Lanlady
JF-Expert Member
- Feb 27, 2019
- 1,913
- 6,524
Kuna wakati huwa natafakari na kufanya tathmini; nadhani kuna ukweli kwa kile ninachotafakari!
Viongozi wengi wa kisiasa hudhani kwamba watanzania hawajui chochote. Wanadhani kwa kuwa wao hawakuwa na fursa ya kujua mambo mengi enzi hizo wanaishi vijijini, basi wanadhani hata sasa hali ni ileile!
Siku fulani nilikuwa kwenye gari ya umma tunasafiri huku (mkoani), nikawa nazungumzia masuala ya kisiasa, baba mmoja akasema kwa kustaajabu "kumbe hata watanzania wa kawaida wanajua kinachoendelea!"
Alionekana kama vile ni mtumishi fulani wa serikali kwa haiba yake. Sikutaka kujieleza sana!
Kwahiyo kama viongozi wanadhani wananchi waliowafahamu hapo kabla ndio hawa wa leo, basi wanajidanganya!
Kuna wasomi wa vyuo vikuu wako huku vijijini wanasubiri ajira. Kuna vijana waliomaliza elimu ya sekondari (shule za kata) wapo mtaani na wanafuatilia kila kinachoendelea.
Ingawaje serikali inawarubuni kucheza kamari kwa kuruhusu biashara ya kubet, na kuhamasisha unywaji wa pombe; bado wapo wachache wanaojitambua!
Nchi ni yetu sote!
Viongozi wengi wa kisiasa hudhani kwamba watanzania hawajui chochote. Wanadhani kwa kuwa wao hawakuwa na fursa ya kujua mambo mengi enzi hizo wanaishi vijijini, basi wanadhani hata sasa hali ni ileile!
Siku fulani nilikuwa kwenye gari ya umma tunasafiri huku (mkoani), nikawa nazungumzia masuala ya kisiasa, baba mmoja akasema kwa kustaajabu "kumbe hata watanzania wa kawaida wanajua kinachoendelea!"
Alionekana kama vile ni mtumishi fulani wa serikali kwa haiba yake. Sikutaka kujieleza sana!
Kwahiyo kama viongozi wanadhani wananchi waliowafahamu hapo kabla ndio hawa wa leo, basi wanajidanganya!
Kuna wasomi wa vyuo vikuu wako huku vijijini wanasubiri ajira. Kuna vijana waliomaliza elimu ya sekondari (shule za kata) wapo mtaani na wanafuatilia kila kinachoendelea.
Ingawaje serikali inawarubuni kucheza kamari kwa kuruhusu biashara ya kubet, na kuhamasisha unywaji wa pombe; bado wapo wachache wanaojitambua!
Nchi ni yetu sote!

