Tutarajie haya baada ya kikao cha cc ya CCM

Tutarajie haya baada ya kikao cha cc ya CCM

Kwenye hiyo rasimu CCM wana mengi ya kupinga lakini kubwa ni la serikali tatu, hata mimi najiuliza hili suala la serikali tatu limechukuaje nafasi katika hii rasimu,ikiwa hayo ni maoni ya wananchi kwa uelewa wangu wa harakaharaka ni kuwa suala la serikali tatu linaweza kusemwa hasa na wanasiasa na baadhi ya wananchi wachache wenye uelewa wa mambo ya siasa, naamini wananchi walio wengi hili suala la serikali tatu kwao ni kama mazingaombwe,naamini kabisa kuwa hilo suala kwenye hiyi rasimu limeingizwa kisiasa na sio maoni ya wananchi walio wengi.......
 
KUNA MENGINE ZAIDI YA HAYO HAPO JUU:...NATABIRI lakini msiniite mchawi.......hii katiba mpya itakuwa na mgogoro sana kabla ya uchaguzi wa 2015......pia natabiri kama jamaa watakuja na hoja hizo hapo juu wananchi wataikataa katiba mpya!!! ni utabiri tu!

Shehe Yahaya kumbe aliacha wanafunzi wengi! Endelea kutabiri, Tanganyika itarudishiwa madaraka yake kamili lini?
 
Wakipinga utakuwa ni udhaifu mwingine wa Mwenyekiti wa CCM maana ndiye aliyemteua Jaji Warioba.
 
Kipindi hiki watahangaika sana lakini hawatashinda,waliowengi wamekwisha funguka kiakili,shule za kata zilisaidia japo kuna wengine wanazitharau hawajui kuwa kilichokosewa ni usimamizi wa serikali kupeleka waalimu na vitendea kazi tuu
 
Katika kikao chao lazima wapinge viti maalum,wapinge tume huru ya uchaguzi kutokuwa chini ya raisi,kupinga idadi ya wabunge kuwa hamsini,kupinga uwepo wa serikali tatu,,kupinga mambo ya kimahakama,kuwepo kwa mahakama ya juu kabisa,,katika katiba hii nadhani policcm watapunguza uuaji wa raia
Serikali Moja tu
 
Mimi kwa hili sitaki ushabiki wa vyama.Nataka nijue kwamba hivi ni kwa nini kama tunataka muungano tusiwe na serikali moja? Hebu fikiri;

1.Tuwe na wabunge wa tannganyika kila jimbo wawili (mwanamke na mwanaume)

2.Tuwe na wabunge wawili kwa kila jimbo la Znbar (mwanamke na mwanaume)

3.Tuwe na wabunge wawili wamuungano kutokata Tanganyika (mwanaume na mwanamke)

4. wabunge wawili wa muungano kutoka zanzbar (mwanamke na mwanaume)
5 mawaziri wa tanganyika na manaibu wao

6.Mawaziri wa zanzbar na manaibu wao

7.Mawaziri wa muungano na manaibu wao

8.Ikulu ya tanganyika

9.Ikulu ya zanzbar

10.Ikulu ya muungano

11.Uchaguzi wa Tanganyika, wa Zanzbar na wa Muungano.

Hivi gharama zote hizi ni kwa maslahi ya nani?Kwa nini tusiwe na serikali moja kama tunataka muungano! Tafakari.


ninaafikiana na mawazo yako. huu muungano umekuwa mzigo. ni aidha serikali moja au tusiwe na muungano kabisa
 
Hii kitu ya serikali 3 nina wasiwasi itamwacha Rais wa muungano kwenye mataa kama vile Gobachev na Perestroika yake!!!
 
Leo kamati kuu ya CCM inakutana kuijadili rasimu ya katiba. Baada ya kikao hicho tutarajie yafuatayo kuwa ndio maoni yao ya CCM
1)kupinga muundo wa serikali tatu na kupendekeza tuendelee na serikali mbili
2)kupinga matokeo ya urais kupingwa mahakamani
3)kupinga kufutwa kwa viti maalum
4)Tuendelee kuorodhesha na kujadiliana mapendekezo yote ambayo kuna uwezekana wa CCM kuyakataa, naomba kuwakilisha jamvini!

kwa kauli moja ccm itapinga tume huru ya uchaguzi. Kwa maoni ya ccm tume ya uchaguzi lazima iteuliwe na Mr. President bila ya kusikiliza ushauri kutoka kwa mtu yeyote kwa madhumuni yanayoeleweka vizuri na kila mtu.
 
Back
Top Bottom