JamiiTalks Tutumie taarifa za Rushwa ya Ngono na Unyanyasaji sehemu ulipo, ili Mamlaka za Serikali zizifanyie kazi

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,012
TUHUMA ZA RUSHWA YA NGONO: TAARIFA ZAIDI ZINAHITAJIKA
jamiiforums_20191212_3.jpg

Habari,

Kumekuwa na tuhuma kadhaa ambazo zimekuwa zikisambaa kwenye Mtandao wa JamiiForums zikielekezwa kwa madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya

Wengi wa walioleta tuhuma hizo hawakuleta taarifa za kina ili kusaidia kuwatia hatiani wanaotuhumiwa

Kupitia Miscellaneous Amendment Act namba 3 ya mwaka 2016, Sheria ya Uhujumu Uchumi ilifanyiwa mabadiliko na kutambua makosa yote yaliyopo ndani ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (isipokuwa kosa chini ya Kifungu cha 15) ni makosa ya Uhujumu Uchumi

Hivyo, Rushwa ya Ngono kwa sasa ni Kosa la Uhujumu Uchumi na adhabu yake sio faini tena ila ni kifungo cha mpaka miaka 20 jela

Vyombo vya Dola vimeziona tuhuma hizo (katika JF) na Mamlaka zinahitaji wenye taarifa za kina zinazoweza kuwasaidia wachunguzi wazilete taarifa hizo zikiwa detailed (hata kama kuna viambatanisho zaidi) ili wahusika/watuhumiwa wachukuliwe hatua stahiki

Unaweza kuweka bayana kwenye mjadala huu au kwa kututumia PM/DM au barua pepe sensitive@jamiiforums.com au uwasiliane na Waziri wa Afya (Waziri Ummy Mwalimu) kwa kumtumia DM kupitia mitandao ya Twitter au Instagram.

Ummy Mwalimu, MP (@umwalimu) | Twitter


Hata walio nje ya Mkoa wa Mbeya, tunapokea taarifa zao pia za Unyanyasaji na Rushwa ya Ngono katika Sekta ya Afya.

Asanteni sana

======

UPDATES

=======

JamiiForums imeyawasilisha kwa Mamlaka husika Malalamiko yaliyotolewa na Mdau wa JamiiForums kupitia hii thread hapa chini, Na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) wameshaanza kuyafanyia kazi.


Soma hapa: Tuhuma za rushwa ya ngono kwa madaktari bingwa Hospital ya Rufaa ya kanda Mbeya

Hatua zimeanza kuchukuliwa

03E420BA-8DDF-46B7-B844-25E0E5990D3D.jpeg
 
Sexual harassment ni tatizo sugu vyuoni na baadhi ya sekondari.

Kama kweli wameamua kuwa serious,wakubali kutoa vifaa maalum vya kurekodi sauti kwa siri.

Pia wakubali kuunda tume za kufuatilia inapojitokeza suala kama hilo.

Wakati mwingine hufanyika vitendo vya unyanyasaji tu ili binti ajiongeze. La asipojiongeza, ndo anaharibiwa maisha hivyo.

Kuna wengine wanafikia kukata tamaa ya kusoma, kutokana na kunyanyaswa kisaikolojia.Mambo haya ni ya kawaida sana ila nashangaa wenye mamlaka ndo wanajidai kustuka.

Nina mfano wa mtoto binti mmoja alikuwa akisoma sekondari moja Mwanza,tena ya kimisionari,aliliwa na mwalimu kisa alikuwa kapaka rangi ya kucha vidole vya miguuni.Bahati yake mbaya alikutwa hivyo akiwa anamwagilia maua. Ilikuwa achague adhabu ya suspension au kuliwa.

Kwa vile alikuwa amebakiza wiki mbili afanye mtihani wa kidato cha nne,aliamua tu isiwe taabu,maana hata aliyekuwa anamsomesha alikuwa mkali kama Simba, akajisalimisha nyumbani kwa mwalimu, kesi ikaisha
 
Dada wa Mbeya, Lete ushahidi wa tuhuma zako maana ni nzito mnoo.
Ule Uzi wa malalamiko ya huyo mwanafunzi wa mbeya ulipowekwa hapa nilishauri malalamikaji aende PCCB HQ lifanyiwe kazi haraka kuna mtu mmoja hapa akajifanya mjuaji kwamba asipeleke malalamiko yatafanyiwa kazi kutokea hapa, hovyo kabisa kuna majitu yanadhani yanajua kila kitu lakini hayaelewi, sasa Leo waziri anataka ushahidi upelekwe, lazima tujue kulalamika tu hakutoshi kuchunguza na kupata ushahidi bila kuwepo mlalamikaje!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akibadilishiwa Wizara leo maana yake project imeishia hapo hakuna sustainability katika mambo ya msingi, nilidhani mawasiliano yangeelekezwa kwenye anuani ya kitengo maalumu cha Wizara badala ya mtu binafsi ili hata kama waziri hayupo basi kazi inaendelea.
 
Mmmh, kuna watu watatumia hii kama mbinu ya kuwakomoa wabaya wao, ukimnyima mtu hela tu anatuma taarifa ya uingo juu yako, kuweni makini, na acheni kudemonise wanaume..
Ni kweli, panahitajika umakini hapa, tena sana, laa sivyo wanaume wanaweza wakawa waathirika wasio na hatia. I would advise anayeona hajatendewa haki awe anaenda mahakamani, mtuhumiwa akikutwa na hatia anachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchi na sheria za ajira yake.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dada wa Mbeya, Lete ushahidi wa tuhuma zako maana ni nzito mnoo.
Yule dokta intern wa mbeya hebu kuja pande hizi
Ule Uzi wa malalamiko ya huyo mwanafunzi wa mbeya ulipowekwa hapa nilishauri malalamikaji aende pccb HQ lifanyiwe kazi haraka kuna mtu mmoja hapa akajifanya mjuaji kwamba asipeleke malalamiko yatafanyiwa kazi kutokea hapa, hovyo kabisa kuna majitu yanadhani yanajua kila kitu lakini hayaelewi, sasa Leo waziri anataka ushahidi upelekwe, lazima tujue kulalamika tu hakutoshi kuchunguza na kupata ushahidi bila kuwepo mlalamikaje!

Sent using Jamii Forums mobile app
Baada ya kuona barua ya wizara ya afya, nikaja hapa kutafuta ule uzi wake, ila sijaupata sijui umefichwa wapi..

Huo uzi upandishwe tuushereheshe zaidi
uzi wa dada wa mbeya uliwekwa mpaka na majina ya wahusika mkaufuta, sasa sijui mnataka ushahidi gani? wa picha? au video?
Wakuu samahani sana kama mlikwazika.

Ukweli ni kwamba ule uzi sasa unafanyiwa kazi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) hivyo tutawaletea Mrejesho hapa hapa. Tunamshukuru Mwanachama wa JamiiForums kwa kuamua kuvunja ukimya kupitia Jukwaa hili. Ndio chanzo cha kuanzisha uzi maalumu ili taarifa zaidi ziletwe na mamlaka zizifanyie kazi.

Kwa mwenye wasiwasi kuwasiliana na Waziri Ummy Mwalimu, tunaomba utufikishie sisi, tutapeleka Mamlaka husika pia tutalinda faragha ya mtoa taarifa.

Kikubwa tupe taarifa iliyo kamili ya kuwezesha watuhumiwa kufikiwa. Ikiwa na vielelezo itakuwa vyema zaidi.

Jisikie huru kutoa taarifa bila ya kuogopa mtu wala kuonea mtu. Sauti yako itaokoa wengi.

Karibuni sana.
 
Inaonekana wewe unaguswa na hizi tuhuma itafika muda kitaeleweka tu
Ni kweli, panahitajika umakini hapa, tena sana, laa sivyo wanaume wanaweza wakawa waathirika wasio na hatia. I would advise anayeona hajatendewa haki awe anaenda mahakamani, mtuhumiwa akikutwa na hatia anachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchi na sheria za ajira yake.


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli, panahitajika umakini hapa, tena sana, laa sivyo wanaume wanaweza wakawa waathirika wasio na hatia. I would advise anayeona hajatendewa haki awe anaenda mahakamani, mtuhumiwa akikutwa na hatia anachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchi na sheria za ajira yake.


Sent using Jamii Forums mobile app
Sisi kama nchi tukiongozwa na kamanda mkuu tulishaacha kufuata sheria kiambo sana
 
Safi sana naona hili litawapa haki yao waathirika

Dunia hii imeharibika sana kwa sasa na kuomba ngono imekuwa kama haki ya mtu
Kama walivyokamatwa advert ya Craig’s list majuu


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom