambapo huahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza ama kutumikia kundi fulani na uoga
 
wanasema ukimnyooshea mwenzio kidole kimoja vitatu vinakunyooshea wewe mwenyewe. Tafakari
Sasa mi nimefanyaje mkuu?
Au hujamsikia aliyetamka?
Mie nimefanya kugoogle tu kujua maana!
 
Tubaki nayo tu hii kama ilivyowasilishwa! Yana mwisho wake hayo yote!View attachment 2748294
Samahani, naomba kuuliza wanajf kwa heshima na taadhima; kama kweli hii ndio maana iliyokusudiwa na kiongozi wetu kwa kutumia lugha ya kiarabu kutoa dukuduku lake, je wajomba wakikodishwa hiyo bandari kwa mkataba wa milele; si watakuwa wanawagombeza (insult) wafanyakazi wa kitanzania kwa kiarabu??
Nimeuliza tu jamani sio kwa ubaya!
 
Back
Top Bottom